Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Sikiliza wewe gamba la kobe, hii ni open forum kwahiyo kila unachokiandika kinasomwa. Hata kama huna jipya utasomeka tu na huo utumbo unaouandika na ndio maana nikakushauri kuwa badilisha santuri badala ya kila post kurudia maneno yale yale. Kama unajiamini kuwa wewe wa uvichaaccm una akili unatakiwa kujenga hoja kulingana na muktadha na sio kukaririshwa maneno hayo hayo kila post kama vile ni zuzu.
Wewe vipi?. Ningekuwa sina jipya ungepoteza muda wako kujibu post isiyokuwa na jipya.
CCM tunaamini na kuishi katika demokrasia ambapo kuna kushinda na kushindwa kwa sababu katika hivyo, tunapata ujumbe kutoka kwa wananchi na katika ujumbe, tunaufanyia kazi.
Hatufanyi siasa za kibavicha ambazo wakishindwa wanasema wameibiwa kura na hawatambui ushindi hata kama mahakama itaamua vinginevyo.
Tutaendelea kuwafundisha maana ya demokrasia kama ilivyotokea katika uchaguzi wa urais 2010 ambao hamkumtambua Rais mchaguliwa lakini tukawapa somo la kidemokrasia ambalo liliwaingia mpaka mkaenda kunywa chai na juice state house na rais ambaye hamkumtambua.