Registered_jf
JF-Expert Member
- Nov 27, 2024
- 920
- 1,454
Nina jambo ambalo ningependa mnishauri, linanisumbua sana. Nisaidie kufanya maamuzi.
Nina miaka 29 ni baba wa watoto wawili. Nimeishi na mke wangu toka 2020 nilipomaliza chuo. Tumepishana umri kidogo yeye ana 34.
Wakati tunakutana alikuwa ameajiriwa na immediately tukawa tumeclick maana nilimuona ni mwanamke mchakarikaji. Tulianza kuishi pamoja baada ya kuona hamna haja kulipa kodi mara mbili nikahamia kwake.
Baada ya miezi 5 wife akapata ujauzito, kiukweli sikuwa tayari kuwa baba lakini niliona wife ana matumaini makubwa sana na kuanzisha familia nikaogopa kumdisappoint tu nikaamua tuendelee kuishi kama familia.
2021 nikapata ajira, ni kama wife alinifanyia connection nikapata pa kuanzia maisha nashukuru Mungu. Na familia pia ikazidi kukua.
Sasa kadri maisha yalivyozidi kusonga ndivyo mapenzi yanavyozidi kupungua kwa mke wangu sielewi. Naona kama nilikurupuka kuoa hivi, au ni kama nilioa kwa sababu ya uoga wa maisha.
Huyu mwanamke kiukweli moyoni simpendi ila naishi nae tu ilimradi kila nikitoka kazini najikuta tu najichelewesha kurudi nyumbani sababu sitaki maongezi mengi na huyu mwanamke. Sina furaha nikiwa nyumbani ila sionyeshi.
Nimejikuta tu nimekuwa mtu wa kuwa na mademu wengi huku nje tu angalau tu nafsi iridhike, nyumbani narudi tu kuzuga. Nafanya mapenzi nae ile tu nitimize wajibu lakini sina furaha.
Sijui kama unanielewa? Huyu mwanamke hana kasoro yoyote amefanya kila kitu mwanamke anatakiwa kumfanyia mume wake lakini bado roho haijamkubali mwisho wa siku najikuta natafuta furaha nje kutoka kwa wanawake wengine na michepuko, sasa sielewi ni mimi au na wanaume wenzangu wanaoishi kwenye ndoa wapo hivo au inakuwaje.
Najiona kama vile naishi ndani ya jela la kujitakia. Naombeni ushauri.
(Kutoka page ya Lawi Murunga)
Nina miaka 29 ni baba wa watoto wawili. Nimeishi na mke wangu toka 2020 nilipomaliza chuo. Tumepishana umri kidogo yeye ana 34.
Wakati tunakutana alikuwa ameajiriwa na immediately tukawa tumeclick maana nilimuona ni mwanamke mchakarikaji. Tulianza kuishi pamoja baada ya kuona hamna haja kulipa kodi mara mbili nikahamia kwake.
Baada ya miezi 5 wife akapata ujauzito, kiukweli sikuwa tayari kuwa baba lakini niliona wife ana matumaini makubwa sana na kuanzisha familia nikaogopa kumdisappoint tu nikaamua tuendelee kuishi kama familia.
2021 nikapata ajira, ni kama wife alinifanyia connection nikapata pa kuanzia maisha nashukuru Mungu. Na familia pia ikazidi kukua.
Sasa kadri maisha yalivyozidi kusonga ndivyo mapenzi yanavyozidi kupungua kwa mke wangu sielewi. Naona kama nilikurupuka kuoa hivi, au ni kama nilioa kwa sababu ya uoga wa maisha.
Huyu mwanamke kiukweli moyoni simpendi ila naishi nae tu ilimradi kila nikitoka kazini najikuta tu najichelewesha kurudi nyumbani sababu sitaki maongezi mengi na huyu mwanamke. Sina furaha nikiwa nyumbani ila sionyeshi.
Nimejikuta tu nimekuwa mtu wa kuwa na mademu wengi huku nje tu angalau tu nafsi iridhike, nyumbani narudi tu kuzuga. Nafanya mapenzi nae ile tu nitimize wajibu lakini sina furaha.
Sijui kama unanielewa? Huyu mwanamke hana kasoro yoyote amefanya kila kitu mwanamke anatakiwa kumfanyia mume wake lakini bado roho haijamkubali mwisho wa siku najikuta natafuta furaha nje kutoka kwa wanawake wengine na michepuko, sasa sielewi ni mimi au na wanaume wenzangu wanaoishi kwenye ndoa wapo hivo au inakuwaje.
Najiona kama vile naishi ndani ya jela la kujitakia. Naombeni ushauri.
(Kutoka page ya Lawi Murunga)