Dokta Uchwara
JF-Expert Member
- Apr 29, 2022
- 1,371
- 3,146
Huyu anayeitwa Nape anaonekana ana uchungu sana na hii nchi. Sijui ndio uzalendo?
Nimekuwa nikimfuatilia tangu kipindi cha awamu ya nne alipokuwa anabwata majukwaani kwa matusi na mbwembwe za kisiasa.
Alipofyekwa na kuondolewa serikalini katika kipindi cha Magufuli, alionekana kujawa na ghadhabu pamoja na gubu kali lililopelekea kuunda genge la kumzodoa Rais wa nchi kwa masengenyo na umbea.
Ni kama vile anaamini yeye ni mtu mwenye sifa spesheli nchini ambaye anastahili kupewa madaraka ya kisiasa wakati wote.
Haamini kama yeye ni mtu wa kawaida kama watu wengine. Anaamini kuna kanafasi fulani nchini ambacho kapo kwa ajili yake siku zote katika hali yoyote.
Nataka kumjua vizuri huyu Nape.
Ametoka wapi? Chimbuko lake ni wapi?
Na kwanini siku zote anaamini ana nafasi spesheli kwenye hii nchi?
Nilisikia babaye alikuwa askari kanzu enzi hizo jeshini. Baadaye akadandia dandia ngazi akawa mwanasiasa.
Tofauti na unasibu huo na babaye, sijafahamu haswa huyu Nape kwanini anafikiri ana nafasi muhimu sana?
Nimekuwa nikimfuatilia tangu kipindi cha awamu ya nne alipokuwa anabwata majukwaani kwa matusi na mbwembwe za kisiasa.
Alipofyekwa na kuondolewa serikalini katika kipindi cha Magufuli, alionekana kujawa na ghadhabu pamoja na gubu kali lililopelekea kuunda genge la kumzodoa Rais wa nchi kwa masengenyo na umbea.
Ni kama vile anaamini yeye ni mtu mwenye sifa spesheli nchini ambaye anastahili kupewa madaraka ya kisiasa wakati wote.
Haamini kama yeye ni mtu wa kawaida kama watu wengine. Anaamini kuna kanafasi fulani nchini ambacho kapo kwa ajili yake siku zote katika hali yoyote.
Nataka kumjua vizuri huyu Nape.
Ametoka wapi? Chimbuko lake ni wapi?
Na kwanini siku zote anaamini ana nafasi spesheli kwenye hii nchi?
Nilisikia babaye alikuwa askari kanzu enzi hizo jeshini. Baadaye akadandia dandia ngazi akawa mwanasiasa.
Tofauti na unasibu huo na babaye, sijafahamu haswa huyu Nape kwanini anafikiri ana nafasi muhimu sana?