Evarm
JF-Expert Member
- Aug 30, 2010
- 1,934
- 1,400
wana mtoto mmoja wa kuzaa na mwingine wa ndugu ambaye ni yatima ila wanalingana kiumri na wote wanaishi nao.
hapa sister haongei kitu zaidi ya imetosha, na huyo bwana amesafiri jana tu
na pia hataki kumwuuliza maana anasema kuuliza si utatuzi maana kwa mtu mwenye akili anajua alkua anayafanya hayo kwa sababu gani! yeye anasem tu imetosha
Pole sana mama D, ila nahisi huyo mwanaume anapata hela ya kutosha ila sababu inagawanywa familia mbili tofauti na ndio maana inaonekana haitoshi.
Mwambie dadako asitishe misaada kwenye familia ya huyo mwanaume na ajijenge kimaisha vizuri, pia ahakikishe watoto wake wanasoma vizuri bila ya shida.
Haina haja ya kuongea tena na mumewe kuhusu hilo jambo kwani amesalitiwa muda mrefu sana na amejiona ni haki yake kuendelea kumsaliti dadako.
Mwisho aanze maisha kivyake yaani aachane na huyo mwanaume kwani siku hizi magonjwa ni mengi sana.