Nape ana hoja ya msingi ila shida ni yeye

Aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM na Mbunge wa jimbo LA Mtama Mh Nape Moses Nnauye,ameibua mjadala mitandaoni kwa hoja yake aliyoitoa bungeni hivi karibuni ya kutaka kuwepo kwa uchunguzi wa kina kuhusu hoja iliyoibuka ya kuwepo kwa deni kubwa LA taifa.

Mh Nape anasema "kufanyike uchunguzi wa kina ili kubaini ukweli wa matumizi ya fedha za mikopo hiyo iliyokopwa na Nchi na kulinganisha na kiasi cha gharama ya miradi ya maendeleo iliyofanyika."

Anasema "kipindi cha awamu ya tano kumekuwepo na usiri mkubwa katika ukopaji wa fedha hizo na ndicho kipindi kilichokopa pesa nyingi ukilinganisha na awamu zote japo ni awamu iliyokaa muda mfupi madarakani kuliko awamu zote."

Akaenda mbali zaidi kwa kutolea mfano awamu ya sita chini Rais Mama Samia, kama mfano bora wa uongozi wa uwazi kwa kuweka bayana matumizi ya mkopo wa fedha za IMF 1.3Trilions namna zilivyoainishwa upatikanaji wake na matumizi yake.

Mm binafsi kama Chakwale naona Nape ana hoja ya msingi ya kutaka kuwepo uwazi na ukweli wa matumizi ya fedha zote za serikali,kwa sababu matumizi yoyote ya hovyo mzigo wote anaubeba or tunaubeba sisi Wananchi wa kipato cha chini.

Unaweza kuona serikali ya awamu ya sita inavyopambana katika kuongeza vyanzo vya vipya vya mapato ikiwemo Kuanzisha tozo Mpya za Miamala ili walau kuongeza wigo wa mapato jambo ambalo limepigiwa kelele na wananchi kuwa linawaongezea mzigo maisha.

Sasa kama Wananchi tumejaribu kupaza sauti zetu kuhusu tozo sababu zimetugusa moja kwa moja nilitarajia hata hili LA Mh Nape lingeungwa mkono kama LA tozo sababu adhari zake ni zilezile kwa mwananchi wa hali ya chini.

Badala yake imekuwa kinyume kwa Mh Nape kuonekana kama ni MTU mwenye Chuki,kisasi or hasira na utawala uliopita wa awamu ya tano,kwa kuwa tu eti alienguliwa Uwaziri wa Habari Sanaa na Michezo kwa kile alichokuwa akikiamini juu ya sakata zima LA aliekuwa Mkuu wa mkoa wa Dar.

Ninachokiona watu hawaangalii hoja iliyotolewa na kuijadili Bali wanachoangalia ni mtoa hoja ni nani,so inaonekana watu hawana shida na hoja ila wana shida na mtoa hoja kitu ambacho katika karne hii ni matumizi mabovu ya rasilimali kichwa.

Kumchukia MTU kwa sababu zako binafsi hakuondoi Uimara,umaana,hekima,busara wala mantiki ya kile alichokisema.kwanza unatakiwa utafakari uchuje then uunge mkono or kukosoa kwa hoja si kwa kutumia chuki zako binafsi.

Kama taifa lililo serious na Maendeleo endelevu ya Nchi yetu tulipaswa kumuunga mkono Nape kwa hoja yake aliyotoa ili kujiridhisha.Sababu haiwezekani watu wengine wabebeshwe mzigo kwa ujinga,tamaa na chuki za watu wengine tutakuwa tunacheza "Mark time" tu bila kusonga mbele.

Kwa Nchi za wenzetu bei tu mkate ikipanda bei pasipokuwapo sababu zinazoeleweka hapakaliki lazima watu wawajibike kwa hilo sembuse sisi ambao Trillions of money hazieleweki zinatumikaje halafu tupotupo tu.

Nilitarajia vyama vyetu vya upinzani vingekuwa vimepata agenda ya kuvifanya vitengeneze uwepo wao,navyo vimelala usingizi wa pono vina ajenda moja tu ya katiba Mpya ambayo imefinyiwa kwapani hawana mbadala tena.Kama huwezi kuwasemea Wananchi katika haya yanayowahusu kama ya Tozo,kupanda kwa bei ya mbolea na bidhaa zingine,mazingira bora ya machinga,ukosefu wa ajira kwa vijana nk nk ni mwananchi gani atakusapoti suala lako LA katiba ambalo anajua ni LA tamaa zako tu za kutaka kukuingiza madarakani ila sio kumtetea yeye??


Alamsiki
Hata ikiundwa tume kuchunguza hiyo kitu, unafikilia nini kitatokea??? Uchunguzi unaweza kufanyiwa na kukuta Kuna ubadhirifu mkubwa na Chama dola kikashindwa kuitoa ripoti hadharani kwa kuhofia itawaghalimu sana ktk uchaguzi.

Sisi wtz ni watu wa ajabu sana. Kazi Yetu kulalamika tu hatuwezi kuiwajibisha Serikali wakati sisi ndio wenye nchi

Kitu kibubwa na cha mingi ili kukomesha haya mambo ya kijinga ni kupata katiba Mya itakayo wawajibisha viongozi na kutupilia mbali Sheria ya kijinga ya kutokushitakiwa kwamakosa watakayofanya wakati wakiwa madalakani kwani hiyo Sheria ndio inayotufanya tuingizwe chaka
 
Nchi ngumu sana hii kwani kuna shida gani kwenye hoja ta Nape, amesema hesabu zikaguliwe kama zinaeleweka povu la nn
 
Kwanza ikumbukwe kuwa, Nape na Genge lake waliwahi kumtukana sana Mzalendo wetu JPM, yeye(Nape) alipoona mambo yote yapo hadharani, aliamua kwenda kwa JPM kuomba msamaha.

Hata kipindi cha Bunge kilichopita, Nape huyu huyu alionesha dalili za moja kwa moja za kupinga kabisa Legacy ya JPM, alipopigwa mashambulizi makali mitandaoni, aliamua kuchuchumaa.

Kwa hiyo, leo hii Nape atatuambia nini ili tumwamini?
Zaidi sana hapo yeye anachokitafuta ni kupata uteuzi tu na wala si vinginevyo.
Ili ujue kichwa chake ni kibovu kabisa ni pale anaposhindwa hata kujua kuwa, Serikali ya awamu ya tano ya JPM ndiyo iluyofanya maajabu ya kufanya mambo makubwa kabisa ambayo wengine wote waliopita walishindwa kabisa ingawa walikaa madarakani kwa miaka 10.
Nape asicheze na akili za Watanzania wa leo. Kuna siku atakuja kuumbuka mchana kweupe.
Ndio mtu wangu
 
Aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM na Mbunge wa jimbo LA Mtama Mh Nape Moses Nnauye,ameibua mjadala mitandaoni kwa hoja yake aliyoitoa bungeni hivi karibuni ya kutaka kuwepo kwa uchunguzi wa kina kuhusu hoja iliyoibuka ya kuwepo kwa deni kubwa LA taifa.

Mh Nape anasema "kufanyike uchunguzi wa kina ili kubaini ukweli wa matumizi ya fedha za mikopo hiyo iliyokopwa na Nchi na kulinganisha na kiasi cha gharama ya miradi ya maendeleo iliyofanyika."

Anasema "kipindi cha awamu ya tano kumekuwepo na usiri mkubwa katika ukopaji wa fedha hizo na ndicho kipindi kilichokopa pesa nyingi ukilinganisha na awamu zote japo ni awamu iliyokaa muda mfupi madarakani kuliko awamu zote."

Akaenda mbali zaidi kwa kutolea mfano awamu ya sita chini Rais Mama Samia, kama mfano bora wa uongozi wa uwazi kwa kuweka bayana matumizi ya mkopo wa fedha za IMF 1.3Trilions namna zilivyoainishwa upatikanaji wake na matumizi yake.

Mm binafsi kama Chakwale naona Nape ana hoja ya msingi ya kutaka kuwepo uwazi na ukweli wa matumizi ya fedha zote za serikali,kwa sababu matumizi yoyote ya hovyo mzigo wote anaubeba or tunaubeba sisi Wananchi wa kipato cha chini.

Unaweza kuona serikali ya awamu ya sita inavyopambana katika kuongeza vyanzo vya vipya vya mapato ikiwemo Kuanzisha tozo Mpya za Miamala ili walau kuongeza wigo wa mapato jambo ambalo limepigiwa kelele na wananchi kuwa linawaongezea mzigo maisha.

Sasa kama Wananchi tumejaribu kupaza sauti zetu kuhusu tozo sababu zimetugusa moja kwa moja nilitarajia hata hili LA Mh Nape lingeungwa mkono kama LA tozo sababu adhari zake ni zilezile kwa mwananchi wa hali ya chini.

Badala yake imekuwa kinyume kwa Mh Nape kuonekana kama ni MTU mwenye Chuki,kisasi or hasira na utawala uliopita wa awamu ya tano,kwa kuwa tu eti alienguliwa Uwaziri wa Habari Sanaa na Michezo kwa kile alichokuwa akikiamini juu ya sakata zima LA aliekuwa Mkuu wa mkoa wa Dar.

Ninachokiona watu hawaangalii hoja iliyotolewa na kuijadili Bali wanachoangalia ni mtoa hoja ni nani,so inaonekana watu hawana shida na hoja ila wana shida na mtoa hoja kitu ambacho katika karne hii ni matumizi mabovu ya rasilimali kichwa.

Kumchukia MTU kwa sababu zako binafsi hakuondoi Uimara,umaana,hekima,busara wala mantiki ya kile alichokisema.kwanza unatakiwa utafakari uchuje then uunge mkono or kukosoa kwa hoja si kwa kutumia chuki zako binafsi.

Kama taifa lililo serious na Maendeleo endelevu ya Nchi yetu tulipaswa kumuunga mkono Nape kwa hoja yake aliyotoa ili kujiridhisha.Sababu haiwezekani watu wengine wabebeshwe mzigo kwa ujinga,tamaa na chuki za watu wengine tutakuwa tunacheza "Mark time" tu bila kusonga mbele.

Kwa Nchi za wenzetu bei tu mkate ikipanda bei pasipokuwapo sababu zinazoeleweka hapakaliki lazima watu wawajibike kwa hilo sembuse sisi ambao Trillions of money hazieleweki zinatumikaje halafu tupotupo tu.

Nilitarajia vyama vyetu vya upinzani vingekuwa vimepata agenda ya kuvifanya vitengeneze uwepo wao,navyo vimelala usingizi wa pono vina ajenda moja tu ya katiba Mpya ambayo imefinyiwa kwapani hawana mbadala tena.Kama huwezi kuwasemea Wananchi katika haya yanayowahusu kama ya Tozo,kupanda kwa bei ya mbolea na bidhaa zingine,mazingira bora ya machinga,ukosefu wa ajira kwa vijana nk nk ni mwananchi gani atakusapoti suala lako LA katiba ambalo anajua ni LA tamaa zako tu za kutaka kukuingiza madarakani ila sio kumtetea yeye??


Alamsiki
Mkuu naona uko kwenye genge la counter attack kuupoteza mwelekeo wa hoja ya uchunguzi wa ufisadi wa mikopo ya JPM.
Haijalishi ukweli unasemwa na nami alimradi ukweli unawekwa wazi.

Hata shetani, kinara wa uongo alilazimika kukubali Yesu ni Bwana.
 
Mkuu naona na ww unapita mulemule kwenye kumuattack MTU personally badala ya kuattack hoja yake.. Niambie hoja yake ina shida gani?wapi pana shida kwenye hoja yake?wapi amepatia pia?kusema sijui alionyesha kupinga Legacy ya JPM hiyo mbona haihusiani na hoja aliyoitoa?hata kama ni kweli alionyesha kupinga shida iko wapi si alitumia Uhuru wake binafsi wa kikatiba kutoa maoni yake?

So unataka kuniaminisha kuwa MTU akiwa kinyume na mawazo or mtazamo aliokuwa nao JPM ni kosa ambalo hastahili kusikilizwa hata anasema nini?

Kama ni hivyo ni akina nani basi wenye haki na hati miliki ya kusema na kusikilizwa bila hata ya kuchuja kuwa wamesema nini?
Nape alichokosea ni kuchagua kwamba ukaguzi uwe kipindi cha Magufuli,angeomba uanze tangia kipindi cha Mkapa mpaka awamu ya sita,watanzania wa sasa sio wale wa miaka ile
 
Siasa zetu zimekuwa za hovyo sana!
Siasa imekuwa ndo uwanja pekee ambao kila mtu anaweza kuingia na kutoboa kwa sasa!
Wameingia kwenye siasa matapeli,waganga wa kienyeji ,machangudoa na vi.laza wengi sana! Hivyo siasa za hoja hazina nafasi tena.
Na pia wananchi wengi wa Nchi yetu kutokana na elimu duni na maarifa madogo hawajui mantiki ni nini na pumba ni nini?!
Angalia hata kwenye Bunge letu akina Musukuma, Lusinde ( Kibajaji) wana nguvu na ushawishi na wanaeleweka kwa Wananchi kuliko hata Maprofesa walioko Bungeni!
Ukiona kina Lusinde na Bajaji wanaeleweka ujue wanaongea lugha inayoeleweka kwa wananch.

RELEVANCY kwenye siasa ni muhimu kuliko LOGIC.
 
So unataka kuniaminisha kuwa MTU akiwa kinyume na mawazo or mtazamo aliokuwa nao JPM ni kosa ambalo hastahili kusikilizwa hata anasema nini
Hapa ndiyo penye shida ya awamu ya JPM. Hawataki mawazo tofauti ili tusonge mbele kujifanya wao ndiyo wenye uelewa mkubwa kuliko waTz zaidi ya milioni 60, Magufuri alikuwa hataki kupata changamoto toka kwa yoyote ukiongea tofauti naye kifo umekikaribisha na hii si sawa. Mungu ametuumba tofauti kwa mawazo na akili ndiyo maana kuna mikutano ili kuchangia mawazo. Mungu ametusaidia haki Magufuli asingetoka madarakani ndiyo maana alimpeleka polepole bungeni ili asimamie kipengele cha kubadili cha ukomo wa urais
 
Nape anataka makamu wake wa Rais achunguzwe. Hata kama JPM angekuwa hai na amestaafu, kwani uchunguzi wa CAG anaotaka Nape utamfanya nini Rais mstaafu? Anaropokwa tu.
 
Tatizo la Nape ni njaa na alijianimisha kuwa yeye ndie mwenye CCM kisa baba yake alikuwa nae mwenye CCM, Nape huyu huyu ndie alijifanya ana uchungu na mali za Umoja wa Vijana baada ya yalipokuwa makao makuu ya Umoja wa Vijana kukwapuliwa na akina mamvi na wahindi wenzake na akasahau kuwa mamvi hakuwa peke yake, matokeo yake akawa anabweka tu na hakuna lolote alilofanya nae ndio akaanza tabia za wizi wa mali za CCM na bwana Ndovu na yule babu wa Lushoto, huyu Nape ni genge la wahuni na wezi na hana uchungu wowote kelele zote za sasa ni kutaka cheo serikalini, ukiangalia timu yake ya mwanzoni wenzake wote ni mawaziri,Bashe,January ni yeye na mtoto wa remote ndio hawamo kwenye baraza ingawa bado mtoto wa remote ameanza kuwa na nguvu hivi sasa kutokana na nguvu za remote alizonazo hivi .

Mali zenu za kikundi chenu cha upatu hapo Lumumba hazituhusu maana hata nyinyi hizo mali mmepata kwa wizi/dhuluma/utapeli.

Nape ana hoja ya msingi na nzito,kufanyike uhakiki kwenye deni la taifa hasa kipindi cha awamu ya 5 ,fedha zimetumika wapi wakati tuliambiwa miradi yote tunatekeleza kwa fedha zetu wenyewe na siyo mikopo.
 
Mkuu naona na ww unapita mulemule kwenye kumuattack MTU personally badala ya kuattack hoja yake.. Niambie hoja yake ina shida gani?wapi pana shida kwenye hoja yake?wapi amepatia pia?kusema sijui alionyesha kupinga Legacy ya JPM hiyo mbona haihusiani na hoja aliyoitoa?hata kama ni kweli alionyesha kupinga shida iko wapi si alitumia Uhuru wake binafsi wa kikatiba kutoa maoni yake?

So unataka kuniaminisha kuwa MTU akiwa kinyume na mawazo or mtazamo aliokuwa nao JPM ni kosa ambalo hastahili kusikilizwa hata anasema nini?

Kama ni hivyo ni akina nani basi wenye haki na hati miliki ya kusema na kusikilizwa bila hata ya kuchuja kuwa wamesema nini?
Wafiwa wa mwendazake wanaamini mwendazake ni mungu wao na hakukosea, hivyo kwenda kinyume nae ni kosa kubwa sana. Badala wajikite katika hoja ya msingi wamebaki kumuattack Nape tu.
 
Nape amesema "kipindi cha awamu ya tano kumekuwepo na usiri mkubwa katika ukopaji wa fedha hizo na ndicho kipindi kilichokopa pesa nyingi ukilinganisha na awamu zote japo ni awamu iliyokaa muda mfupi madarakani kuliko awamu zote."
Ningependa kujua yule aliyemtoleaga bastola Nape awamu ya tano anaendeleaje awamu hii ya sita? Na je vip bado anaendelea kuvimba kama kipindi kile?
 
Nchi ngumu sana hii kwani kuna shida gani kwenye hoja ta Nape, amesema hesabu zikaguliwe kama zinaeleweka povu la nn
Nashangaa sana kwakweli..kama hakuna shida si basi tutakuwa tumejiridhisha??
 
Wafiwa wa mwendazake wanaamini mwendazake ni mungu wao na hakukosea, hivyo kwenda kinyume nae ni kosa kubwa sana. Badala wajikite katika hoja ya msingi wamebaki kumuattack Nape tu.
Chuki binafsi tu ambazo kimsingi hazisaidii kitu
 
Back
Top Bottom