mashikolomageni
JF-Expert Member
- Jan 5, 2010
- 1,570
- 193
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, ametangaza kiama cha walanguzi wa ufuta kwa kuitaka Serikali ya Wilaya ya Kilwa na Mkoa wa Lindi kuhakikisha inakomesha ulanguzi huo mara moja.
Aidha, amemtuhumu waziwazi mmoja wa wabunge, Mbunge wa Kilwa Kusini, Selemani Bungala `***** (B.we.g.e ili ni tusi) kuwa ni mmoja wa walanguzi, huku akimtaka arejee bungeni kuwawakilisha wananchi wake, badala ya kuwakandamiza kiuchumi.
Nape aliyasema hayo kwa nyakati tofauti katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika mji mdogo wa Kilwa Kivinje na Kilwa Masoko katika ziara ya siku mbili ya baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti ya CCM mkoani Lindi katika kufikisha ujumbe wa maamuzi ya NEC yaliyofanyika mjini Dodoma Aprili mwaka huu.
Kwa mujibu wa Nape wapo viongozi wa kisiasa wanaongoza dhuluma hiyo kwa kisingizio cha kuwasaidia wakulima wakati ukweli wanawadhulumu na kumshushia tuhuma hizo Mbunge wa jimbo hilo, *****(Bweg.e) kuwa ni kinara wa dhuluma hiyo.
Naambiwa Mbunge wenu bwana ***** (Bweg.e)kaacha Bunge la Bajeti na kuja kusimamia dhuluma yake dhidi ya wakulima masikini wa ufuta.
*****(Bweg.e) rudi bungeni kama hujui kazi yako ni kuwatetea wananchi, basi bora ujiuzulu
wananchi wapate mwakilishi na si mlanguzi alisema Nape.
Alisema wakati bei ya dira mwaka huu ni Sh 1,000 ambayo Serikali iliagiza mkulima alipwe yote ndio asubiri malipo ya pili ambayo nayo yatakuwa mazuri kwani bei ya ufuta safari hii ni nzuri, walanguzi wananunua ufuta kwa kati ya Sh 1,150 na Sh 1,200 ambayo ni wizi kwa
wakulima.
Akifafanua wizi huo Nape alisema, ushahidi wa wazi uliopo walanguzi wamechezea mizani yao na kwa kila kilo moja wanaiba kati ya robo na nusu kilo na hivyo bei ya Sh 1,200 wanayonunua walanguzi ni danganya toto kwani tayari wameshafidia kwenye mizani za wizi.
Mizani za vyama vyetu vya ushirika imepimwa na wakala wa vipimo hivyo ni sahihi na tayariS yenu imeshasimamia upatikanaji wa bilioni kumi na moja kutoka benki za NMB na CRDB kwa ya ununuzi wa ufuta msimu huu, hivyo hakuna sababu ya wakulima wa ufuta kuendelea kudhulumiwa na hawa matapeli, Alisisitiza Nape.
Alisema kuendelea kukwepa mfumo wa stakabadhi ghalani ni kwenda kinyume na maamuzi ya RCC, ambacho ni kikao halali na hata Baraza la Madiwani ambao ni wawakilishi halali wa wananchi.
Naambiwa wako na baadhi ya madiwani wa CCM wanaojihusisha na dhuluma hii, naagiza ushahidi ukipatikana vikao vya chama mchukue hatua kali dhidi yao, tuko tayari kufanya uchaguzi mdogo kuliko kuvumilia dhuluma hii, alisema Nape.
Mapema, Nape akizungumza na viongozi hao alieleza kwa kina lengo la hatma ya CCM kufanya mabadiliko kujivua gamba mjini Dodoma na kwamba moja ya malengo ni kukirejesha chama kwenye misingi yake ili kiweze kukidhi kwa dhati matarajio ya wananchi hasa wanyonge.
tatizo ni yeye kwenda hapo kusema kisha anapotea, kama ni wizi ni kweli kwa sasa watumishi wa umma na wawakilishi wa jamii katika mambo mbalimbali ni wapolaji
yeye anaposema arudi bungeni hali anamjua ni mlanguzi hiyo inatija kwa taifa kweli?
au ndio ana jijenga kisiasa kwa alimtaja mbunge mlanguzi?
ina maana NAPE anataka kuiambia jamaa leo kwamba ccm inakubaliana na wabunge walanguzi kuwa bungeni?
Hii stori nashindwa kuiamini vile.
Sehemu ya hii stori inadai Nape kumwita mbunge wa Kilwa as B.W.E.G.E, wakati huo huo kuna stori nyingine inadai kuwa Nape kawaliza watu na mbunge CUF kumshangilia. Sasa huyo anayeitwa B.W.E.G.E mbele ya constituents wake hapo hapo anamshangilia tena huyo aliyemtusi. Hainiingii kichwani hata kidogo, moja ya stori inatakiwa kurekebishwa.
Unategemea kwa nafasi yake kama kiongozi wa chama afanye nini? Yeye amemlipua na sasa ni juu ya wahusika kuchukua hatua za kuchunguza na kama kuna ushahidi kuchukua hatua. Hilo siyo jukumu la kiongozi wa chama cha siasa.
Hapa nimekukubali sana nape. Si wakati wote ni ushabiki wa kisiasa.KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, ametangaza kiama cha walanguzi wa ufuta kwa kuitaka Serikali ya Wilaya ya Kilwa na Mkoa wa Lindi kuhakikisha inakomesha ulanguzi huo mara moja. Aidha, amemtuhumu waziwazi mmoja wa wabunge, Mbunge wa Kilwa Kusini, Selemani Bungala `*****' (B.we.g.e ili ni tusi) kuwa ni mmoja wa walanguzi, huku akimtaka arejee bungeni kuwawakilisha wananchi wake, badala ya kuwakandamiza kiuchumi. Nape aliyasema hayo kwa nyakati tofauti katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika mji mdogo wa Kilwa Kivinje na Kilwa Masoko katika ziara ya siku mbili ya baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti ya CCM mkoani Lindi katika kufikisha ujumbe wa maamuzi ya NEC yaliyofanyika mjini Dodoma Aprili mwaka huu. Kwa mujibu wa Nape wapo viongozi wa kisiasa wanaongoza dhuluma hiyo kwa kisingizio cha kuwasaidia wakulima wakati ukweli wanawadhulumu na kumshushia tuhuma hizo Mbunge wa jimbo hilo, '*****'(Bweg.e) kuwa ni kinara wa dhuluma hiyo. "Naambiwa Mbunge wenu bwana '*****' (Bweg.e)kaacha Bunge la Bajeti na kuja kusimamia dhuluma yake dhidi ya wakulima masikini wa ufuta. *****(Bweg.e) rudi bungeni kama hujui kazi yako ni kuwatetea wananchi, basi bora ujiuzulu wananchi wapate mwakilishi na si mlanguzi" alisema Nape. Alisema wakati bei ya dira mwaka huu ni Sh 1,000 ambayo Serikali iliagiza mkulima alipwe yote ndio asubiri malipo ya pili ambayo nayo yatakuwa mazuri kwani bei ya ufuta safari hii ni nzuri, walanguzi wananunua ufuta kwa kati ya Sh 1,150 na Sh 1,200 ambayo ni wizi kwa wakulima. Akifafanua wizi huo Nape alisema, ushahidi wa wazi uliopo walanguzi wamechezea mizani yao na kwa kila kilo moja wanaiba kati ya robo na nusu kilo na hivyo bei ya Sh 1,200 wanayonunua walanguzi ni danganya toto kwani tayari wameshafidia kwenye mizani za wizi. "Mizani za vyama vyetu vya ushirika imepimwa na wakala wa vipimo hivyo ni sahihi na tayariS yenu imeshasimamia upatikanaji wa bilioni kumi na moja kutoka benki za NMB na CRDB kwa ya ununuzi wa ufuta msimu huu, hivyo hakuna sababu ya wakulima wa ufuta kuendelea kudhulumiwa na hawa matapeli," Alisisitiza Nape. Alisema kuendelea kukwepa mfumo wa stakabadhi ghalani ni kwenda kinyume na maamuzi ya RCC, ambacho ni kikao halali na hata Baraza la Madiwani ambao ni wawakilishi halali wa wananchi. "Naambiwa wako na baadhi ya madiwani wa CCM wanaojihusisha na dhuluma hii, naagiza ushahidi ukipatikana vikao vya chama mchukue hatua kali dhidi yao, tuko tayari kufanya uchaguzi mdogo kuliko kuvumilia dhuluma hii," alisema Nape. Mapema, Nape akizungumza na viongozi hao alieleza kwa kina lengo la hatma ya CCM kufanya mabadiliko ‘kujivua gamba' mjini Dodoma na kwamba moja ya malengo ni kukirejesha chama kwenye misingi yake ili kiweze kukidhi kwa dhati matarajio ya wananchi hasa wanyonge.
Huyu mbunge kama sikosei ni wa chama cha CUF kwa hiyo ndio maana kasema haya, kama angekuwa mwanamagamba mwenzake asingesema. Hana lolote vuvuzela huyo
Hapa nimekukubali sana nape. Si wakati wote ni ushabiki wa kisiasa.
sasa Nape amfanye nini? keshamwambia jamaa atajirekebisha na kuacha ulanguzi....kwa nini tunapenda sana kumshambulia Nape hata kwenye mazuri? kwazna badilisha tittle ya thread...iandike kiustaarabu acha jazba
Mkuu hapo kwenye Red akifika Masasi awaambie na wabunge wengine wanaofanya ulanguzi wa Korosho waache, asipofanya hivyo tutaona kamuonea huyo kwa sababu ni wa CUF
sasa Nape amfanye nini? keshamwambia jamaa atajirekebisha na kuacha ulanguzi....kwa nini tunapenda sana kumshambulia Nape hata kwenye mazuri? kwazna badilisha tittle ya thread...iandike kiustaarabu acha jazba