Nape aunguruma Njombe....

Nape aunguruma Njombe....

Shagiguku

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
409
Reaction score
138
Mh: Nape Nnauye ameunguruma leo jioni hapa mkoani Njombe katika mkutano wake wa hadhara uliohudhuriwa na ma-mia kwa maelfu ya wananchi na kuzungumzia juu ya masuala ya uundaji wa tume mbalimbali katika nchi yetu ambazo zimeleta tija kwa maendeleo ya taifa.

Katika mkutano huo mh: Nnauye amewakemea watu wanaobeza jitihada za serikali katika kushughulikia mambo mbalimbali ambayo ni kero kwa wananchi.



Hii ni taarifa kwa ufupi kwa wale ambao hawakuwepo ktk mkutano huo.
 
Nnauye amewakemea watu wanaobeza jitihada za serikali katika kushughulikia mambo mbalimbali ambayo ni kero kwa wananchi.

Kiongozi mzuri ni yule anaeshawishi siyo kukemea. Nnauye Jr alipaswa awashawishi kwa hoja watu wanaobeza jitihada za serikali katika kushughulikia Mafisadi, Ugumu wa maisha na upatikanaji wa huduma za kijamii.

TUMBIRI (PhD, Hull University - UK),

tumbiri@jamiiforums.com
 
03.jpg

Hawa ndio mamia kwa maelfu? Hesabu tena.
 
Weka basi hiyo picha ya njombe unayodai ya ukweli tuone hao "mamia kwa maelfu"

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kwa mahudhurio hayo... CCM kwisha kazi!!!! ha ha ha ha!!! Labda mtafute mganga mwingine awasaidie kwa ramli! Sheikh Yahya alikuwa anawafaa sana lakini sasa naona ameamua kuondoka na ninyi!!
 
Hii sio picha ya Njombe, acha kuwadanganya watu. Mtapata tabu sana kudanganya watu kwani UONGO HAUDUMU!!

Uongo hujibiwa kwa ukweli, hebu weka iyo picha ya njombe tuone nani mkweli, otherwise we call it the last kick of the dying donkey.
Upo bwana Nnauye Jr??
 
Ama kweli Nape na CCM ni kama kupe:
Ng'ombe anachinjwa kupe hana habari!
Ng'ombe anachunwa kupe hana habari!
Ngozi inawambwa kupe hana habari!
Ngozi ikianza kukauka kupe ndo anastuka!
Alaa! Huyu ngo'mbe kumbe keshachinjwa!
 
wewe uliyeanzisha thread hii, yafaa sana uweke ukweli wa mambo kama ulivyo!

kama watu mliowakodi kwa kuwapa pesa za mafuta ya pikipiki na magari ili waongeze uwingi wa watu, walifikia maelfu, basi haujakosea sana!
 
Hii sio picha ya Njombe, acha kuwadanganya watu. Mtapata tabu sana kudanganya watu kwani UONGO HAUDUMU!!

tuwekee picha za ukweli acha kulalamika. sisi tunaamin kile tunacho kiona.
 
Hii sio picha ya Njombe, acha kuwadanganya watu. Mtapata tabu sana kudanganya watu kwani UONGO HAUDUMU!!

Hahahaaa, mkuu weka picha basi za ukweli na uweke data walioletwa kwa fuso from Uwemba, Iwungilo, Lugenge, Matola, Boimanda, Kifanya, Lupembe na Wangama. Maana alipokuja JK wenu mliniboa kweli, nusura nikose hela kwani fuso zote za kubebea viazi mmepakia watu. Nonsense!
 
Tunasubiri ukweli sasa (kama upo)!
 
Hii sio picha ya Njombe, acha kuwadanganya watu. Mtapata tabu sana kudanganya watu kwani UONGO HAUDUMU!!

Mkuu, kwa kazi yako ya uenezi ulitakiwa wewe ndo utuletee hii habari pamoja na hizo picha unazodai ni halisi. Unapoanza na wewe kulalamika kwa mtindo huu inakuwa inapoteza maana kabisa. Ni ushauri tu lakini.
 
Mikutano yako ni na wazee tu? ANYWAY UTAPATA THAWABU KWA KUWAPA BRAND NEW T-SHIRTS!

4.+Nape+akishiriki+kucharaza+ngoma+kata+ya+Mlangali,+Njombe.jpg
 
Back
Top Bottom