Nape, Mnyika, Mtatiro: Wapi Itikadi Zenu?

He might be a ccm but SIKILIZA hoja

Kwanza nakushukuru kaka Mchambuzi, hili ni jamboambalo ni la msingi sana, kuliongelea maana kwa sasa mimi naona ilivyo ni kama vile, pamoja na serikali kuongozwa na ilani ya chama tawala, lakini ukweli ni kuwa sehemu kubwa inaongozwa na priority za aliyeko madarakani, i mena raisi, ina maana regardless ni nani atakuwa raisi, ila akishika nchi vipaumbele vyake ndivyo vitakavyofanya kazi, that is why leo tumefika point nchi hii haieleweki ni ya kijamaa au ya kibepari ama ni mixed economy??!! (kama unajua unisaidie).

Nashukuru sana kwa mchango wako kwani unazidi kuhalalisha hoja yangu kwamba tuna tatizo kubwa la ki-tikadi, jambo ambalo linachangia sana umaskini wa walio wengi. Umeniuliza swali la msingi sana kwamba, Je Tanzania ni nchi inayofuata mfumo wa aina gani? Kijamaa? Kibepari? Mixed economy? Hili ni swali gumu, yet muhimu sana. Ugumu na umuhimu unatokana na ukweli kwamba, kwanza, ubepari katika jamii kubwa ya watanzania (vijijini), ni one way i.e. kuzalisha for exports to feed the global capitalist system; vilevile watanzania wengi (ambao ni vijijini) hawana uhusiano wa karibu sana na public sector, badala yake wana ukaribu karibu zaidi na NGO sector, na pia kwa mbali sana private sector. Pia vijijini suala la ‘market’ ni kama no- existence kutokana na uwepo wa subsistence economu, hivyo market forces don’t exist; na hata kungekuwepo na ‘market’, ingekuwa ni ‘market failure’.Ni kutokana an mvurugano huu ndio maana sitaweza kujibu swali lako, na badala yake kulijadili tu randomly (niwie radhi kwa hilo),kwani hakuna jibu rahisi. Hivyo naomba tusaidiane mawazo ili tupate jibu zuri.

Kwanza, Tanzania kama taifa, inafuata soko huria ambapo wananchi wanaathirika nalo either directly au indirectly, kutegemeana wanaishi wapi baina ya modern and subsistence sector. Na katika hili, tusisahau kwamba ‘soko’ ni kitu kilichokuwepo kwa karne nyingi hata kabla ya kuzaliwa ‘ubepari’. Kilichobadilishwa na ujio wa ubepari duniani ni aina tu ya soko, ambalo kwa sasa, tofauti na zamani, linaitwa ‘soko huria’.

Pili, kwa vile Tanzania ni nchi inayotegemea mataifa makubwa kwa misaada, sera zetu ni mchanganyiko wa zile za kihafidhiana, kiliberali, na Ujamaa wa demokrasia, kutegemeana na vyanzo vya misaada hiyo. Kwa mfano, misaada kutoka nchi kama Sweden,Norway ina leftist agenda na inaenda kwenye huduma za kijamii zaidi, while misaada inayotoka Marekani, Japan, na hata WorldBank au IMF, kwa kawaida inaenda kwenye maeneo ambayo wana amini yataleta economic growth (hata kama such a growth is not pro – poor). Vilevile, mchanganyiko wa sera hutokana na chama gani/itikadi ipi imekamata DOLA katika nchi kama UK, USA, na Ujerumani, ambao ni wahisani wakubwa sana wa Tanzania. Na mchanganyiko unazidi kushika kasi pale tunapobaini kwamba wakati CCM ni rafiki mkubwa wa vyama kama Labour (UK) na Democrats (US), Chadema ni rafiki mkubwa wa vyama kama Conservatives (UK) na Republicans (US, ingawa vyama hivi sio vya mrengo wa kati kama Chadema bali mrengo wa kulia. Vilevile CCM ni rafiki mkubwa wa Chama Cha Kikomunisti, China.

Kwa mtazamo wangu, njia nyingine ya kutusaidia ubaini mfumo gani Tanzania inaufuata ni kwa kuangalia vitu viwili:
Moja, Je wananchi walio wengi wanaishi katika mfumo upi? Maoni yangu ni kwamba, wapo katikati, na kote ni kubaya. Kwa upande mmoja, wanaumizwa na mfumo ule ule wa kikoloni wa kuwazalisha mazao ya mataifa matajiri (kahawa, chai, n.k), na pia kuwazalishia elites wa mjini (DSM etc) vyakula (mahindi, viazi, mchele), bila ya faida yoyote ya maana in return. Na kwa upande mwingine, hawafaidiki na mfumo wowote uliopo Tanzania (whether ni ubepari, mixed, n.k) kwa sababu ambazo nimezitaja kwa mfano, huduma za sekta binafsi na sekta ya umma kule vijijini ni kama hakuna, zaidi ya zile zinazotolewa na NGO sector, au zitokanazo na juhudi binafsi za wananchi wenyewe kama vile kujijengea nyumba, na madaraja ya ovyo ovyo, kuishi kwa kutegemea tiba za kienyeji, kujilisha chakula kwa kulima nyuma ya nyumba/uani, badala ya kutegemea exchange in the market, n.k.

Pili ni kuangalia, Je wananchi wengi wanaamini katika itikadi ipi. Kwa mtazamo wangu, wengi vijijini (ni muhimu tuangalie zaidi wa vijijini kwani ndio walio wengi Tanzania), watavutiwa zaidi na itikadi za mrengo wa kushoto kuliko wenzao wa mijini kutokana na ukweli kwamba – kwa hali zao duni, wanahitaji msaada wa serikali/sekta ya umma katika kila hali. Hili linachangiwa pia na ukweli kwamba viijiji havivutii sekta binafsi kuwekeza/kuendesha shughuli kibiashara. Isitoshe dhana ya ‘efficient allocation of resources’ chini ya soko huru inahimiza uwekezaji/mitaji kwenda kule tu panapozaa faida, na ni bayana kwamba vijijini suala la faida kwa mwekezaji halipo.

Kwa upande watanzania wanaoishi mijini, hawa kuna uwezekano wa kugawanyika kati ya wanao unga mrengo wa kushoto, mrengo wa kati na mrengo wa kulia. Lakini wengi wa wakazi wa mijini pia wana hali duni sana, Kwahiyo wao pia watavutiwa zaidi na itikadi na sera mrengo wa kushoto. Sakata la ongezeko la nauli za Kivuko cha kigamboni ni mfano mmoja wapo.
Niwie radhi kwa majibu yasiyokuwa na mpangilio wa maana, lakini natumai angalau inaweza kuweka msingi tuanzie wapi juu ya mjadala huu wa mfumo gani Tanzania inafuata n.k….
 
Mkuu Mchambuzi ni vigezo gani umetumia kumpa mtu kama Habib Mnyaa wa cuf eti yuko 5 bora ya wabunge? Huyu Mnyaa aliwakashifu sana wabunge wazalendo wa Chadema na Nccr waliokuwa wamesimama kidete kupinga mswada wa katiba ulioletwa bungeni.Tangu siku ile nilimpuuza huyu Mbunge.Kamwe kwake yeye hajui utaifa ni nini anachojua ni maslahi ya Zanzibar.Mnyaa yuko Tayari kutukana yeyote kama alivyofanya anapodhania kitumbua chake kinaguswa.Kwa msimgi huu ni kituko kusema Mnyaa wa Cuf naye ni mbunge bora

naelewa hoja yako vizuri sana, hawa kwa kuzingatia alivyopwaya katika mjadala wa katiba na Lissu wakati fulani. Nimekuwa namfuatilia siku nyingi katika bunge, sio hili la 2010 - hadi sasa; lakini cha kutizama hapa ni ukweli kwamba huyu mwenzetu yupo kwenye mapambano ya kudai their autonomy, and there is nothing noble than that;
 
Mkuu Mchambuzi ni vigezo gani umetumia kumpa mtu kama Habib Mnyaa wa cuf eti yuko 5 bora ya wabunge? Huyu Mnyaa aliwakashifu sana wabunge wazalendo wa Chadema na Nccr waliokuwa wamesimama kidete kupinga mswada wa katiba ulioletwa bungeni.Tangu siku ile nilimpuuza huyu Mbunge.Kamwe kwake yeye hajui utaifa ni nini anachojua ni maslahi ya Zanzibar.Mnyaa yuko Tayari kutukana yeyote kama alivyofanya anapodhania kitumbua chake kinaguswa.Kwa msimgi huu ni kituko kusema Mnyaa wa Cuf naye ni mbunge bora

naelewa hoja yako vizuri sana; pia alipwaya sana kwenye mjadala wa katiba na Lissu wakati fulani. Nimekuwa namfuatilia siku nyingi katika bunge, sio hili la 2010 - hadi sasa pekee, hata huko nyuma, na kwa wastani, amekuwa mbunge mzuri; lakini cha kutilia maanani zaidi hapa Molemo ni ukweli kwamba huyu mwenzetu yupo kwenye mapambano kudai their autonomy, and there is nothing noble than that;
 
Nitapita baadae kwani nahitaji muda kidogo kukusoma na kutafakari kabla kukupa maoni yangu kuhusu mada yako.

lakin kwa nilivyopitia haraka haraka nimegundua ni mada nzuri sana.
 
Ahsante Mchambuzi...
Labda kuweka kwenye mfumo wa swali, je nini hasa mapungufu ya itikadi ya "mlengo wa kiliberari wa kati na ujamaa wa demokrasia"?
Na je ni namna gani chama cha siasa kinaweza kubadili itikadi husika?
Labda jibu la maswali hayo linaweza kunogesha zaidi kwamba ni kwanini chama flani kifuate itikadi ipi na kwa njia gani.
Nipo hapa, ntarudi.
 
Ijue CHADEMA
Utangulizi

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama mbadala kinachokua na kinachoongozwa kwa Falsafa ya “Nguvu ya Umma” na kuamini katika itikadi ya “Mrengo wa Kati”. CHADEMA inawataka watanzania kuelewa kwamba mabadiliko ya kweli yataletwa na kubadilisha mfumo wa utawala. Maendeleo ya kweli hayawezi kuletwa na mafisadi walewale wa chama kile kile chenye uoza ule ule wakiendeleza yale yale kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. CHADEMA inatambua kwamba kwa falsafa ya Chukua Chako Mapema (CCM), Tanzania yenye neema kamwe haitawezekana. Lengo la CHADEMA ni kusimamia mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli ili kuunda Taifa la watu walio huru na lenye kuzingatia misingi ya utawala bora na linalotoa fursa kwa wananchi wake kushiriki katika kuboresha maisha yao. Tanzania endelevu, yenye haki na isiyovumilia ukandamizaji wa aina yeyote kwa wananchi wake-ndiyo nchi tunayoitaka. CHADEMA inafanya kazi kuhakikisha kuwa vyombo vya utawala na viongozi wanafanya maamuzi ya busara na makini yanayowaletea wananchi nafuu ya maisha na kuwapa matumaini ya kuendelea kupiga hatua za kimaisha katika nyanja zote za maendeleo.


Chama kimezinduliwa Upya?

Agosti 13, 2006 Chama cha Demokrasia na Maendeleo kilizinduliwa Upya. Ilikuwa siku ya kipekee na muhimu sana katika historia ya Chama.
arw1.gif
soma zaidi


Nini Falsafa ya Chama?

Falsafa ni fikra na mtazamo wa Chama ambayo ni kuamini katika “Nguvu na Mamlaka ya Umma” (The People’s Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni, na kuendeleza maamuzi, mawazo, rasilimali, uchumi na siasa ya nchi yao.
arw1.gif
soma zaidi



Chama kina Itikadi gani?

Itikadi ya Chama
  1. CHADEMA ni chama cha itikadi ya MRENGO WA KATI (center party).
  2. CHADEMA ni chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kutumia raslimali za nchi yetu bila kuathiri uhuru wa Taifa, na kuhakikisha kuwa umma kwa ujumla unanufaika na raslimali zao.
  3. CHADEMA inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa soko huru, utakaoheshimu na kulinda haki na mali za watu, biashara huru na sekta ya watu binafsi bila kupoka mamlaka ya umma katika maeneo nyeti hususani pale penye hitilafu ya soko au penye maeneo nyeti ya kiuchumi. Tunaamini katika soko huru sio soko holela.
  4. CHADEMA inaamini kuhakikisha matumizi bora ya raslimali asilia za nchi ili zichangie kikamilifu katika pato la taifa na hasa kuboresha huduma za kiuchumi zinazotumiwa na wananchi wote.
  5. CHADEMA inaamini katika uzalendo na kuthamini mila na desturi zetu zilizo nzuri.
  6. CHADEMA inaamini katika uhuru chini ya sheria zilizo za haki.
  7. CHADEMA inaamini katika siasa ambazo ziko juu ya vyama zenye kusimamia zaidi maslahi ya Taifa.
  8. CHADEMA inaweka umuhimu wa pekee katika familia kama moja ya taasisi muhimu ya kijamii.
  9. CHADEMA inaamini katika umuhimu wa uhuru wa kuamini katika kujenga maadili ya mwanajamii mmoja mmoja bila kuifanya dini kuwa sehemu ya dola.
  10. CHADEMA inaamini taifa linaundwa na watu, hivyo uhai wake unawategemea watu, na mabadiliko yake yanatokana na watu.
  11. CHADEMA inaamini katika kujenga uwezo wa wazawa katika kumiliki na kuendesha uchumi.
  12. CHADEMA inaamini kumiliki raslimali na mali miongoni mwa wananchi kunawapa uhuru zaidi hivyo tunataka kujenga chama na baadaye taifa lenye kutoa fursa, ambapo kila mtu bila kujali asili na hali yake anaweza kutimiza na kufanikiwa kadiri ya vipaji vyake.



Nini Falsafa ya Chama?

Falsafa ni fikra na mtazamo wa Chama ambayo ni kuamini katika “Nguvu na Mamlaka ya Umma” (The People’s Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni, na kuendeleza maamuzi, mawazo, rasilimali, uchumi na siasa ya nchi yao.
arw1.gif
soma zaidi


Kwa hiyo chambua hii useme mapungu ili Mhe Mnyika ayafanyie kazi.
 
Mchambuzi habari za leo,
Makala yako naona ililenga wana magamba zaidi na CUF amabao wanaunda serikali. Ni ukweli CCM ya leo haina itikadi kwani kilichopo kwenye katiba yao sio wanachokitenda.

Mzee Mchambuzi, mifumo ya na itikadi za vyama vya siasa zinatokana na wakati, mazingira , uchumi , utamaduni elimu na mwingiliano wa kijamii kiuchumi na kisiasa. Tanzania inahitaji mambo mengi yatkee kwanza kama elimu na kuimarisha uchumi. Hata hizo itikikadi ulizozitaja huwa haziko sawa kwenye kuziiishi au kuzitenda kati ya nchi na nchi. Na vilevile ni imani yangu kwamba mifumo ni ugunduzi na dunia haiwezi kusimama pale pale. Kama chama cha siasa kitakuja na mfumo unawork hakuna haja ya kucopy na kupaste hata yaliyoshindwa.

Matatizo ya kucopy na paste yalitufanya tukaangamia na siasa za ujamaa amabzo zilivyoshindwa bila ya sisi kuwa na formula tulijikuta katikati ya nja bila kujua tuendekao.

Tatizo kubwa la Tanzania sio mfumo ni katiba inayowajibisha wote pamoja na wanasiasa. Itikakadi haiwezi kutuletea maendeleo kama katiba yetu itaendelea kuwa ya kifalme. Tanzania ya leo bado haijajengeka watu kuweza kujikita kwenye itikadi zaidi. Ukisoma historia za vyama vikongwe duniani utaona walipitia matatizo mengi, kubwa zaidi matatizo ya kiuchumi huwamaliza uwezo wa kukumbatia imani, itikadi na ukada. Tanzania bado hatujafikia mbali sana bado wengi ni wanasiasa kwa sababu ya matumbo na mishahara.

Mpaka pale vikundi vitakapoaanza kutetea value zao ndipo itikadi dhabiti zitazaliwa. Leo ukisema unakuwa conservative Tanzania utakuwa wa nini, dini?, jamii, uchumi? au. Kwanza tuelimishe wananchi na tuendeleze nchi yetu.

CCM imeonyesha kupwaya kwa kiasi kikubwa sana imepoteza malengo pamoja na kuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 30 haijawa taasisi imara. Vyama kama CDM ina miaka 20 tu na inajijenga, nashindwa kuchelea kukuona hukutumia umakini mzuri kuingia kwenye mkumbo wa Mwenyekiti wako JK kusema CDM ni chama cha matukio/msimu. Nitakuuliza tena baada ya miaka 15 je hayo matukio yamekwisha?

Chama makini cha siasa lazima ki-connect na wapiga kura na usiasahau CDM inajijenga CCM inasambaratika kwani ilikuwa na mtandao nchi nzima. CCM imehodhi rasilima ilizozipata kifedhuli kutoka kwa wananchi wote kimtaji inamtaji mkubwa sana kulinganisha na vyama vingine kuvilinganisha unachekesha.

CDM inakuwa na inatikadi, CCM inakufa na imeacha misingi yake. CDM wakikenguhuka na kuacha misingi yake tutawauliza ila bado hawajashika dola. Ila kama ungekuwa unahudhuria mikutano ya CDM ungesikia wakitangaza sera na itikadi zao. Chama kipo kwa wananchi. Ukiona wanashinda serikali za mitaa ujue wapo kwa wananchi.

Mchambuzi wote ni mashahidi kuwa CDM inaenea kwa kasi sana, kwani imebeba ujumbe wa kumkomboa mnyonge na CCM inakufa kwani imebeba ujumbe wa kumlinda fisadi.

Huwezi kusema Ufisadi sio sababu ya kuiua CCM, unataka kuaminisha umma wizi, uzembe, hujuma, ukwepaji kodi, ufisadi, mikataba mibovu, viongozi wabovu sio sababu ya kufa kwa CCM? Haya yote yamesababisha kuacha kuzifuata na kuzisimamia sheria za nchi na chama chenu.

Umejaribu sana kuelezea mifumo ya dunia ila umeshindwa kuoanisha na hali na mahitaji halisi ya Mtanzania. kama unaona World bank na IMF haitufai hata mifumo iliyotoka kwao inaweza kuwa haitufai pia.
 
Nashukuru sana kwa mchango wako kwani unazidi kuhalalisha hoja yangu kwamba tuna tatizo kubwa la ki-tikadi, jambo ambalo linachangia sana umaskini wa walio wengi. Umeniuliza swali la msingi sana kwamba, Je Tanzania ni nchi inayofuata mfumo wa aina gani? Kijamaa? Kibepari? Mixed economy? Hili ni swali gumu, yet muhimu sana. Ugumu na umuhimu unatokana na ukweli kwamba, kwanza, ubepari katika jamii kubwa ya watanzania (vijijini), ni one way i.e. kuzalisha for exports to feed the global capitalist system; vilevile watanzania wengi (ambao ni vijijini) hawana uhusiano wa karibu sana na public sector, badala yake wana ukaribu karibu zaidi na NGO sector, na pia kwa mbali sana private sector. Pia vijijini suala la ‘market’ ni kama no- existence kutokana na uwepo wa subsistence economu, hivyo market forces don’t exist; na hata kungekuwepo na ‘market’, ingekuwa ni ‘market failure’.Ni kutokana an mvurugano huu ndio maana sitaweza kujibu swali lako, na badala yake kulijadili tu randomly (niwie radhi kwa hilo),kwani hakuna jibu rahisi. Hivyo naomba tusaidiane mawazo ili tupate jibu zuri.

Kwanza, Tanzania kama taifa, inafuata soko huria ambapo wananchi wanaathirika nalo either directly au indirectly, kutegemeana wanaishi wapi baina ya modern and subsistence sector. Na katika hili, tusisahau kwamba ‘soko’ ni kitu kilichokuwepo kwa karne nyingi hata kabla ya kuzaliwa ‘ubepari’. Kilichobadilishwa na ujio wa ubepari duniani ni aina tu ya soko, ambalo kwa sasa, tofauti na zamani, linaitwa ‘soko huria’.

Pili, kwa vile Tanzania ni nchi inayotegemea mataifa makubwa kwa misaada, sera zetu ni mchanganyiko wa zile za kihafidhiana, kiliberali, na Ujamaa wa demokrasia, kutegemeana na vyanzo vya misaada hiyo. Kwa mfano, misaada kutoka nchi kama Sweden,Norway ina leftist agenda na inaenda kwenye huduma za kijamii zaidi, while misaada inayotoka Marekani, Japan, na hata WorldBank au IMF, kwa kawaida inaenda kwenye maeneo ambayo wana amini yataleta economic growth (hata kama such a growth is not pro – poor). Vilevile, mchanganyiko wa sera hutokana na chama gani/itikadi ipi imekamata DOLA katika nchi kama UK, USA, na Ujerumani, ambao ni wahisani wakubwa sana wa Tanzania. Na mchanganyiko unazidi kushika kasi pale tunapobaini kwamba wakati CCM ni rafiki mkubwa wa vyama kama Labour (UK) na Democrats (US), Chadema ni rafiki mkubwa wa vyama kama Conservatives (UK) na Republicans (US, ingawa vyama hivi sio vya mrengo wa kati kama Chadema bali mrengo wa kulia. Vilevile CCM ni rafiki mkubwa wa Chama Cha Kikomunisti, China.

Kwa mtazamo wangu, njia nyingine ya kutusaidia ubaini mfumo gani Tanzania inaufuata ni kwa kuangalia vitu viwili:
Moja, Je wananchi walio wengi wanaishi katika mfumo upi? Maoni yangu ni kwamba, wapo katikati, na kote ni kubaya. Kwa upande mmoja, wanaumizwa na mfumo ule ule wa kikoloni wa kuwazalisha mazao ya mataifa matajiri (kahawa, chai, n.k), na pia kuwazalishia elites wa mjini (DSM etc) vyakula (mahindi, viazi, mchele), bila ya faida yoyote ya maana in return. Na kwa upande mwingine, hawafaidiki na mfumo wowote uliopo Tanzania (whether ni ubepari, mixed, n.k) kwa sababu ambazo nimezitaja kwa mfano, huduma za sekta binafsi na sekta ya umma kule vijijini ni kama hakuna, zaidi ya zile zinazotolewa na NGO sector, au zitokanazo na juhudi binafsi za wananchi wenyewe kama vile kujijengea nyumba, na madaraja ya ovyo ovyo, kuishi kwa kutegemea tiba za kienyeji, kujilisha chakula kwa kulima nyuma ya nyumba/uani, badala ya kutegemea exchange in the market, n.k.

Pili ni kuangalia, Je wananchi wengi wanaamini katika itikadi ipi. Kwa mtazamo wangu, wengi vijijini (ni muhimu tuangalie zaidi wa vijijini kwani ndio walio wengi Tanzania), watavutiwa zaidi na itikadi za mrengo wa kushoto kuliko wenzao wa mijini kutokana na ukweli kwamba – kwa hali zao duni, wanahitaji msaada wa serikali/sekta ya umma katika kila hali. Hili linachangiwa pia na ukweli kwamba viijiji havivutii sekta binafsi kuwekeza/kuendesha shughuli kibiashara. Isitoshe dhana ya ‘efficient allocation of resources’ chini ya soko huru inahimiza uwekezaji/mitaji kwenda kule tu panapozaa faida, na ni bayana kwamba vijijini suala la faida kwa mwekezaji halipo.

Kwa upande watanzania wanaoishi mijini, hawa kuna uwezekano wa kugawanyika kati ya wanao unga mrengo wa kushoto, mrengo wa kati na mrengo wa kulia. Lakini wengi wa wakazi wa mijini pia wana hali duni sana, Kwahiyo wao pia watavutiwa zaidi na itikadi na sera mrengo wa kushoto. Sakata la ongezeko la nauli za Kivuko cha kigamboni ni mfano mmoja wapo.
Niwie radhi kwa majibu yasiyokuwa na mpangilio wa maana, lakini natumai angalau inaweza kuweka msingi tuanzie wapi juu ya mjadala huu wa mfumo gani Tanzania inafuata n.k….
Mchambuzi, nadhani sio sahihi kuwaweka wakulima vijijini ktk Tanzania katika kapu moja kana kwamba ni 'homogenius', mkulima wa Mchichila kule Tandahimba anaye zungumzia milioni 50 mwishoni mwa msimu wa korosho hawezi kufanana na mkulima wa Manyoni anayesubiri chakula cha msaada, au mkulima wa Ludewa, songea, Rukwa anayenyimwa ruzuku ya mbolea huku anazuiwa kuuza mahindi yake nje ya nchi hafanani na mkulima wa kahawa wa Mbozi.
 
Ahsante Mchambuzi...
Labda kuweka kwenye mfumo wa swali, je nini hasa mapungufu ya itikadi ya "mlengo wa kiliberari wa kati na ujamaa wa demokrasia"?
Na je ni namna gani chama cha siasa kinaweza kubadili itikadi husika?
Labda jibu la maswali hayo linaweza kunogesha zaidi kwamba ni kwanini chama flani kifuate itikadi ipi na kwa njia gani.
Nipo hapa, ntarudi.

Nashukuru kwa mchango wako,
upo sahihi kwamba majibu kwa maswali haya yatatupatia mwongozo mzuri zaidi. Ningependa kukujibu kama ifuatavyo.

Uliberali:

Chama Cha CUF itikadi yak e ni Uliberali.
Mapungufu yaliyopo katika uliberali (kiuchumi) ni kwamba hupelekea inequality kati ya winners na loosers kutokana na forces za soko huria. Hili tatizo hutokea hata kwenye jamii zilizoendelea, hivyo kwa nchi kama Tanzania ambayo sio kwamba tu inafuata soko huria, bali soko huria kiholela, madhara yake yanaweza kuwa makubwa zaidi, hasa kutokana na ukweli kwamba watakao weza kushiriki kwa ukamilifu kwenye uliberali, chini ya soko huria ni wachache sana, kwani over 70% ya watanzania wapo vijijini, wakiendeleza shuguli zao katika subsistence sector/sekta isiyo rasmi. Hivyo itikadi hii katika Tanzania itajenga long term poverty, haitamwinua mtanzania wa kijijini hata siku moja, watabakia kama walivyo, if not worse. Ni kwa chama cha CUF (iwapo kitakamaat nchi) kulitambua hili, hivyo kuepuka kupandikiza uliberali, chini ya soko huria ‘holela' katika jamii ambayo tayari inaishi katika umaskini wa kutupwa, under the subsistence economy, ambao ni majority ya watanzania i.e. 70%.

Udhaifu mwingine, wa itikadi hii, pengine udhaifu muhimu kuliko yote, ni kwamba, itikadi hii inalea mfumo ule ule wa mataifa tajiri kunyonya mataifa maskini, kwani uliberali haujali tofauti za kiuchumi zilozopo baina ya nchi tajiri na nchi maskini, badala yake lengo kuu ni soko huria kwa nchi maskini, tena lisilo na mchujo. Mbaya zaidi ni kwamba, itikadi ya uliberali ina amini kwamba wadau wakubwa/taasisi kubwa za Maendeleo ya kimataifa kama vile WorldBank na IMF, wapo katika nchi zetu maskini kutokana na ukarimu wao, sio kibiashara zaidi, wakati ukweli wa mambo sote tunaujua juu ya madudu haya mawili ya IMF na WorldBank katika nchi maskini. Hawa wapo for self-interest, ni engine ya ukoloni mamboleo, ndio maana pamoja na uwepo wao katika nchi maskini kwa miaka zaidi ya 50 sasa, wameleta maafa kuliko mafanikio.

Demokrasia ya Kijamaa:

Kwa sasa hakuna chama chochote cha siasa Afrika kinachofuata itikadi hii. Itikadi ya Demokrasia ya Kijamaa ina mapungufu yake, lakini ukitazama kwa umakini, faida zake ni kubwa kuliko mapungufu yaliyopo, especially ikitumika katika nchi maskini kama Tanzania, au nchi nyingine yoyote inayoamua kuridhika na Maendeleo ya kiuchumi/pato la taifa, ili mradi wananchi wake wanapata huduma za msingi, kama nchi za Nordic/Scandavia. Nchi hizi haziendeshi sera zake kwa kushindana na mataifa mengine makubwa duniani in terms of ukubwa wa GDP. Kwa mfano, kuna criticism onthis ideology kwamba – serikali kuratibu uchumi ni kunapunguza ufanisi pamoja na ukuaji wa uchumi, na matokeo yake ni kuathiri GDP kwa kupunguza kasi ya ukuaji wake, tofauti na iwapo uchumi ukiachwa ujiendeshe wenyewe. Lakini tukiangalia kwa nchi kama Tanzania ambapo chini ya soko huria (holela), tumekuwa katika kundi la nchi bora duniani (top 30) kwa karibia miaka kumi, in terms of high and impressive GDP Growth rate – kwani since 2000, wastani wetu umekuwa karibia 7%. Ni kawaida kusikia wanasiasa wa CCM wakijisifia kwa hili. Lakini je, is this growth inclusive? Is it pro – poor? Au ni impressive growth kwenye makaratasi tu? Ukweli ni kwamba GDP growth yetu imeanza kuwa kubwa baada ya zoezi la chota chota ya Dhahabu kuanza kule migodini miaka ya mwishoni ya 1990s, madini ambayo hayana faida yoyote kwa mtanzania, kwani hayalipiwi kodi ya maana, pamoja na matatizo mengine chungu nzima yanayoletwa na sekta ya madini. Kwa mfano, Tukiondoa exports za gold katika equation ya GDP ya Tanzania na kubakisha sekta ya kilimo na sekta nyingina kama zilivyo, thamani na pia kasi ya kukua kwa GDP yetu itakuwa ya chini sana, pengine sawa na kiwango sawa na nyakati fulani fulani chini Nyerere/Ujamaa. Tutambue kwamba,n chi kama Sweden na nyingine zenye kufuata itikadi ya Ujamaa wa kidemokrasia kwa miaka mingi sana, hazina GDP value (in dollar terms), wala growth rates za kutisha kama mataifa mengine.

Lakini pamoja na haya, bado wananchi wa Sweden kwa mfano wapo ranked kama wananchi wenye maisha ya amani, furaha na quality ya hali ya juu kiuchumi na kijamii kuliko mataifa mengine yote duniani, kuliko hata wananchi kutoka mataifa tajiri (in terms of GDP), Top 5 duniani i.e in order of ranking - (USA, China, Japan, UK na France). Inabidi ifikie mahali nchi ijiridhishe kwamba lengo kuu ni kuwa na GDP growth ambayo ni inclusive/pro-poor, na yenye impact ya kweli katika maisha ya watu i.e. kuhudumia wananchi katika masuala ya msingi. Kwahiyo kutokana na haya, itikadi ya Ujamaa wa Kidemokrasia ina nafasi kubwa sana ya kuleta faida kubwa kuliko hasara kwa wananchi walio wengi Tanzania.

Critisism nyingine inayotolewa dhidi ya itikadi ya Ujamaa wa Kidemokrasia ni kwamba, kitendo cha serikali kutoa huduma za kijamii kama vile afya, elimu, n.k, bure, inawapunguzia wananchi – ‘individual choice' in the economy , kwa madai kwamba, wananchi lazima waachwe wajichagulie huduma wanayopenda chini ya sekta binafsi, na sio kulazimishwa na serikali. Ebu tutazame suala hili katika ya Tanzania. Tuna hospitali nyingi binafsi kwa mfano, kama vile Agha Khan, Hindu Mandal, Regency, Trauma Centre, TMJ, lakini je, under the argument of ‘individual choice', ni watanzania wangapi wana uwezo wa kwenda kwenye hospitali hizi? Ukweli uliopo ni kwamba, watanzania wengi wanategemea hospitali aidha za serikali, za NGOs, au waganga wa kienyeji. Ni kutokana na ukweli huu pia, itikadi ya Ujamaa wa kidemokrasia ina nafasi kubwa ya kutuleta faida kuliko hasara.

Na mwisho – Kuna hoja dhidi ya itikadi ya kidemokrasia, inayodai kwamba, chini ya mfumo huu, tabaka la wafanyakazi linaumia zaidi kuliko tabaka lingine lolote, kutokana na ukubwa wa kodi wanazotozwa katika mapato yao, huku matajiri wengi wakikwepa kodi hizo kwa ujanja mbalimbali. Critics wanadai pia kwamba, hali hupelekea utajiri wa nchi kujengwa na tabaka la wafanyakazi, kuliko na matajiri. Lakini ukweli unabakia wazi kwamba – nia ya itikadi hii ya Ujamaa wa kidemokrasia, hasa kuhusu progressive taxation i.e kutoza viwango vya kodi sambamba na ongezeko la kipato, lengo lake sio kupelekea hali hii wanayosema critics, na badala yake, kuisaidia tabaka la wafanyakazi kupata huduma zote za msingi za kijamii. Suala la msingi hapa ni kwa tabaka hili kujiridhia kwamba kodi wanayolipa inatoa huduma zenye thamani inayoendana na kodi hizo. Isitoshe, suala la kukwepa kodi kiujanja ujanja ni kubwa sana pia chini ya itikadi za mrengo wa kulia, hasa uhafidhiana (conservatism), ambapo ni jadi kwa matajiri wengi Marekani, Ufaransa, Ujerumani, n.k, kuanzisha charity organizations mbalimbali ambazo huwa ni vichaka vya kukwepa kodi. Hivyo, itikadi ya Ujamaa wa kidemokrasia, pamoja na mapungufu yake tuliyoyaona, ina nafasi ya kutuletea faida zaidi ya hasara sisi Watanzania, pengine kuliko itikadi ya sasa ya CCM (Ujamaa makaratasi, soko huria vitendo), Chadema (mrengo wa kati ambao una elements nyingi za uliberali na ambao hautambui mapungufu ya uliberali tuliyoyaona hapo juu), na pia itikadi ya CUF ya kiliberali ambayo mapungufu yake pia tumeyaona. Nitazidi kuchambua itikadi za vyama hivi kila nitakapopata nafasi.
 
Mchambuzi, nadhani sio sahihi kuwaweka wakulima vijijini ktk Tanzania katika kapu moja kana kwamba ni 'homogenius', mkulima wa Mchichila kule Tandahimba anaye zungumzia milioni 50 mwishoni mwa msimu wa korosho hawezi kufanana na mkulima wa Manyoni anayesubiri chakula cha msaada, au mkulima wa Ludewa, songea, Rukwa anayenyimwa ruzuku ya mbolea huku anazuiwa kuuza mahindi yake nje ya nchi hafanani na mkulima wa kahawa wa Mbozi.

Kimsingi nakubaliana na wewe, lakini tutambue kwamba almost 75% ya watanzania ajira yao ni kilimo, na majority ya hawa ajira yao ni kilimo sio kwa kupenda, bali kwa shingo upande, kwani hawana choice, na kilimo chao ni duni sana kwani mpaka amalize mchakato wa kupanda, kupalilia, kuvuna, na kuuza katika mazingira ya soko huria 'holela', faida yake ni ndogo sana. ndio maana uzalishaji umepungua kwani nguvu kazi kwenye sekta hii imekata tamaa na imekimbilia mijini. Hao waliojiajiri kwenye kilimo kwa kupenda ni kweli wapo, lakini ni wachache ukifananisha na wale wasio kuwa na choice nyingine katika mfumo wa uchumi ulipo sasahivi. Ni kundi hilo ndilo nilikuwa ninalijadili.
 
Mchambuzi habari za leo,
Makala yako naona ililenga wana magamba zaidi na CUF amabao wanaunda serikali. Ni ukweli CCM ya leo haina itikadi kwani kilichopo kwenye katiba yao sio wanachokitenda.

Mzee Mchambuzi, mifumo ya na itikadi za vyama vya siasa zinatokana na wakati, mazingira , uchumi , utamaduni elimu na mwingiliano wa kijamii kiuchumi na kisiasa. Tanzania inahitaji mambo mengi yatkee kwanza kama elimu na kuimarisha uchumi. Hata hizo itikikadi ulizozitaja huwa haziko sawa kwenye kuziiishi au kuzitenda kati ya nchi na nchi. Na vilevile ni imani yangu kwamba mifumo ni ugunduzi na dunia haiwezi kusimama pale pale. Kama chama cha siasa kitakuja na mfumo unawork hakuna haja ya kucopy na kupaste hata yaliyoshindwa.

Matatizo ya kucopy na paste yalitufanya tukaangamia na siasa za ujamaa amabzo zilivyoshindwa bila ya sisi kuwa na formula tulijikuta katikati ya nja bila kujua tuendekao.

Tatizo kubwa la Tanzania sio mfumo ni katiba inayowajibisha wote pamoja na wanasiasa. Itikakadi haiwezi kutuletea maendeleo kama katiba yetu itaendelea kuwa ya kifalme. Tanzania ya leo bado haijajengeka watu kuweza kujikita kwenye itikadi zaidi. Ukisoma historia za vyama vikongwe duniani utaona walipitia matatizo mengi, kubwa zaidi matatizo ya kiuchumi huwamaliza uwezo wa kukumbatia imani, itikadi na ukada. Tanzania bado hatujafikia mbali sana bado wengi ni wanasiasa kwa sababu ya matumbo na mishahara.

Mpaka pale vikundi vitakapoaanza kutetea value zao ndipo itikadi dhabiti zitazaliwa. Leo ukisema unakuwa conservative Tanzania utakuwa wa nini, dini?, jamii, uchumi? au. Kwanza tuelimishe wananchi na tuendeleze nchi yetu.

CCM imeonyesha kupwaya kwa kiasi kikubwa sana imepoteza malengo pamoja na kuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 30 haijawa taasisi imara. Vyama kama CDM ina miaka 20 tu na inajijenga, nashindwa kuchelea kukuona hukutumia umakini mzuri kuingia kwenye mkumbo wa Mwenyekiti wako JK kusema CDM ni chama cha matukio/msimu. Nitakuuliza tena baada ya miaka 15 je hayo matukio yamekwisha?

Chama makini cha siasa lazima ki-connect na wapiga kura na usiasahau CDM inajijenga CCM inasambaratika kwani ilikuwa na mtandao nchi nzima. CCM imehodhi rasilima ilizozipata kifedhuli kutoka kwa wananchi wote kimtaji inamtaji mkubwa sana kulinganisha na vyama vingine kuvilinganisha unachekesha.

CDM inakuwa na inatikadi, CCM inakufa na imeacha misingi yake. CDM wakikenguhuka na kuacha misingi yake tutawauliza ila bado hawajashika dola. Ila kama ungekuwa unahudhuria mikutano ya CDM ungesikia wakitangaza sera na itikadi zao. Chama kipo kwa wananchi. Ukiona wanashinda serikali za mitaa ujue wapo kwa wananchi.

Mchambuzi wote ni mashahidi kuwa CDM inaenea kwa kasi sana, kwani imebeba ujumbe wa kumkomboa mnyonge na CCM inakufa kwani imebeba ujumbe wa kumlinda fisadi.

Huwezi kusema Ufisadi sio sababu ya kuiua CCM, unataka kuaminisha umma wizi, uzembe, hujuma, ukwepaji kodi, ufisadi, mikataba mibovu, viongozi wabovu sio sababu ya kufa kwa CCM? Haya yote yamesababisha kuacha kuzifuata na kuzisimamia sheria za nchi na chama chenu.

Umejaribu sana kuelezea mifumo ya dunia ila umeshindwa kuoanisha na hali na mahitaji halisi ya Mtanzania. kama unaona World bank na IMF haitufai hata mifumo iliyotoka kwao inaweza kuwa haitufai pia.

Asante sana kwa mchango wako mzuri. Naomba nijibu hoja zako kama ifuatavyo:
1. Hoja zangu zimelenga vyama vyote kwani udhaifu wa itikadi upo katika vyama vyote vikubwa vilivyopo. Sijui kwanini haulioni hilo, especially ukweli kwamba ni mara chache sana kusikia idara za uenezi zikitoa elimu kwa umma juu ya itikadi za vyama vyao tofauti na vyama vingine vilivyopo, badala yake CCM, CDM, kwa mfano, siasa zao ni kuhusu katiba na ufisadi. Je, tusema haya yanapatiwa ufumbuzi by 2014, CDM na CCM vitakuwa vinashindania nini? Au CDM banks on the idea kwamba CCM haitajirekebisha katika hayo? Sikumsikia JK akizungumza kuhusu siasa za msimu, lakini kauli hiyo sio ya ajabu, ila ingetoka kwa mtu mwingine, sio yeye ambae hata chama chake hakina dira kwa miaka 20 sasa, na badala yake kinapeta kutokana na mazoea pamoja na hulka/personalities za baadhi ya viongozi ambao wakihama tu, wameondoka na personalities zao. Nilimsikia Dr. Slaa wiki kadhaa zilizopita akitamka kwamba lengo kuu la Chadema ni kuikosoa serikali, na serikali ikijirekebisha, Chadema itaishiwa hoja. Hili lilinishangaza sana, na ndio udhaifu ninao uzungumzia.

2. Kuhusu suala la copy and paste - sijasisitiza hilo, bali umuhimu wa kuangalai itikadi zilizopo duniani, kubaini strengths and weakness mbali mbali then determine nini ni kizuri kukitumia katika mazingira yetu. Jibu langu kwa Joune Gwali )see post 29 of this thread) limefafanua kidogo suala hili. Vinginevyo pamoja na ukweli kwamba suala la copy and paste ni suala la hatari, lakini sio hatari zaidi kama suala la kujaribu to reinvent the wheel, ' kitu ambacho kama nakusoma vizuri, unajaribu kupendekeza in the context of our society - choice ya aina za politics na itikadi, in particular.

3. Kimsingi nakubaliana na wewe kwamba CDM imezidi kukomaa over the years, but this success remains fragile kwani mafanikio yake yanatokana zaidi na CDM kuikosoa CCM, wakati nia yao wana amini kwamba wanaweza kutekeleza sera za IMF na WorldBank better, kwani uliberali (elements of which pia zipo katika itikadi ya CDM ya mrengo wa kati), uliberali una amini kwamba hawa ni mama tereza kwa nchi maskini. Sitasahau kauli yako leo kwangu kwamba nisubiri baada ya miaka 15 nitaona CDM imefanikiwa vipi, lakini pia na mimi naomba nikuambie kwamba, subiri pale CDM itakapochukua nchi, e.g. 2015 ili kwenda kutekeleza sera za uliberali/soko huru kwa ufanisi zaidi ya CCM, itachukua miaka michache sana kwa wananchi kuona CDM ilikuwa blah blah, wakati kumbe ukweli ni kwamba inawezekana wana nia nzuri lakini hawawezi kuleta lolote tofauti kwa mtazamo wao wa sasa (wenye elements za uliberali), ambao unaamini kwamba IMF na World Bank ni mama tereza kwa nchi maskini, badala ya kuwaona hawa kama ni kikwazo kikubwa cha kuinua wananchi maskini. In short, wananchi wanaweza kuiweka CDM madarakani 2015, lakini ni upuuzi wa WorldBank na IMF ndio utawafanya wananchi hao hao kuona kumbe CDM nao sio kitu, hivyo kukiondoa CDM madarakani, pengine in 5 to 10 years.

4. Kuhusu mimi kushindwa kuweka mifumo ya kidunia in practical terms - kwa Tanzania, nilichofanya ilikuwa ni kuanzisha tu mjadala na nika ahidi kuchambua zaidi mada hii in the context of political practicalities za Tanzania. Nimeanza kufanya hivyo katika post 29 ya thread hii, na nitaendelea.

Ni hayo tu kwa sasa.
 
point yangu ni kuwa,hapa kuna point nzuri na ya nsingi sana ambayo sote nivyema tuijadili. nitafurahi nikiwaona hapa kwa ID zao watu kama Zitto, Mnyika, Nape, Kigwangala, Mtatiro, Waberoya. Kiranga, Mwita, na wadaue mbalimbali wa siasa tuwasikie pia majibu yao.

Ingekuwa vizuri wangefanya hivyo, hasa Nape, Mnyika, Zitto, Mtatiro na Kigwangala lakini silioni wao kuja humu kwa majina yao, pengine kwa ID tofauti. Hata hivyo, kutokushiri kwao sio kikwazo cha madhumuni yetu, kwani kama walivyokuwa wao, sisi pia ni sehemu ya taifa hili, tena tuliopo 'kule site'; Mijadala kama hii ni muhimu kutufanya sisi na wenzetu tunaokunywa nao kahawa na kashata, become more informed kisiasa, hivyo kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanya maamuzi bora zaidi ya kisiasa.

Otherwise suala la udhaifu wa itikadi kwa CCM, CHADEMA, CUF, ni suala lililo wazi, kama nilivyokwisha ainisha, na sioni viongozi hao uliowataja wakija humu watajenga vipi hoja zenye mashiko kupingana na ukweli huo, wakifanya hivyo, nitazidi kutoa ufafanuzi, kwani nina mengi sana ya kueleza lakini lazima yawe triggered na hoja za wadau wengine. Kutokana na ukweli juu ya udhaifu huu, ni bora wawe tu observes, lakini kama wataamua kuingia humu, basi wajikite zaidi kuhusu the way forward ili kuondoa udhaifu huu wa ki-itikadi. Lakini iwapo wataamua kujiunga na mjadala kwa kupinga hoja hii, my response will be a merry chase i.e. 'quick and energetic'.
 
Mchambuzi habari za leo,
Tatizo kubwa la Tanzania sio mfumo ni katiba inayowajibisha wote pamoja na wanasiasa. Itikakadi haiwezi kutuletea maendeleo kama katiba yetu itaendelea kuwa ya kifalme. Tanzania ya leo bado haijajengeka watu kuweza kujikita kwenye itikadi zaidi. Ukisoma historia za vyama vikongwe duniani utaona walipitia matatizo mengi, kubwa zaidi matatizo ya kiuchumi huwamaliza uwezo wa kukumbatia imani, itikadi na ukada. Tanzania bado hatujafikia mbali sana bado wengi ni wanasiasa kwa sababu ya matumbo na mishahara.

Mpaka pale vikundi vitakapoaanza kutetea value zao ndipo itikadi dhabiti zitazaliwa. Leo ukisema unakuwa conservative Tanzania utakuwa wa nini, dini?, jamii, uchumi? au. Kwanza tuelimishe wananchi na tuendeleze nchi yetu.

Suala la katiba na itikadi ni simple logic: Katiba ya aina yoyote ile haiwezi kuja kabla ya uwepo wa itikadi katika jamii; Itikadi hutangulia kwanza, ndipo katiba hufuatia; this is true whether katiba in question ni katiba ya ya NGO, Chama Cha Siasa au Katiba ya nchi; Hii ni kwa sababu kuu moja tu, kwamba: Itikadi ni mtazamo, mwongozo, value system, spirit ya taifa, around which matukio na matendo yote ndani ya jamii revolves, hivyo kuimarisha maana, mwelekeo, na tafsiri ya masuala mbali mbali ya ulimwengu, kwa jamii husika. Jamii isiyojitambua ki-itikadi ni jamii legelege, na jamii ya namna hii haiwezi kuzaa Katiba nzuri ya nchi. Ndio maana katika hali ya sasa (tofauti na miaka ya zamani), watanzania wengi wapo katika kuchanganyikiwa ki-itikadi (rejea definition ya itikadi hapo juu), kwani kwani their value system, national spirit, world view n.k. imekuwa interrupted na ujio wa mageuzi ya kiuchumi na kisiasa, na mbaya zaidi ni kwamba taasisi muhimu katika jamii (vyama vya siasa, taasisi za elimu, n.k), hazikuingilia mapema kutoa mwongozo jinsi gani ya kuyapokea mageuzi haya. Ndio maana hata katika mchakato wa katiba mpya, wananchi wanahitaji guidance ya hali ya juu, vinginevyo watajikuta wanaunda taifa lisiloendana na mtazamo, value system, beliefs, national spirit, na matarajio yao. Vilevile ni muhimu kutambua kwamba itikadi sio zao la chama cha siasa bali ni zao la jamii; hivyo, itikadi ya chama cha siasa ni reflection ya mitazamo, value systems, matarajio, na national spirit iliopo katika jamii husika (na sio kinyume chake). Kwahiyo, kwa kuzingatia maana na umuhimu wa 'itikadi', ni lazima itikadi itangulie kwanza kabla ya chama cha siasa, kabla ya katiba ya chama cha siasa, na hata kabla ya katiba ya nchi (kama lengo nikupata katiba nzuri), kwani ni itikadi ndiyo inayo feed katika maeneo haya yote.
 
@mchambuzi

one: Nini hasara ya itikadi ya conservative inayofuatwa na chadema?

two: unafikiri kipi kianze uongozi bora au itikadi bora?
 
@mchambuzi

one: Nini hasara ya itikadi ya conservative inayofuatwa na chadema?

two: unafikiri kipi kianze uongozi bora au itikadi bora?

Asante kwa maswali yako mazuri yenye kuchangamsha mjadala.

Kwanza naomba nisisitize na kuweka mkazo kwamba - Chadema sio Chama cha Conservatives (wahafidhiana). Hakisemi hayo katika katiba yake. Itikadi ya Chadema ni ya Mrengo wa Kati, na awali nilifafanua itikadi hii inasimamia vitu gani. Sijafanya bado uchambuzi wa kina juu ya udhaifu wa itikadi hii katika mazingira ya Tanzania. Lakini nipo tayari kufanya hivyo iwapo itahitajika. Vinginevyo nilitoa tu dondoo za juu juu.

Kwahiyo naomba tuwekane sawa kwamba Chadema sio chama cha wahafidhiana/conservatives. Lakini pia tutambue kwamba Chadema kina vyama marafiki na washirika huko nje, kama ilivyokuwa CCM, na CUF. Vyama marafiki na washirika wakubwa wa Chadema ni vyama vinavyofuata itikadi ya uhafidhiana/Conservative parties, kwa mfano Conservative Party (UK), Republican Party (USA) na kile cha Ujerumani; Lakini CCM nao wana marafiki na washirika wake wengi huko nje, hasa vyama vyenye itikadi za mrengo wa kushoto kati na pia vile vyenye itikadi ya kushoto (kwa ufafanuzi wa mirengo hii, rejea my original post), kwa mfano Labour Party (UK), Democrat Party (USA), Social Democratic Party (Sweden), Communist Party (Cuba), Communist Party (China) na ANC (South Africa).

Baada ya kuwekana sawa katika hayo, sasa naomba nijibu swali lako kuhusu hasara ya itikadi ya conservatives kama ifuatavyo, huku msisitizo ukiwa kwamba – Chama Cha Chadema hakina uhusiano na mambo haya.
1. Itikadi ya conservatives haijali hali za wananchi wa kada ya chini/maskini. Sera chini ya itikadi hii huwa zinazidisha pengo baina ya watu maskini na matajiri. Nilishajadili hili kidogo hapo awali.

2. Itikadi ya conservatives ina impose moral standards kwenye jamii based on UDINI, mfano vyama vya Republican (Marekani), Conservatives (UK), na Ujerumani. Naomba hapa turejee kidogo kwenye maana ya ‘conserve' – maana yake ni ‘kuhifadahi' Kwahiyo itikadi hii lengo lake kuu ni kuhifadhi yale ya kale, ikiwa ni pamoja na taasisi, mila, desturi, imani, n.k ambazo zimeota mizizi mirefu katika jamii. Pia ni muhimu nikasema hili – iwapo wimbi la mageuzi ya kisiasa litazidi kushika kasi kule North Africa and Middle East, hivyo kupeleka mfumo wa vyama vingi, vyama hivi vikuu lazima vitafuata itikadi ya Conservatism, ambazo, kama katika jamii za ulaya na marekani, itikadi hizi huko middle east nazo zita impose moral standards kwenye jamii based on UDINI. Kwa mfano, Misri inaelekea huko chini ya chama cha Muslim Brothers.

3. Na mwisho, itikadi ya conservatives inabagua jamii nyingine kama vile watu weusi, wahindi, waarabu n.k, lakini wakibanwa juu ya hilo wanadadi kwamba hufanya hivyo kwa nia yaku preserve traditional values zao. Wazungu conservatives ni mabingwa katika hili, lakini pia hili litatokea katika nchi za middle east na uarabuni iwapo mfumo wa vyama vingi utaingia. Tofauti na waafrika, Wazungu na Watu wa Middle East huthamini na kutunza sana mila, tamaduni na desturi zao, ki-itikadi na pia kiutekelezaji.

Kuhusu umuhimu baina ya Itikadi Bora na Uongozi Bora

Hili ni swali zuri sana. Lakini kama nilivyoeleza kwenye mjadala wangu wa awali (rejea post number 33 hapo juu), itikadi ni kitu cha mwanzo kabla ya kitu kingine chochote. Masuala kama vile kipimo cha uongozi bora, aina za siasa kufuata, katiba ya nchi iwe ya namna gani, n.k, ni matokeo ya itikadi. Kwani tuliona kwamba itikadi ni: "mtazamo, mwongozo, value system, spirit ya taifa, around which matukio na matendo yote ndani ya jamii revolves, hivyo kuimarisha maana, mwelekeo, na tafsiri ya masuala mbali mbali ya ulimwengu, kwa jamii husika."

Jamii yenye itikadi legelege huzaa viongozi legelege, hivyo huwa na vyama legelege, siasa legelege, na katiba ya nchi legelege.
 
@mchambuzi

Asante kwa majibu utaona kuwa katika kila itikadi kuna mapungufu yake kama ulivyosema; kwa maana hiyo itikadi unayotaka kila chama iweke wazi si kitu ya maana kama "uongozi" bora..

Kama umesoma historia ya uongozi (leadership trends and history) utagundua kuwa itikadi si msingi hasa wa taifa kuendelea kwasababu itikadi haijali "situations na time" wakati leadership inaangalia situation and time..

Kwangu mimi tusihangaike sana na itikadi ya vyama, (by the way si lazima vyama ndio vitoe viongozi), tuhangaike na namna bora ya kupata viongozi bora wanafanana na situation tuliyonayo; kwani viongozi wetu enzi hizo chiefs walikuwa na itikadi gani????

Mkuu cha muhimu kwenye taifa hili si vyama na itikadi zao ni katiba yenye kutoa fursa ya kuchaguliwa kiongozi bora pengine ambaye si lazima hatokane na vyama vya siasa (na itikadi) zao bali na uwezo wake wa kuchambua yafuatayo na kutoa solutins accordingly??

a. Nini mahitaji ya wananchi ili kuendelea; haki na usawa, kazi na heshima mbele ya jamii, etc

b. Nini mahitaji ya wakati; internal na external challenges na namna bora ya ku-strike to win national interest

Mengine kama itikadi ni redudancy na obselete kwa maisha ya watu; ni mambo ya wanasiasa na elites kutafuta difficult terminologies kuonyesha kwamba siasa ni kwa ajili ya watu fulani fulani wenye ufahamu fulani wa itikadi etc..blah blah.

Bottom line ni kwamba itikadi haina maana zaidi slogans, elites and politicians world of complexity in essence tunahitaji "KIONGOZI" na siyo itikadi
 
@mchambuzi

Asante kwa majibu utaona kuwa katika kila itikadi kuna mapungufu yake kama ulivyosema; kwa maana hiyo itikadi unayotaka kila chama iweke wazi si kitu ya maana kama "uongozi" bora..

Kama umesoma historia ya uongozi (leadership trends and history) utagundua kuwa itikadi si msingi hasa wa taifa kuendelea kwasababu itikadi haijali "situations na time" wakati leadership inaangalia situation and time..

Kwangu mimi tusihangaike sana na itikadi ya vyama, (by the way si lazima vyama ndio vitoe viongozi), tuhangaike na namna bora ya kupata viongozi bora wanafanana na situation tuliyonayo; kwani viongozi wetu enzi hizo chiefs walikuwa na itikadi gani????

Mkuu cha muhimu kwenye taifa hili si vyama na itikadi zao ni katiba yenye kutoa fursa ya kuchaguliwa kiongozi bora pengine ambaye si lazima hatokane na vyama vya siasa (na itikadi) zao bali na uwezo wake wa kuchambua yafuatayo na kutoa solutins accordingly??

a. Nini mahitaji ya wananchi ili kuendelea; haki na usawa, kazi na heshima mbele ya jamii, etc

b. Nini mahitaji ya wakati; internal na external challenges na namna bora ya ku-strike to win national interest

Mengine kama itikadi ni redudancy na obselete kwa maisha ya watu; ni mambo ya wanasiasa na elites kutafuta difficult terminologies kuonyesha kwamba siasa ni kwa ajili ya watu fulani fulani wenye ufahamu fulani wa itikadi etc..blah blah.

Bottom line ni kwamba itikadi haina maana zaidi slogans, elites and politicians world of complexity in essence tunahitaji "KIONGOZI" na siyo itikadi

Pengine tuanze kwa kuangalia nini maana ya itikadi. Kwa mtazamo wangu, uelewa wako ni kwamba itikadi ni zao la chama cha siasa wakati huu sio ukweli. Hata kama hakuan chama cha siasa, itikadi itakuwepo tu katika jamii, huku jamii moja ikiamini itikadi hii, wakati jamii nyingine ikiamini itikadi nyingine tofauti, lakini pia wakiwa na common agreement katika masuala fulani fulani kuhusu jamii yao na pia mtazamo wao kuhusu ulimwengu unaowazunguka. Nilielezea hapo awali kwanini itikadi ndio mama wa chama cha siasa, na hata katiba ya nchi. Ntakupa mfano mmoja au kukuuliz swali moja - Kwa nchi kama Saudi Arabia ambako hakujawahi kuwa na chama cha siasa, unataka kuniambia kwamba hakuna itikadi mbalimbali ndani ya jamii ile? Na je, vyama vya siasa vikizaliwa Saudi Arabia, vitafuata itikadi gani? Hakika vyama hivi vitafuata itikadi zilizopo lakini kwa kuziboresha katika mazingira ya kisiasa, sera za ushindani n.k. Pia, iwapo nchi kama Saudi Arabia itaingia katika mchakato wa kuzaa katiba mpya ya taifa lile, mchakato huu utakuwa informed na itikadi zilizopo katika jamii, vinginevyo katiba hiyo itakuwa legelege kwani maana ya itikadi ni:

mtazamo, mwongozo, value system, spirit ya taifa, around which matukio na matendo yote ndani ya jamii revolves, hivyo kuimarisha maana, mwelekeo, na tafsiri ya masuala mbali mbali ya ulimwengu, kwa jamii husika.


Naomba unirudie ukipata muda, na maelezo juu ya uelewo wako juu ya itikadi.Post yangu Number 33 inaweza kukusaidia zaidi kuja na hoja za kupingana au kukubaliana na mimi, ili tuzidi boresha mjadala kwa ku agree au kwa agree to disagree.
 
Pengine tuanze kwa kuangalia nini maana ya itikadi. Kwa mtazamo wangu, uelewa wako ni kwamba itikadi ni zao la chama cha siasa wakati huu sio ukweli. Hata kama hakuan chama cha siasa, itikadi itakuwepo tu katika jamii, huku jamii moja ikiamini itikadi hii, wakati jamii nyingine ikiamini itikadi nyingine tofauti, lakini pia wakiwa na common agreement katika masuala fulani fulani kuhusu jamii yao na pia mtazamo wao kuhusu ulimwengu unaowazunguka. Nilielezea hapo awali kwanini itikadi ndio mama wa chama cha siasa, na hata katiba ya nchi. Ntakupa mfano mmoja au kukuuliz swali moja - Kwa nchi kama Saudi Arabia ambako hakujawahi kuwa na chama cha siasa, unataka kuniambia kwamba hakuna itikadi mbalimbali ndani ya jamii ile? Na je, vyama vya siasa vikizaliwa Saudi Arabia, vitafuata itikadi gani? Hakika vyama hivi vitafuata itikadi zilizopo lakini kwa kuziboresha katika mazingira ya kisiasa, sera za ushindani n.k. Pia, iwapo nchi kama Saudi Arabia itaingia katika mchakato wa kuzaa katiba mpya ya taifa lile, mchakato huu utakuwa informed na itikadi zilizopo katika jamii, vinginevyo katiba hiyo itakuwa legelege kwani maana ya itikadi ni:

mtazamo, mwongozo, value system, spirit ya taifa, around which matukio na matendo yote ndani ya jamii revolves, hivyo kuimarisha maana, mwelekeo, na tafsiri ya masuala mbali mbali ya ulimwengu, kwa jamii husika.


Naomba unirudie ukipata muda, na maelezo juu ya uelewo wako juu ya itikadi.Post yangu Number 33 inaweza kukusaidia zaidi kuja na hoja za kupingana au kukubaliana na mimi, ili tuzidi boresha mjadala kwa ku agree au kwa agree to disagree.

Najua maana ya itikadi, itikadi ni muongozo kuhusu namna ya kuendesha mambo ya nchi mfano sheria, biashara na siasa. Itikadi ya nchi kama saudia haitokani na mawazo ya watu wa nchi ile bali imejngwa katika misingi ya Quran (dini) kwa hiyo religion is the source of directions; kwamba vipi wafanye biashara, vipi watoe haki, vipi wagawe mapato ya serikali...

Kwa nchi kama yetu itikadi ya jumla ya jumla ya kuendesha nchi ni KATIBA; katika hiyo inaeleza kiongozi apatikane vipi, vipi aendeshe development programmes na vipi wagawe mapato ya serikali...sasa tukirudi kwenye itikadi ya vyama kwangu mimi naona ni redudancy kama Tanzania itaamua kuwa na katiba yenye kuonyesha vipi watu wapatiwe haki, vipi mapato ya serikali yagawanywe na vipi shughuli za maendeleo zifanyike..

Kwahiyo kwangu mimi tungeanza kufikiri "KIONGOZI BORA" apatikanaje na si itikadi bora ni ipi maana kwa ujumla hakuna ITIKADI BORA itakayotengenezwa na mtu au watu bila mapungufu!??

Kipi kifanyike kwa siasa za Tanzania; Country situational analysis (characteristics): sisi kama nchi tunapata fursa ya ku-analyze nchi kila miaka mitano (uchaguzi) kungalia nini matatizo yetu kama jamii, nini kifanyike kwa wakati huu ambacho ni beneficial kwa taifa Leadership analysis: kwakuwa tunajua mahitaji yetu tunaangalia characteristics za kiongozi ambaye atafaa ili kufaidi kama taifa kwa muda huo..

Itikadi yoyote ile bila uongozi haina maana yoyote ile kwani itikadi zote zina faida na hasara; tena kwa viwango vinavyofanana.
 
Najua maana ya itikadi, itikadi ni muongozo kuhusu namna ya kuendesha mambo ya nchi mfano sheria, biashara na siasa. Itikadi ya nchi kama saudia haitokani na mawazo ya watu wa nchi ile bali imejngwa katika misingi ya Quran (dini) kwa hiyo religion is the source of directions; kwamba vipi wafanye biashara, vipi watoe haki, vipi wagawe mapato ya serikali...

Kwa nchi kama yetu itikadi ya jumla ya jumla ya kuendesha nchi ni KATIBA; katika hiyo inaeleza kiongozi apatikane vipi, vipi aendeshe development programmes na vipi wagawe mapato ya serikali...sasa tukirudi kwenye itikadi ya vyama kwangu mimi naona ni redudancy kama Tanzania itaamua kuwa na katiba yenye kuonyesha vipi watu wapatiwe haki, vipi mapato ya serikali yagawanywe na vipi shughuli za maendeleo zifanyike..

Kwahiyo kwangu mimi tungeanza kufikiri "KIONGOZI BORA" apatikanaje na si itikadi bora ni ipi maana kwa ujumla hakuna ITIKADI BORA itakayotengenezwa na mtu au watu bila mapungufu!??

Kipi kifanyike kwa siasa za Tanzania; Country situational analysis (characteristics): sisi kama nchi tunapata fursa ya ku-analyze nchi kila miaka mitano (uchaguzi) kungalia nini matatizo yetu kama jamii, nini kifanyike kwa wakati huu ambacho ni beneficial kwa taifa Leadership analysis: kwakuwa tunajua mahitaji yetu tunaangalia characteristics za kiongozi ambaye atafaa ili kufaidi kama taifa kwa muda huo..

Itikadi yoyote ile bila uongozi haina maana yoyote ile kwani itikadi zote zina faida na hasara; tena kwa viwango vinavyofanana.

Bado tunapishana kidogo kuhusu itikadi. itikadi haitungwi, itikadi ni matokeo ya mila, desturi, mtazamo, maadili, imani za dini n.k. Sana sana, kinachofanyika chini ya itikadi ya chama cha siasa ni kuyaweka haya katika lugha mbalimbali ili kupata wafuasi kwa lengo la kuwapigania wafuasi husika bungeni etc, kuwakilisha kutokana na maoni yao, mawazo yao (itikado zao...)...

Uongozi bora ni matokeo ya uwepo wa itikadi ya au za aina fulani katika jamii ambapo jamii 'A' inaweza amini sifa za kiongozi bora ni hizi, wakati jamii 'B', inawez amini sifa za kiongozi mwingine kuwa tofauti, kutokana na mila, desturi, imani, mtazamo n.k (vitu ambavyo ndio vinajenga itikadi). hata unapoenda kutoa maoni yako kwa mfano mbele ya tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya, mawazo yako yatatokana na imani, desturi, mtazamo wako kuhusu ulimwengu, n.k, au sio?
 
Back
Top Bottom