Post zingine ukisoma unapata hasira sema tu inabidi tuvumulie! Mkuu
jamiimemba, acha kujifanya unajua kupenda sana kuliko wenzako! Ni kweli kabisa kwamba busara ya mapenzi inashawishi kwamba fuata kule moyo unakokutuma lakini si mara zote moyo unakuwa upo right... and I hate to say this, more often than not, moyo huwa hauna uwezo wa ku-anticipate for the future coz' unatawaliwa na emotions! Mara zote hakikisha moyo unaupa ushirikiano wa kutosha kutoka kwenye akili zako otherwise, you'll always be a failure! Hata wanyama wa mwituni wanapenda... ajabu hata kuku nao wanapenda na ndio maana si ajabu kuona jogoo linamtoa nduki jogoo mwenzako anayeona anamlia mingo kademu kuku wake! Lakini pamoja na wanyama kupewa uwezo wa kupenda sawa na mimi na wewe, lakini Mungu amewanyima akili zinazotawala utashi na ndio maana wanyama wanawapanda wazazi na binti zao!!
Moyo wako unampenda mtu mwingine... je, umejiridhisha kwamba nae anakupenda kama unavyompenda wewe? Iko hivi! Ni heri kuishi na mpenzi anayekupenda hata kama humpendi kihivyo kuliko kuishi na mpenzi asiyekupenda lakini wewe unam-feel ile mbaya! Case ya pili ni kujitafutia machungu ya kila mara lakini case ya kwanza, itakuwa ni kumtafutia mwenza wako machungu ya mara kwa mara! Lakini kwavile ni wewe mwenyewe utakuwa umeushirikisha ubongo wako kufanya maamuzi, basi kuna uwezekano kwamba hutakuwa chanzo cha maudhi ya mara kwa mara kwa mwenza wako... kinyume chake, huwezi kumfanya yule unayempenda(huku akiwa haja-fall kihivyo kwako) wewe aushirikishe ubongo wake kwa ajili yako wewe...
Mwanamke anakupenda ile mbaya... mbaya zaidi umezaa nae! Si hivyo tu, ni mpenda kujenga badala ya kubomoa! Anaamua kujipiga pini kwa kuchukua mkopo kwa ajili yenu!
Anyway, talk quitely to your heart na kama kweli you feel nothing about her, better you let her go! Usijaribu kuchukua picha zake (kama unazo) ukajaribu kutafuta kitu kitakachokushawishi umpende! Itoshe tu kujiuliza na kuyatafakari kwa kina ni mambo gani ungempenda mke wako awe nayo... haya mambo will never and ever be seen through your heart but your brain, centre of judgement!