JACADUOGO2.
JF-Expert Member
- Dec 13, 2010
- 930
- 217
Jamani ndugu zangu wanajf naombeni tuwe makini na tuache unafiki. Nape Nnauye amefika chuo kikuu cha Dodoma (Udom) majira ya saa 5 asubuhi. Hivi Nape alikuja kufanya nini Udom na alitumwa na nani kwani amekuja na kuingia bwenini na ndani ya baadhi ya vyumba na kudai kuwa anakagua nyufa ndani vyumba na kukagua maeneo machafu ndani ya chuo. Hivi Nape ni injinia wa Udom? Au Nape ni bwana afya wa Udom? Au Nape ndiye msemaji wa wanachuo kwa rais wa nchi? Tunaomba Nape atueleze vizuri alichoijia Udom kwani hatujajua alichokuja kufanya. Mimi ni mwanafunzi wa Udom na ninavyokijua Udom na viongozi wa Udom siyo rahisi kumruhusu mwanasiasa kuingia ndani ya chuo bila wanafunzi kujulishwa juu ya ujio wake na lengo lake. Mbaya zaidi Nape ameruhusiwa kuingia hadi ndani ya vyumba vya wanafunzi. Hata Lema hakuwahutubia wanafunzi ndani eneo la chuo. Tunaomba ufafanuzi!