Naongea naye nini?



Kwa hapo tu (Blue)....naomba utegemee kupokea PM yangu muda si mrefu...Ikizingatia tuvyokaangwa huku site...Unaweza kuwa mkombozi bila kutegemea!!

Nakubaliana na wewe, watoto ni waelewa sana endapo tukiwafundisha kuelewa kwa kuwapa sababu ya kitu tunachokiongea....Nashukuru sana kwa michango yako na pia nimefurahi kwamba bado kuna wazazi wanawaona watoto kama watu wazima wa kesho ambao wanatakiwa kuwa reasonable and responsible!!

Nachukia watu wanaowadekeza watoto na kuwaona kama vile wameumbwa kwa precious metals au fragile materials!

Babu DC!!
 
Kitu kikubwa kinanipa msukumo wa kufanya hayo ni fact kwamba sisi ni binadamu......... hatujui kesho kitatokea nini...... Hatuombei mabaya, nakiukweli naomba Mungu sana mabaya yasinikute, lakini Mungu huyo huyo ana mpango na kila binadamu, hatuwezi kubadilisha mipango yake, hakuna aliyewahi kufanya hivyo.
Hebu imagine unawalea wanao kwa mtindo huo, kesho haupo, unamuachaje mwanao? kama kuna vitu nang'ang'ania sana kwa maisha ya wanangu ni kuwawekea akiba, siyo kuwa-spoil. siku ambayo sitakuwepo, hata kama ni miaka 50-60 ijayo, watanikumbuka kwa vitu nilivyowaachia. nimeona watoto wengi wanahangaika sana wazazi wao wanapoishia, au kufilisika...... mtoto anashindwa kwenda shule sababu hawezi kulipa ada.
hata kazi za nyumbani, huwa nahakikisha wanangu wanafanya kazi, kwa kushirikiana na mimi mwenyewe na wadada wa kazi.... hakuna mtu special nyumbani kwangu, kila mtu anafanya kazi kulingana na umri na nguvu zake...... hii ni amri na inatekelezwa.
 
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…