Scott junior
JF-Expert Member
- Mar 24, 2022
- 2,376
- 3,136
Wakubwa kwema, Tafadhali naomba ushauri mimi ni kijana wa miaka 32 sijao ila nina mchumba ambaye tuna mpango wa kuoana mwaka huu na maali nimeishapeleka kwao.
Ni mwanamke ninayempenda ambaye nimekaa naye kwenye mahusiano takribani miaka mitatu ila kipindi nimeanza mahusiano nae tulisumbuana kidogo nikapata mwanamke nikaanzisha mahusiano.
Japo sikuwa na malengo naye kwa bahati mbaya au nzuri akashika ujauzito, ila kipindi hicho hicho nikarudiana na mpenzi wangu ambaye ninampango wa kumuoa,kutokana na umri kuwa umesogea na sina mtoto nikakubali uyo mwanamke azae ili nimtunze mtoto atakayezaliwa.
Mtoto kazaliwa wa kiume na nikawajibika kama baba kumtunza mpaka saivi ana umri wa mwaka mmoja.
Huyu mwanamke niliyezaa nae ni mtu wa nyumbani bukoba na mwanamke ninayetaka kumuoa ni mtu wa mbeya.Nafanya kazi serikalini na nimeishajenga nyumba morogoro maana ndo nimeamua kuweka maisha yangu.
Mwanamke ninayetaka kumuoa aligundua kuwa nimezaa na mwanamke mwingine tukagombana lakini akakubali kunisamehe na akasema amekubali kuishi na huyo mtoto.
Changamoto mwanamke ninayetaka kumuao saiv amezidisha wivu anakagua simu mara kwa mara na kunifatilia sana.
Changamoto nyingine mtoto amekuwa mkubwa inaniwia vigumu kumfanya mtoto wa nje ya ndoa pia huyu mwanamke ninaetaka kumuoa anataka aje kuishi na mdogo wake mwenye miaka 10 ambaye anasoma nimtunze.
Mimi kitu ambacho mimi kinaniwia kigumu nikifikilia nitunze watoto wa watu wakati wakwangu yupo nje,
na pia kuanza kutunza familia ya kwao wakati mimi malengo yangu ni kuoa mwanamke ambaye tutajenga Familia yetu kwanza wengine tukawapa kipaumbele baadae.
Kinachonisukuma kumuoa huyu mwanamke niliyechumbia ni mwanamke mwenye akili nyingi za maisha na kinachonizuia kumuoa mwanamke niliyezaa nae namuona ni mwana mke ambaye hana future.ila wazazi wake na ndugu wananishinikiza nimuoe kisa nimemmzalisha.Naomba ushauri wenu niko njia panda.
Ingawa mbeba maono ni mwanaume.
MWANAUME MWENZETU ANAOMBA USHAURI.🙏🏻
Ni mwanamke ninayempenda ambaye nimekaa naye kwenye mahusiano takribani miaka mitatu ila kipindi nimeanza mahusiano nae tulisumbuana kidogo nikapata mwanamke nikaanzisha mahusiano.
Japo sikuwa na malengo naye kwa bahati mbaya au nzuri akashika ujauzito, ila kipindi hicho hicho nikarudiana na mpenzi wangu ambaye ninampango wa kumuoa,kutokana na umri kuwa umesogea na sina mtoto nikakubali uyo mwanamke azae ili nimtunze mtoto atakayezaliwa.
Mtoto kazaliwa wa kiume na nikawajibika kama baba kumtunza mpaka saivi ana umri wa mwaka mmoja.
Huyu mwanamke niliyezaa nae ni mtu wa nyumbani bukoba na mwanamke ninayetaka kumuoa ni mtu wa mbeya.Nafanya kazi serikalini na nimeishajenga nyumba morogoro maana ndo nimeamua kuweka maisha yangu.
Mwanamke ninayetaka kumuoa aligundua kuwa nimezaa na mwanamke mwingine tukagombana lakini akakubali kunisamehe na akasema amekubali kuishi na huyo mtoto.
Changamoto mwanamke ninayetaka kumuao saiv amezidisha wivu anakagua simu mara kwa mara na kunifatilia sana.
Changamoto nyingine mtoto amekuwa mkubwa inaniwia vigumu kumfanya mtoto wa nje ya ndoa pia huyu mwanamke ninaetaka kumuoa anataka aje kuishi na mdogo wake mwenye miaka 10 ambaye anasoma nimtunze.
Mimi kitu ambacho mimi kinaniwia kigumu nikifikilia nitunze watoto wa watu wakati wakwangu yupo nje,
na pia kuanza kutunza familia ya kwao wakati mimi malengo yangu ni kuoa mwanamke ambaye tutajenga Familia yetu kwanza wengine tukawapa kipaumbele baadae.
Kinachonisukuma kumuoa huyu mwanamke niliyechumbia ni mwanamke mwenye akili nyingi za maisha na kinachonizuia kumuoa mwanamke niliyezaa nae namuona ni mwana mke ambaye hana future.ila wazazi wake na ndugu wananishinikiza nimuoe kisa nimemmzalisha.Naomba ushauri wenu niko njia panda.
Ingawa mbeba maono ni mwanaume.
MWANAUME MWENZETU ANAOMBA USHAURI.🙏🏻