Naombeni ushauri ndugu zangu, nakaribia kuchanganyikiwa

Saoka

JF-Expert Member
Oct 23, 2018
405
565
Habari za muda huu Wakuu. Niende direct to the point.

Mimi ni kijana umri ni miaka 24 nimemaliza chuo kikuu mwaka jana mwezi wa 9 Ila kiukweli bado sijafanikiwa kupata ajira mpaka hivi ninavyoandika hapa bado na fight popote ili niweze kujishikiza na niweze kupata chochote mkono uende kinywani.

Japokuwa bado nipo kwa wazazi na napata mahitaji yote vizuri tokea nimalize ila nikaamua kujiongeza na kutaka kutoka hapa nyumbani niweze kwenda hata mikoani huko kutafuta njia yeyote ya kujikwamua hata kama sitapata ajira ila nipate pa kujishikiza hata kama ni mchongo (kazi yeyote ya kufanya).

Tatizo lina kuja upande wa wazazi hawataki kabisa nitoke hapa nyumbani na nikisema nijishughulishe na vishughuli vidogo vidogo vya kawaida ila naona bado kama sitafanya kama ninavyotaka kutoka nje ya mkoa kwenda huko kusaka life.

Tatizo linakuja hapo upande wa mzazi hataki nikae mbali na nyumbani kwa kuhofia labda kuteseka au huko niendapo.

Wakuu naombeni mnishauri nitatokaje hapa na ukicheki muda unakwenda na sio vizuri kwa mtoto wa kiume kuendelea kukaa hapa nyumbani. Yaani nakosa kabisa njia ya kufanya.
 
Saoka,
pole sana dogo,,,,ndo maisha yenyewe hayo,ushauri wangu ni kwamba kama hauna specific activity ambayo unaenda kuifanya huko unakopanga kwenda basi baki nyumbani, fanya kazi kwa bidii hapo home,jitume sana,nyumbani ni sehem sahihi ya ww kusubir mambo yako yanyooke kama hauna shughuli maalum ya kufanya huko mikoani
 
Mkuu kwa umri huo na kama umeshamaliza chuo wewe ni mtu mzima sasa, unaweza kujitegemea, kuwa na familia na kubeba majukumu. Kuendelea kukaa hapo nyumbani ni kujilemaza na kupoteza muda bila sababu. Kumbuka sasa unatakiwa kujenga maisha yako na inabidi wazazi waelewe hivyo. Hebu jiulize hapo nyumbani utakaa hadi lini? Unachosubiri hasa ni nini? Je kesho na keshokutwa wazazi wasipokuepo utaishi vipi..?
 
Waombe mtaji uanze business. Kwani wew unahis ukiondoka hapo nyumbani na kwenda mikoa mingine kutafuta kazi utazipata?

Wazazi wako wameona hesabu zako zitafeli.

Chagua mkoa unaotaka kwenda kutafuta kazi, waombe mtaji wazazi wako, halafu anza biashara za kusafiri katika huo mkoa, unakuwa unaenda na kurudi home huku ukitafuta hizo kazi, japo unaweza kujikuta unanogewa na biashara na kujikuta hauna tena mpango wa kutafuta kazi.

Najua unao uchungu wa kusoma hiyo degree na unataka uifanyie kazi mdogo wangu, lakini kwa dunia ya leo, inabidi ukubaliane na matokeo kwani kazi zimekuwa ni chache. Kwa sasa ni kutafuta hela, degree ni kuelimika tu. Kuna watu walisoma degree miaka kumi iliyopita lakini hawajawahi kuzifanyia kazi, yaani wanapiga dili tofauti kabisaaaa.
 
We sio mtoto mdogo huo ndo umri wa kutafta. Kaa na wazazi waeleze wazi kumbka miaka 3 ijayo si muda mrefu ujao utakua na miaka 27. Shangaa shangaa 30 hii hapa imegonga hodi.Nakupongeza kwa kujtambua mapema
 
Dogo tuliza tako kaa nyumbani,kama unapata mahitaji yote muhimu hapo nyumbani una haraka ya nini!!!!! Maisha sio simple kihivyo.Unanikumbusha stori ya kwenye bible ya mwana mpotevu aliyepewa mtaji akaenda kutapanya na kuishi maisha magumu kama shetani mwisho wa siku aliishi kama shetani na mwisho wa siku akarudi kwao alipotoka.

Sent from my TECNO_W4 using JamiiForums mobile app
 
We sio mtoto mdogo huo ndo umri wa kutafta. Kaa na wazazi waeleze wazi kumbka miaka 3 ijayo si muda mrefu ujao utakua na miaka 27. Shangaa shangaa 30 hii hapa imegonga hodi.Nakupongeza kwa kujtambua mapema
Shukrani kaka ngoja nijaribu kukaa nae tena
 
Saoka,

Kama unapata mahitaji yote vizuri kutoka kwa wazazi, unaweza fanya mambo haya
1. Tafatu sehem ya kujitolea japokuwa huajasema umesomea nini. Mfano mimi nimemaliza chuo mwaka juzi na nimesomea BAF baada ya kumaliza tu wazazi waliniambie ni rudi nyumbani nikakataa nikasema hadi nifanye mahafali lakini moyoni nilikuwa sitaki kuludi home nikawa nakazana kutafuta sehem ya kuafanya kazi bure kabisa yapo kuwa nilitumia mwezi 9 kupata (toka 8, 2017 nikaja kupata sehem ya kujitolea bure bilakulipwa hata tshs10 mwz 6,2018. Kipindi chote hicho sikuludi nyumbani, life nililokuwa na na ishi kipindi chote hicho Mungu ndo anajua. Baada ya mwezi 2 nikaonekana kwa maboss kuwa najua kazi nikapata sehem nyingine hapo ndo ukawa mwazo wakulipwa hadi leo nipo hapo, japo kuwa silipww vzr lakini naweza kulipa kodi ya nyumba, chakula , mavazi na kidogo na save na kusaidia ndg zangu pale wanapopata matatizo

2. Unaweza ingia kwenye ujasilia mali mdg mdg. Kwa kuangalia unapenda nini . Mfano biashara ya nguo au chakula cos kila siku watu wanaitaji vitu ivi. Hasa fanya unacho taka au moyo unapo taka kwa kuanza kidogo kidogo

Kwa haya machache siku ya leo japokuwa ninamengi ya kusema, cos hadi leo sijarudi home official japo kuna siku nilipita home niliitwa kwenye interview sehem, ndo mikapita kuwasalim
 
Upo mkoa gani,sikia usiende kinyume na wazazi wako japo sidhani kama wapo aware na hii time tuliopo,maisha yanayokuzunguka fursa zipo pambana mwaka mzima usave huku unakula bure na kulala bure,save kwa nguvu zote by then utakua na plan wakati uo 25 sio mbaya mafanikio ni kucheza na strategy na akili zako si kukimbizana na umri, uwe na kiasi ukijilipua na return
 
LUKAMA,
Mkuu ,Tatizo naona nikilazimisha kuondoka nahisi kama sitabeba zile baraka za mzazi yaani naona atakuwa ananung'unika mno yani hapo ndio nazidi kuwa Totally Confused
 
Upo mkoa gani,sikia usiende kinyume na wazazi wako japo sidhani kama wapo aware na hii time tuliopo,maisha yanayokuzunguka fursa zipo pambana mwaka mzima usave huku unakula bure na kulala bure,save kwa nguvu zote by then utakua na plan wakati uo 25 sio mbaya mafanikio ni kucheza na strategy na akili zako si kukimbizana na umri, uwe na kiasi ukijilipua na return
Najiskia aibu mno mpaka muda huu nikiwa nipo nyumbani
 
Asee miaka 24 unauliza utatokaje. Oky shida uliyonayo nikwamba bado unachoice either ubaki au uondoke.

Na kwa mantiki hiyo hata ukiondoka ukipigwa tatizo tu kidogo utakuwa unakumbuka nyumban, life litakushinda utakuwa mzigo tena kuwaambia wakutumie pesa za matumiz.

Kama umeamua kutoka kwa dhat wewe toka mfano mm hapa unanizid kama mwaka, familia inanitegemea ,sina back up yoyote lakini nakomaa na maisha hapa town japo life ni gumu sana,, kuongea mwenyewe barabaran kwangu nikitu cha kawaida sana

lakini najua one day nitarudi home na ushindi mzito kwa furaha ,sasa kwann wewe usitoke kujaribu maisha bro.
 
Back
Top Bottom