Wakuu kwanza poleni na majukumu ya siku. Kiukwel mwenzenu nipo katika hali ngumu, nilikuwa kwenye mahusiano na dada mmoja takribani mwaka umeisha. Sasa toka mwaka uanze amekuwa mtu wa vituko sana, nikaamua kupeleleza kimyakimya ila sikufanikiwa, kunà siku moja nilitumiwa msg na mtu kuwa niachane na huyo dada ila nikaipuuzia, sasa last week nikaenda kwake nikiwa hapo akampigia mtu simu katika maongezi ni kama walikuwa wanapanga mwezi wa kubeba ujauzito, aliongea muda mrefu na baada ya mazungumzo nikamuuliza alikuwa anaongea navnani, akanijibu ni rafiki tu niyapuuzie coz uwa wanataniana, ofcoz nilimbana sana kwa maswali lakini nikawa nimehisi jambo, jana nikamchukua rafiki yangu tukaenda ili aniweke wazi kwasababu tokabmwaka uanze simuelewi, kiukweli alikiri aliyoyaongea na huyo kaka na akasema yupo nae kwenye mahusiano kitambo sana ata kazi alimuunganishia yeye hivyo pia ngumu kutengana nae, wakuu niliona kama utani vile nikaanza kumbembeleza asifikie hatua hiyo ila akakomaa na msimamo wake, sie tukaondoka nakumbuka usiku nimemtumia msg nyingi sana za kuonyesha jinsi gani ana thamani kwangu, cha kusikitisha kascreen msg then akamtumia Mike ambaye ni mtu wake kama alivyodai, Mike kachukua namba akanipigia simu leo mchana kuwa niachane na huyo binti kwani ni mchumba wake na ni jukumu lake, kusema ukweli nilimjibu mshkaji sorry bro sikujua japo moyoni kimeniuma kupita kiasi, sina amani ata kidogo, naombeni ushauri tu nichukue harua gani, maana ksemà kweli bado sijaridhika, au na mimi nimthibitishie Mike kuwa nilikuwa nae kwenye mahusiano?