Naona huruma kumpiga chini, nifanyeje?

Naona huruma kumpiga chini, nifanyeje?

hyo mkeo mmefunga ndoa gani?
Maana unavyoongea kumpiga chini kirahisi mh!?
 
Nishajaribu sana. Nishampeleka shule ya hotel management alipomalza akasema hataki kazi za hotelini. Akataka fungua tailoring mart tukanunua vifaa vyote vya lazima mpaka leo vipo ndani, baadhi aligawa. Akasema anataka biashara za mikoani nikampa mtaji akaenda trip mbili tu akaacha, akasema anataka biashara ya duka nikampa mtaji, fremu nikamlipia duka lina bidhaa za kutosha anafungua akijisikia, say once a week or in two weeks. Nikiwa mkali anasema namnyanyasa! Mwe!!!!

Kama wewe ni muislam oa mke wa pili tu huyo wa kwanza atie akili. wanawake wengine bwana???
 
Hiyo nyumba ndogo inajifanya kukupenda na kukujali ili umuache mkeo, ukishamuacha na kumuoa yeye ndio utajua tabia yake iliyojificha
 
Hapo kati mamsapu aliniletea sana za kuleta na siku moja akanitamkia wazi kuwa amechoka kuishi na mimi (baadae aliomba msamaha akasema alipandwa na hasira). Kipindi tulichochuniana nikakutana na kadem fulani na nikawa nimeamua mamsap akisepa tu, navuta jumla hako kadada.(ni kadada kwa sababu kiumri nakazidi sana halafu ni kipotabo). Sasa wife hakusepa wala nini na mimi nikawa nimekolea nje mpaka nimepangishia chumba na gheto nimelikamilisha. Wife alikuja futa kauli zake za kuondoka hazingui tena na kawa mpole na mwenye heshima mpaka naona aibu kuendelea na nyumba ndogo. Wife Sitaki kumwacha na nyumba ndogo naona huruma kummwaga kwa sababu yaani kakolea kishenzi. Sidhani kama atamwamini mwanaume mwingine Mimi nikimtosa. Naogopa kumwambia wife nataka oa mke wa pili kwa sababu atasepa, japo ningewamudu na napenda wake wawili. Kitu kingine mamsap hapendi kujishughulisha na utafutaji hela wakati hii nyumba ndogo inajituma kwenye utafutaji kishenzi (mchaga), mara kadhaa ashanikwamua kwenye vishida vya lakilaki hizi. Sasa nipo kwenye dilemma!!!

Acha uhuni wewe.huyo barmedi uliyempangishia sio chochote,kwa hiyo unamwamini barmedi wakati ni cha wote??? mkeo hajishughulishi sababu kila wakati anawaza uhuni wako wewe.kwa hadhi yako na ulivyo wewe ni mtu mzima sana achana na hayo mambo ndandawamalenja
 
Last edited by a moderator:
Mbona kama unaelekea style fulani hivi ya kulelewa??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom