Nape: Hata mimi nataka Katiba Mpya

Analogia Malenga

Platinum Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,292
Reaction score
10,842
Waziri wa Mawasiliano Nape Nnauye amesema ubaya uliopo ni kuwa wanaohitaji katiba Mpya wanahitaji kwa kudai badala ya kuwa na majadiliano kati yao na serikali. Katiba Mpya ni majadiliano katika wadau wote, isionekane kuna mtu anadai, kumdai mwingine.

Amesema hakuna asiyehitaji katiba mpya, watu wote wanataka katiba mpya kwa kuwa kila mmoja anahitaji maisha bora hata yeye anahitaji katiba mpya

Ameyasema hayo katika kipindi cha Dakika 45 ITV, Jumatatu, Machi 6, 2023. Katika kuzungumzia suala la mitandao kuzimwa amesema wala serikali haikuzima mtandao wa ClubHouse.
 
Sasa ujadiliane na nani wakati kila kitu kipo wazi toka katiba pendekezwa ya jaji Warioba ikae mbele ya wenye nchi!.
 

Ao wana katiba mpya yao tayar iko kwenye makabati! Watakachofanya hapo ni kubadili rangi ya gamba tu ilo.
 
Sasa ujadiliane na nani wakati kila kitu kipo wazi toka katiba pendekezwa ya jaji Warioba ikae mbele ya wenye nchi!.
Ndio hapo sasa. Yaani ccm hawataki kukubari kwamba hoja ya Katiba Mpya ilianzishwa na Chadema. Walitarajia iwe wao.
 
Emu subiri kipindi kiishe tafadhali

Mbona unavunja ethics za uandishi wa taarifa?
 
Na kwa kauli yake ya kugawana rasilimali kwa usawa, inaonesha kuna sintofahamu kwenye ugawaji wa rasilimali za umma, ndio maana kila mmoja najichotea tu. Sema Farhia hajagongelea msumali hapo
 
Emu subiri kipindi kiishe tafadhali

Mbona unavunja ethics za uandishi wa taarifa?
Kwahiyo tuache kucomment?
Mbona wachambuzi wanachambua mechi ya mpira wakati bado unaendelea?
 
Utawala wa Magufuli umewafanya watu waone umuhimu wa Katiba mpya.
 
Kuna mahala wanakaa wanatucheka
 
Nape amelamba asali ya bhugwi kutoka chadema.
 
Nchi hii haiishi vituko. Huyo aliyekua anashambulia wanamabadiliko ndio huyo tena.
Enzi hizo watu walitukanwa na waliojiona wanahatimiliki na nchi hii.

Siasa zisizo zauhasama za mama zinawachanganya hao wabaguzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…