Nape azomewa, Kinana amshusha jukwaani

Nape azomewa, Kinana amshusha jukwaani

Tatizo huwa wanapeana uongozi kiundugu na fadhira lakini kiukweli Nape hana uwezo wa kupambanua vitu kwa busara na kutumia akili za ziada. Ni mkurupukaji na mropokaji. Siasa inahitaji fikra pevu, bado kabisa huyo na mara nyingi huwa ni mpiga kelele tu majukwaani.
 
chaikavu

Hii source ya habari ina ugomvi na serikali iko bias inashambulia upande inaouchukia. Hata siku moja usiamini habari zao kichwakichwa.
 
Last edited by a moderator:
Mtu anayedharau maamuzi ya wananchi na kuwaita wanywa viroba ni kuwazomea tu mpaka anaacha kuongea pumba

Ukweli Mkuu mtu wa aina hiyo ni wazi dharau zilizochanganyika na jazba ndizo zinamsukuma kuropoka, vinginevyo alitakiwa akubali kuwa kwenye ule mkutano wapo pia wapenzi wa UKAWA na ndio ilikuwa nafasi yake kueleza sera ili awavute karibu, mwanasiasa bora ndicho anachofanya sio Nape na kupayuka.
 
Huyu mtu siku ccm itaondoka madarakani, ataishi maisha ya aibu na fedheha siku zote
 
Huku ni kudanganyana fisadi mnaemwita ni lowassa na hadi dakika hii anakusanya watu kila kona sasa ni vema useme utamzomea na siyo mtamzomea, maana mwenzako kajipanga na sasa elewa hajawa mgombea rasmi akipitishwa akapewa na ulinzi imara kamwe hutasikia unachokiwaza! Nilitarajia wakati ni sasa mngedhihirisha hauziki na hafai lakini anaonekana ndiye lulu kuliko yeyote ndani ya ccm. Tuache ubishi wa hisia zenu na kina nape jamani



hii zomea zomea itazidi maradufu ikiwa ccm watasimamaisha mgombea fisadi au galasa, vile vile zomea zomea hii itapungua ikiwa ccm itasimamisha mgombea anayekubalika kwa wananchi, anayeakisi kile wananchi wanapenda, alietayari kupambana na kile wanachukia

akipatikana mgombea safi, akauzwa na watu safi, basi atasaidia sana kurudisha imani ya watanzania kwa ccm, na atasaidia sana kuuza wagombea wa udiwani na ubunge wa ccm. Otherwise, hali ni mbaya kwa ccm kuekea october
 
Jana niliangalia TBCiii (kwa bahati mbaya) taarifa ya usiku, hakika hawakuonesha kabisa kipande hicho:becky:
 
Back
Top Bottom