Nape nauye asema UKAWA wasirudi bungeni

Nape nauye asema UKAWA wasirudi bungeni

Kama hawana njaa kwanini walisubiri posho itoke ndiyo waondoke bungeni?
Halafu eti mnajitia mnauchungu na hela ya mlipa kodi?!
Shame on you.
Hizo posho unazoziongelea zinalipwa kwa mwezi au siku?? Walienda pale kuwakilisha wananchi wao wanao waongoza ajabu CCM wanatumia kigezo cha POSHO kuwabeza UKAWA hali kwamba siku walizokuwa wakikaa kule ndani walikuwa wakiongelea msimamo wao na walipoona manyanyaso ya CCM na huo unao uita UCHUNGU wa hela ya mlipa kodi ndio ulio wafanya waondoke ili wasiendelee kuziharibu fedha hizo.

Vipi wangeondoka bungeni siku moja tuu kabla ya kupiga kura mngewaitaje?? Na CCM kama sio tamaa ya hizo posho kwa nn wanajiongezea siku za kuendelea kukaa bungeni wakati wanajua kwa kanuni zilizopo "KATIBA ITAKUWA BATILI MWISHO WA SIKU" sababu ya kutokutimia kwa mgawanyiko wa % ya wajumbe???

Yupi mlafi na yupi mchungu hapo??
 
Hizo posho unazoziongelea zinalipwa kwa mwezi au siku?? Walienda pale kuwakilisha wananchi wao wanao waongoza ajabu CCM wanatumia kigezo cha POSHO kuwabeza UKAWA hali kwamba siku walizokuwa wakikaa kule ndani walikuwa wakiongelea msimamo wao na walipoona manyanyaso ya CCM na huo unao uita UCHUNGU wa hela ya mlipa kodi ndio ulio wafanya waondoke ili wasiendelee kuziharibu fedha hizo.

Vipi wangeondoka bungeni siku moja tuu kabla ya kupiga kura mngewaitaje?? Na CCM kama sio tamaa ya hizo posho kwa nn wanajiongezea siku za kuendelea kukaa bungeni wakati wanajua kwa kanuni zilizopo "KATIBA ITAKUWA BATILI MWISHO WA SIKU" sababu ya kutokutimia kwa mgawanyiko wa % ya wajumbe???

Yupi mlafi na yupi mchungu hapo??

Siku waliyotoka ndiyo posho ilitoka, posho yote mpaka siku ya kuahirishwa kwa bunge la katiba, ilitoka saa tano, walipo sign tu na kuingia ndani ndiyo wakatoa tamko inamaana walikuwa wanasubiri itoke, wahuni hao.
Sasa wewe unafikiri ukawa wakitoka ndiyo shughuri za bunge la katiba zitasimama? Thubutu!!
Linaendelea tena August kwa siku 60 hata bila ukawa nyie endeleeni kuzurula mitaani.
 
Mjomba unapoambiwa kuwa bila ukawa katiba haiandikiki huelewi? Ama kweli sisiemu wamewafanya watu wao kama misukule. Yaani hata masuala ya kawaida mnashindwa kubaini. Sasa shughuli gani itaendelea na wakati ushasikia bila ukawa katiba haipo. Huna hata aibu?
 
Honey mimi sipendi siasa ila napenda amani!
PHP:
Sasa kuna kikaragosi kimoja toka
Hun mimi mtu wa bata nikae ndani kweli nisitoke kwa kuhofia vurugu kisa njaa na uroho wa madaraka ya watu wachache?
hahahahaaaa lol ukawa kilisema mbele ya camera eti bila serikali 3 hakutakuwa na amani, watachochea vurugu kama Kenya 2007!
hii post angu hun imenipa rahaaa...loh kwel bata la muhimuu:redface:
 
Siio UKAWA tu wote wasirudi. Ni kupoteza muda na pesa zetu. Bora kuendelea na katiba iliyopo mpaka tutakapokuwa tayari huko mbele. Kuna haja gani ya kula chakula ambacho hakijaiva sawasawa? Si utaumwa tumbo. Rasimu ya CCM ni kama chakula kibichi.
 
Hivi, sisiemu walikosa kabisa viongozi? Au haya ndo matokeo ya kurithishana madaraka kisa babako alikuwa kada? Huyo dogo anayepayuka hovyo ka mpigadebe akaisome tena sheria ya mabadiliko ya katiba juu ya namna ya kupitisha vifungu ndo ataujua umuhimu wa Ukawa. Kura zao ni muhimu mno japo ccm hawakiri waziwazi na hata jana kwenye mdahalo katibu wao wa visiwani alikiri hilo.
 
safi sana mkubwa unduzation umeleta shida ccm, wanajiona wao ndo kila kitu, zindukeni vijana mkaitapike hiyo sumu isije wazuru
 
Nape ni mbwatukaji mzuri kwani hamkumbuki ahadi zake kuondoa magamba ccm?magamba yapo au hayapo.?hayo ndio matokeo ya uropokaji.
 
Tatizo la nchi hii ni kila Kada wa Chama kutoa MATAMKO kana kwamba wana mamlaka ya kufanya hivyo! Nnauye anasema UKAWA wasirudi Bungeni; Makonda naye anasema vyake; Bulembo naye vyake na kadhalika na kadhalika. Katiba ni Sheria Mama kwa watanzania wote. Itakuwa ni jambo la ajabu sana kama watanzania tutakubali Katiba ya Chama fulani kuwa ndiyo Sheria Mama ya Tanzania!
 
hahahahaaaa lol ukawa kilisema mbele ya camera eti bila serikali 3 hakutakuwa na amani, watachochea vurugu kama Kenya 2007!
hii post angu hun imenipa rahaaa...loh kwel bata la muhimuu:redface:

I wish u could be here with me right now! Napenda raha hasa nikiwa na Mtoto mzuri kama wewe.
 
Honey mimi sipendi siasa ila napenda amani!
Sasa kuna kikaragosi kimoja toka ukawa kilisema mbele ya camera eti bila serikali 3 hakutakuwa na amani, watachochea vurugu kama Kenya 2007!
Hun mimi mtu wa bata nikae ndani kweli nisitoke kwa kuhofia vurugu kisa njaa na uroho wa madaraka ya watu wachache?
acha unafiki na lile dubu lililosema litaingia msituni mbona hulitaji we gamba tu
 
Katibu mwenezi wa CCM mh.Nape Nauye, amesema ukawa usirudi tena bungeni. Je, hii kauli yake ni sahihi?

Kabadilika juzi baada ya kikao cha cc na kusema bila ukawa mchakato utavurugika
 
Honey mimi sipendi siasa ila napenda amani!
Sasa kuna kikaragosi kimoja toka ukawa kilisema mbele ya camera eti bila serikali 3 hakutakuwa na amani, watachochea vurugu kama Kenya 2007!
Hun mimi mtu wa bata nikae ndani kweli nisitoke kwa kuhofia vurugu kisa njaa na uroho wa madaraka ya watu wachache?
Ikifika huo muda we nenda nchi za jirani ukale bata utuache WANAUME tujenge nchi yetu, halafu tutakuita uje kuendelea na bata wako na hata ngiri na kunguru ukitaka!
 
Mpaka August watakuwa na njaa sana posho zimeisha na zile hela walizopewa kutoka nje ili kuvuruga amani yetu watakuwa wamedhurumiana na kusambalatika, bunge likianza utawaona haoo mmoja mmoja wa kwanza lema labda wamfunge kamba

Rich Pol;

Wewe ni mnafiki,mwongo,mzushi na kizabinazabina!

Siku zote nimesema na nitaendelea kusema kuna Mijitu mitanzania ambayo imelishwa yamini na CCM ili kusema uongo na kupindisha ukweli kwa maslahi ya Chama Twawala! Hii ni kansa ambayo imekomaa na lazima ikomeshwe aidha kwa mionzi au kwa kukatwa!Tukikubana hapa sasa hivi ulete ushahidi wa HELA WALIZOPEWA UKAWA TOKA NJE utakuwa nao???Acha propaganda za kijinga pse!

CCM na wapambe wao wewe ukiwa mmojawapo,mmeshindwa kujenga hoja dhidi ya ukawa badala yake mnazungumzia watu. This is absurd and non-sense! Hoja hapa ni kwanini UKAWA waliamua kutoka nje ya BMK? Je, wewe kwa akili yako ndogo ulitaka UKAWA waendelee kukaa Bungeni ili kusikiliza matusi ya nguoni,kebehi, dharau, mipasho na vitisho???Wewe ulimsikia Bibi kizee Makame aliyesema, nanukuu:''Mimi sijaufyata, nimeufyatua. Jussa ndiye ameufyata maana hana mtoto lakini mimi nina watoto 3. Tena nataka nimwambie kule kwetu Pemba kuufyata manake ni MTU MWENYE BUSHA KULIWEKA KWA NYUMA.....'' mwisho wa kunukuu! Haya ni maneno ya aibu kabisa kuzungumzwa tena na mwanamke wa CCM mbele ya Wanaume kwenye chombo kikubwa kama hichi. Hii ni laana kwa CCM, na iko siku CCM mtalipia huu upuuzi wenu.

Turudi kwa mwendawazimu huyu anayeitwa NEPI. KATIBA mahali popote duniani kwenye nchi zinazojua maana ya Demokrasia ya kweli ni MARIDHIANO. NEPI anafikiri Katiba inaweza kupatikana hata UKAWA wasipokuwepo Bungeni, this is very very wrong!!!Nepi anatakiwa kukumbushwa kuwa KATIBA ni mali ya WANANCHI na hawa UKAWA ni sehemu ya Wananchi hawa Watanzania wanaotaka Katiba mpya. Yeye kwa akili yake ndogo kama ilivo yako anaweza kuona na kusema kama anavyoropoka kuwa UKAWA NI KIKUNDI CHA WAHUNI! Bwana Nepi anasahau kuwa nyuma ya UKAWA kuna mamilioni ya Watanzania ambao wanawaunga mkono hoja yao!!!

Kuwaita UKAWA kuwa kikundi cha WAHUNI ni kuwatukana Watanzania ambao mawazo na maoni yao ndiyo yamo kwenye RASIMU YA 2.Matamshi ya NEPI na Viongozi wengine wa CCM kina KINENA, LUKUVI,WASSIRA,MAKONDA,KOMBA na wengineo ni kuonyesha KIBRI na JEURI iliyopitiliza kwa kujiona kwamba wao ndiyo wana HAKI ya kusikilizwa mawazo yao ambayo hayamo hata kwenye hiyo Rasimu-2. Huu kama siyo wendawazimu ni kitu gani????

Mtu anasimama ndani ya BMK huku mishipa imemsimama na povu linamtoka anaanza kutukana na kuporomosha matusi kama vile amemeza kaseti ya matusi...... !Mwanamke mzima na heshima zake anataja mambo ya BUSHA Bungeni badala ya kujenga hoja ya kutetea Serikali 3 zilizopo kwenye Rasimu-2. Kuna huyu mwanamke mwingine anajiita Hawa Ghasia anasimama na bila aibu au soni anamwambia Mwenyekiti wa Tume ya Katiba- Jaji Joseph Sinde Warioba, AFUNGE MDOMO WAKE!!!Hawa Ghasia anaweza kweli kumwambia mtu wa makamo ya Baba yake au Babu yake afunge mdomo mbele ya hadhiri kama ile???? Huu kama si utovu wa nidhamu au laana tuuiteje???

Hivi Jaji Warioba na huyu Jike Hawa asiye na Adabu nani anatakiwa kumpa heshima mwenzake???Pengine nimkumbushe HISTORIA huyu mwanamke-haramu asiye na adabu kuwa Jaji Warioba amewahi kuwa MWANASHERIA MKUU, MSHAURI WA RAIS(WAKTI HUO BABA WA TAIFA MWL.NYERERE) na hatimaye kuwa WAZIRI MKUU nyadhifa ambazo huyu jike maaluni hawezi kuzipata hata kama ataamua kugawa URODA kama njugu!!!She will never ever climb to those positions!!

Lakini kwa vile CCM imewafanya Wabunge na Wafuasi wake kuwa kama UTAWALA WA KAMBARE kila mmoja ana sharubu, mtoto,jike na dume wote wana sharubu kwa hiyo hakuna mkubwa wala mdogo!!Kila mmoja ni msemaji wa Chama, Serikali, Ikulu au Jeshi na kila mahali!!!Hii yote inaonyesha kuwa CCM na Serikali yao wamepoteza haki ya kuongoza nchi hii sana sana kinachoendelea kuwaweka madarakani ni UFISADI,UDIKTETA,UBABE na VITISHO!
 
Amalizie kuwavua gamba wale alotumia pesa ya chama kuzunguka nchi akiwataka wajivue wenyewe wakikataa chama kitawavua. Akimaliza ndo aje kwa UKAWA.
 
Back
Top Bottom