Naombeni ushauri/mke wangu "ana sauti" kwangu

Kaa na mkeo!Vunja ukimya zungumza naye,kila mtu atoe dukuduku lake! ili kama uliwahi kumtendea mabaya omba msamaha yataisha! Kumbuka Ndoa ni ya WAWILI huku Mungu akiwa kati yenu! Nakushauri kama inawezekana tafuteni mahali palipo na utulivu mbali na nyumbani ili mkapate kuzungumza vizuri kila mmoja atoe aliyonayo! then msameheane na kuanza upya! Usikimbilie kushtaki kwa wazazi ,ndio maana ya kuwaacha babayo na mamayo na kuambatana na mkeo, pia hata hao wazazi wana matatizo yao! Ikishindikana nendeni kwa viongozi wenu wa dini wakawasaidie.
Pia ninamashaka na hiyo ndoa uliilazimisha nini?
 
hapa ndipo namkumbuka Martin Lawrence ktk Badboys 1 movie,..."that is marriage, you sleep with a woman but you don't get" I know one fella had the same issue na mkewe, alitoka nje na akahakikikisha mkewe kajua, na mkewe alivyo mjinga aliitisha kikao cha wazazi eti kumshtaki mume, on a meeting mke alibwabwaja muda mrefu sana akijua anammaliza mumewe kwa sababu waliokuwepo na wazazi wa wake tu na matron na mumewe, jamaa spoke only two line, na kibao kikamgeukia mwanamke. since then mwanamke alishika adabu yake.

Ndio ushauri ninaokupa fanya kweli, au anakudunda? Kama jibu ni "NO" gonga nje siku akitaka yeye we kataa mwisho atajua tu kuwa hapa kuna namna. Upande mwingine labda hana hamu ya ile kitu (labda ana maradhi yanayomkwaza hapo unaweza kutafuta ushauri kwa madaktari)
 
Hapo kuna tatizo aidha kwako/kwake..hiyo huduma huitoi kwa ufasaha.. au unalelewa (mme magazeti) kama ndiyo learn how 2 rise ur masculine..kama wife ndio wale wa mdomo wa chuchunge..tafuta mama mtu mzima unayemwamini amfunde..pole sana kaka ndo ukubwa huo.
 
Utingo-what words did he uses ,I might need them-ahaaaaaaaaaha!

Tunafanya mapenzi anapotaka yeye kwa mwezi mara moja au baada ya miezi miwili mpaka mitatu. Nimetoka nje kwa makusudi ili ajue na mjue, akitaka anaweza kuondoka kwani nimechoshwa na tabia hii.

---sometimes huhitaji hekima kudeal na wapumbavu.
 
Pole sana,kaka inawezekana mke wako upendo umepungua kwako,jaribu kufanya utafiti wa kina,mlivyoanza mahusiano mpaka hivi sasa kwanini kuwe na mabadiliko lakini usikate tamaa jaribu kuongea naye mkiwa wawili tangu mlivyoanza na kumuuliza kwanini anakuwa hivyo usitumie nguvu jaribu kuwa mpole wakati wa mazungumzo ili upate ukweli wake.
 
mkuu nadhani case yako inastahili kufikishwa kwa TGNP.sio wewe tu kuna wanaume wengi wananyanyaswa na wake zao lakini mara nyingi chombo cha kuwatetea hakipo.sema yote mkuu inawezekana ukirudi umechelewa unapata kichapo cha mbwa mwizi!!!
mpeleke mahakamani kupitia TGNP.
 
Pole sana kaka. Ila ulikosea njia ulioitumia kuvunja ukimya. Ilibidi ujadiliane na umueleze mkeo kuwa hauko huru.
 
Pole kaa nae umweleze, atakuelewa, kwa upole sio kwa mabavu, tatizo ushaiweka mnyonge tangu mwanzo
 
Nimekosa cha kuchangia nimeishia kucheka japo si mazuri. Akyanani! Sasa anapiga makelele kuhita watu ili iweje? Na ungemwacha atoke angewaambia nini hao majirani? My goodness! Kwa nini anakuogopa? Hata wanawake wenye vidumu sidhani kama wana behave hivyo kwa waume zao. Kuna kitu kinaendelea hapo na si suala la sauti kama unavyodhania. Labda una muumiza ainjoy. Vunja ukimya zungumzeni.

Au ana pyschological problem kubwa ambayo ni mpaka kwa wataalamu ndio wanaweza kutambua. I mean may be she has mental problems. Huwezi piga makelele ni aibu kwa majirani.
 
1 Corinthians 4-5
Mke hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mumewe anayo; hali kadhalika naye mume, hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mkewe anayo. Msinyimane haki zenu, isipokuwa kama mnaafikiana kufanya hivyo kwa kitambo tu, ili mpate nafasi nzuri ya kusali. Kisha rudianeni tena mara, ili Shetani asije akawajaribu kwa sababu ya udhaifu wenu.
nimeipenda hii lolyz,,,,,kaka hapo mke huna ila ndo majaribu ya ndoa hayo unatakiwa huyashinde,kaa nae mahali muulize kwa upole kuwa tatizo ni nini hasa,ikishindikana muitie wazee,unyumba ndo msingi na chakula cha wanandoa
 
Mmh! Umesema anakuheshimu nawe unamshimu. Basi kila mtu anaheshimu hisia za mwenzake. It's NOT true story jipange kaka!
 
Tatizo naliona unalo mwenyewe coz unakubali kusema mkeo ana sauti zaidi yako. Sasa sijui ndo ana kipato zaidi au anaongea kwa nguvu sana. Kama umekubali endelea na maisha yako ya kukaliwa kama usingekubali wala usingekuja kuomba ushauri hapa coz ungeshajua la kufanya. Mwanamke yoyote ukimpa nafasi lazima akuchezee! We sema tu kama na nguo unamfulia!

in red, mkuu umeua...............
 
1 Corinthians 4-5
Mke hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mumewe anayo; hali kadhalika naye mume, hana mamlaka juu ya mwili wake, bali mkewe anayo. Msinyimane haki zenu, isipokuwa kama mnaafikiana kufanya hivyo kwa kitambo tu, ili mpate nafasi nzuri ya kusali. Kisha rudianeni tena mara, ili Shetani asije akawajaribu kwa sababu ya udhaifu wenu.

iMEKAA VYEMA HIYO !
 
Back
Top Bottom