Ciril
JF-Expert Member
- Jan 10, 2011
- 8,558
- 7,156
bado kidogo ataeleza jinsi gani wanavyoiba kura
Masikini mbavu zangu!!!!!!!!!!Asante mkuu.
bado kidogo ataeleza jinsi gani wanavyoiba kura
yupo umu JF anasoma ujumbe , but habadiliki , hajifunzi, anyway yeye na waliompa nafasi, na chama chake kwa ujumla sio watu makini, naamini kila anachofanya anakuwa ametumwa na anasema kama kilivyo , they are on the way to their grave
bado kidogo ataeleza jinsi gani wanavyoiba kura
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye amekivua nguo chama tawala.Amedai kuwa wakati wa kampeni,vyama hubeba watu kutoka sehemu mbalimbali ili kujaza wahudhuriaji.Watu hao,ingawa si wapiga kura,hubebwa ili kuuhadaa umma kuwa mkutano wa chama husika umehudhuriwa na umati wa watu.Hakutaja ni chama gani hasa.Nani asiyejua kuwa mtindo huu hutumiwa na CCM tu? Kwanini Nape ameamua kuiumbua nyumba yake?
Kama hiyo haitoshi,Nape amedai kuwa CCM ina utaratibu wa kuwalazimisha wanachama wake kujiandikisha na kupiga kura. Akitoa mfano,Nape amedai kuwa hata kwenye kura za maoni CCM ilanzisha utaratibu wa kila mwanachama kuwa na kadi mbili:ya kupiga kura na ya uanachama.Nani hajui kuwa huu haukuwa utaratibu rasmi wa CCM? Utaratibu huu ulileta sintofahamu kubwa ndani ya CCM kwa kuletwa kwa kukurupuka.Uliwalenga wachache ili washindwe.Nape ameudanganya umma.Amefanya kusudi?
Source: Mahojiano yake na Issac Gamba wa Radio One Stereo katika kipindi cha Hoja ya Leo jana.
Ukatae kuingia kwenye roli wakati wanagawa na posho, pilau ya bure na ze comedy ya bila kiingilio.Lakini cha kufurahisha pilau wanakula na kura kwa CDM hayo ndio malipo ya kufikiri watu wote ni wajinga.Yuko sawa. ccm wanabeba watu kwenye malori. Sasa jambo la kujiuliza mbumbumbu ni wanaobwebwa au wanobeba? Hivi wananchi wakikataa kuingia kwenye hayo malori watakamatwa kwa nguvu? Nape na wenzake wameshapima kuwa watanzania hamnazo siku moja wakiona malori yao yanapata hasara watabeba watu kwenye majeneza na kwa kuwa yatakuwa majeneza ya chama dume, chama tawala watu watapanda tena kwa kugombania.
Hiyo idara ya uenezi ingebadilishwa jina iwe"Idara ya uropokaji na itikati isiyojulikana na uenezi wa uongo"