Naombeni ushauri ndugu zangu

Naombeni ushauri ndugu zangu

sawa mkuu ila kila nikimwangalia yule bint mwingne roho inashndwa kabisa kuwa mbali nae

Pole ndugu sasa hivi ni mrembo piga picha 20yrs to come atakuwaje? Atakuwa kazaa na hivi ni kilaza kazaa vilaza maisha ni magumu mzigo wote wa majukumu umeachiwa wewe i am sure utamkumbuka uliyemwacha.
 
oa unayempenda......ila kataa katakata kuchukua hela ya huyo dada.......na umwambie ukweli kuwa hauwezi kuwa nae........
 
Pole ndugu sasa hivi ni mrembo piga picha 20yrs to come atakuwaje? Atakuwa kazaa na hivi ni kilaza kazaa vilaza maisha ni magumu mzigo wote wa majukumu umeachiwa wewe i am sure utamkumbuka uliyemwacha.

Sio kumkumbuka tu, atataka na kurudi lkn ndio itakuwa imemegwa kwake.
 
Kumbuka malipo ya dhambi ni umauti. Na mwisho wa ubaya ni aibu. Mazuri yote anayokufanyia leo hii ukimfanyia ubaya utakuja kuumbuka vibaya sana. Chagua mwenyewe nguvu ya pesa bila mapenzi, au nguvu ya mapenzi bila pesa. Acha tamaa, tamaa mbaya.
 
Agata, usituogope wanaume sbbu sio sote tupo kama huyu mleta mada, tupo tunaojitambua na wapo wanaojitambua, kwa hiyo huna sbbu ya kutuogopa wanaume.

wengi mpo ivyo fwatilia topic nyingi zinazoletwa na wakaka jf
 
Duu!huyu jamaa naye wa ajabu..Kama kweli humpendi na huna mpango naye mwambie ukweli,usiendelee kumpotezea bint wa watu muda,,sijui utaanzia wap!
 
hapana mkuu hata mie nna profesion yangu nzuri tu ila ndo ajira kitendawil ndo ninauza hii midosho

Kila lenye kheri kijana lakini kumbuka kuwa ukiwa msituni huoni msitu,unaona miti tu.

Kuwa makini sana kwenye hii issue la sivyo itakugharimu na utajutia.

Hivi what if huyo form 4 ni mgumba? Utaishi naye hivyohivyo au utampiga chini?
 
Kama huyo dada wa Iringa yupo jf hope hii topic itamzindua ajue hana lakr
 
Nilifikiri wanaume wana uwezo mkubwa wa kufikiri kuliko wanawake,kumbe sivyo na hapo ndipo tunapowashinda.

Mwanamke akijua tu una pesa au una uwezo wa kumlisha na baadae kuja kuhudumia watoto vizuri na ndugu zake basi hata kama ni kibogoyo atalazimisha upendo mpaka utakuja tu.Utapewa majina mengi saaana,mara honey,dear,my love sijui nini ilimradi tu mambo yaende na kweli baadae wanaishi hadi wanazeeka pamoja.

Sasa nyie mnabaki kuangalia sura, haya shauri yako
 
umeniudhi sana mleta mada nilikua nasoma kama guest imenibidi ni log in nikupe za uso
Huyo mdada anaye kupenda sana ndio mzuri wa kumuoa ,anaakili ya maisha,msomi,na atakuja kua msaada mkubwa katika maisha yako
Acha na mambo ya muonekano wa nje watu wameoa wanawake wabaya kwa sura lakini kichwa ni very intelligent saiv wanafurahia maisha saafi .Sasa fanya blunder uje kujutia maishani
"Mkataa pema pabaya panamuita"-wahenga
 
Oa tu huyo wa O level ndo mzur zaid huyu mwngne mwambie humpend na asikutumie hela zake.
 
Kama uujampeda usichukue pesa zake....muache ikiwa nado mapema usije kumtesa badaee...pesa sio kila kitu raha ya mapenzi mpendane usiwe na MTU usiyempenda
kuwa na uyo uliyempenda....
 
Uzuri wa mwanamke ni tabia yake! Na hiyo baada ya miaka kadhaa unadhani nawewee utabaki na ujana ulio nao sasa!!! Mpende anayekupenda
 
Uzuri wa mwanamke ni tabia yake! Na hiyo baada ya miaka kadhaa unadhani nawewee utabaki na ujana ulio nao sasa!!! Mpende anayekupenda

Nadhani anahisi maisha ni kesho aiseee
 
Unaonekana bado mtoto sana wewe...
 
Mkuu Waballa, ni mara chache sana waliobahatika huweza KUMAIZI kuwa hii ni Bahati napaswa kuitumia. Mara nyingi bahati ukiipata huiona mtu alie kando, muhusika huwa mara nyingi hilo halijui.Lakini huja kujua inapokuwa imeondoka kwenye himaya yake. Huyu muungwana anaingia ktk kundi hili.Na nnachokiona mbele ya safari huyu mshikaji atarudi kwa huyu mwanamke ( kama itatokea atamuacha na kwenda kwa huyu aliyempenda) lkn itakuwa kachelewa. Maana wachache wanaojua maana ya bahati watakuwa washamchukua.Hili neno halianguki. "Ule msemo wa ukishikwa shikamana" muungwana umempitia mbali.NAKUBALI MISEMO YA WAHENGA,".... KWELI. KWENYE MITI HAKUNA WAJENZI.
Dah...nimependa ushauri wako!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom