Nape aivua nguo CCM,audanganya umma...

Nape aivua nguo CCM,audanganya umma...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,006
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amekivua nguo chama tawala.Amedai kuwa wakati wa kampeni,vyama hubeba watu kutoka sehemu mbalimbali ili kujaza wahudhuriaji.Watu hao,ingawa si wapiga kura,hubebwa ili kuuhadaa umma kuwa mkutano wa chama husika umehudhuriwa na umati wa watu.Hakutaja ni chama gani hasa.Nani asiyejua kuwa mtindo huu hutumiwa na CCM tu? Kwanini Nape ameamua kuiumbua nyumba yake?

Kama hiyo haitoshi,Nape amedai kuwa CCM ina utaratibu wa kuwalazimisha wanachama wake kujiandikisha na kupiga kura. Akitoa mfano,Nape amedai kuwa hata kwenye kura za maoni CCM ilanzisha utaratibu wa kila mwanachama kuwa na kadi mbili:ya kupiga kura na ya uanachama.Nani hajui kuwa huu haukuwa utaratibu rasmi wa CCM? Utaratibu huu ulileta sintofahamu kubwa ndani ya CCM kwa kuletwa kwa kukurupuka.Uliwalenga wachache ili washindwe.Nape ameudanganya umma.Amefanya kusudi?


Source: Mahojiano yake na Issac Gamba wa Radio One Stereo katika kipindi cha Hoja ya Leo jana.
 
...sioni cha ajabu hapo. Ni sawa na kumshangaa shetani akitenda maovu.
 
Alililia wembe sasa unamkata kila asubuhi, waacheni wafu kwa wafu wazikane
 
HUu nin ujumbe wake kwa chama chake. Hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii inamaaana hawakubariani kabla ya kufanya mambo yao ki-chama.
 
huyu jamaa ana DEAD END kwenye siasa , uyu jamaa sio Makini kabisa, i take him as a JOKE -


Nape ni muongo halafu hana kumbukumbu; muongo mzuri anatakiwa awe na kumbukumbu nzuri !! He is a disaster in the making.
 
Alishasema anapenda magwanda ya cdm,
anatafuta tu njia ya kuondokana na hayo magamba.
 
Nape ni muongo halafu hana kumbukumbu; muongo mzuri anatakiwa awe na kumbukumbu nzuri !! He is a disaster in the making.
yupo umu JF anasoma ujumbe , but habadiliki , hajifunzi, anyway yeye na waliompa nafasi, na chama chake kwa ujumla sio watu makini, naamini kila anachofanya anakuwa ametumwa na anasema kama kilivyo , they are on the way to their grave
 
Hiyo ndiyo STYLE ya CCM kubeba watu kutoka sehemu mbalimbali kwenda kwenye mikutano.

Hata Rehema Nchimbi ametumia UZOEFU wa chama chake kufikia uamuzi wa kupiga mikutano ya hadhara Dodoma!
 
Back
Top Bottom