Mkuu nasikitika lakini pia nafurahi kukwambia kuwa wewe bado hujakua. Bado mtoto wewe na hujui maana ya ndoa.
1. Kuchepuka ni maamuzi na haina uhusiano na kuoa mke anaye kuvutia kwa sura na maumbile. Una uhakika gani kuwa ukioa huyo unaye muona ni mzuri hauto chepuka? Hakuna mwanamke mzuri duniani, ukiwa na fikra hizo siku utakutana na mzuri zaidi ya huyo kilaza wako aliye ishia kidato cha IV, sujui utamuacha kisa umepata mzuri zaidi yake
2. Aliye kwambia uzuri ndio utakuza familia bora ni nani? Maisha ya sasa magumu kuanzia malezi Mpaka matunzo ya watoto, sasa wewe oa huo mzigo ambao mwenyewe unasema hauna akili ya maisha halafu uone
3. Mkisha zoeana Ndani ya ndoa uzuri unakuwa sio ishu tena bali tabia ndio inakuwa jambo la muhimu.
Nakushauri muoe huyo unayesema ni mzuri maana ndio unalotaka kufanya kwasababu unatumia akili za Ujana za vijiweni. Kila la kheri kwenye kujizamisha kimaisha