Naombeni ushauri katika hili

Naombeni ushauri katika hili

KIDHEA, ni mengi sijayazungumza kwani kila ninavyozidi kuandika maumivu hayauachi moyo wangu. Lkn mawazo niliyoyapata hapa hakika naendelea kujifunza na mwisho nitatoa final say and decision. Kisha nianze safari ya matumaini.
 
Asanteni kwa ushauri wanajf kama ni kupiga nilishapiga mpaka nikapeleka hosipitali ya rufaa mkoa flani hivi lakini sioni sababu ya kumpiga tena. Na isitoshe alishasema nikimpiga tena ananifunga so hiyo option nimeiacha wadau.
 
pole mkuu, ukimuoa huyo lazma uje kuwa mwanafalsafa, na jihesabie kupata stroke, BP na kifo kabla hujaona wajukuu.
mshukuru Mungu umeona hayo yote mapema.
karipoti polisi kama anakutishia maisha.
kimbia kabla hujazeeka kabla ya umri, ila usisahau kumlea mwanao.
 
Nina miaka 28 kwasasa, ni university graduate na nimeajiriwa serikalini. Nina mwanamke ambaye bado hatujafunga ndoa lakini pia bado hata nyumbani kwao sijajitambulisha. Naye pia ni graduate na yupo kazini pia. Umri wake ni 25yrs, kwa ufupi tulikutana chuoni na tuna miaka kama minne hivi and we have been blessed with a lovely and precious daughter aged 3yrs now. Ok kilichosababisha niandike uzi huu ni kutokana na anayonifanyia huyu mwenzangu, kwa kipindi chote hicho its only 3 months labda ndio nilienjoy mapenzi naye.

1. Haishi kunitukana matusi ambayo yameenda beyond hata kuhusisha wazazi wangu.

2. Alishanitishia nikicheza ataniua kisirisiri au anifanye msukule, nilijipa moyo haiwezekani.

3. Kila ninachonunua anasema ni chetu hata kama hajui nimenunuaje mfano nimenunua uwanja na nishaanza kujenga, sijawahi kumuonesha ila niliwahi kumwambia kuwa nina mipango hiyo surprisingly hajigusi kuhusu hilo lakini kila siku anasema nyumba yetu ikiisha sijui atanya hivi mara vile.

4. Yupo busy na simu yake mara whatsapp sijui FB hata kama ni usiku. Tatizo nikijaribu kuwa busy na simu yangu analeta ugomvi.

5. Pesa zake hataki nijue anafanyia nini wala nisiulize. Kwani nikuliza ni ugomvi.

6. Habari za wazazi wangu hataki kuzisikia kabisa.

7. Kubwa zaidi ilishafika siku akanitemea hadi mate mbele ya wadogo zangu wa kike.

8. Nanii yenyewe napewa kwa masharti mpaka siku apende yeye.

9. Akijua nina pesa anataka mpaka iishe ndio aridhike. Note. Bado sijamuoa rasmi and regardless of all these anasisitiza nimvishe pete ya uchumba na nyumbani kwao niende.

Real nimepata hofu na sina hamu ya kumuoa sababu nahisi she is hunting marriage coz topic kubwa kwake ni ndoa hasa anapoona rafiki zake wamepost may be engaged au wedding pictures.

Kwa haya yote natamani kuachana naye lakini hataki kusikia hilo. Mind u, for the whole time i have been playing role kama baba na mama yake.

Naombeni ushauri wana Jf nifanyeje? Moyo umekufa sina hamu ya mapenzi kwa haya yote na mengine mengi na sioni kama ninaweza kufurahia mapenzi tena.

Usimchekee simama kama mwanaume atabadilika tu, ila usimpige chunga sana mkono wako usimpige, ila act kama mwanaume lazima abadilike tu, na hii ni nzuri zaidi kama unategemea awe mkeo. Asipobadilika baada ya ku act kama Mwanaume, basi atakua ktk kundi la magumegume na hivyo, nini ufanye itabaki ni wewe tu mwenyewe. Naamini wewe ni msomi umenielewa, chunga mkono wako usimpige, ila act kama Mwanaume.
 
sanyingine ata kwakutumia vibao inakuwa ni njia tosha yaku mfundisha mtu anapo kosea.....mpenzi wako bado anakutemea mate...umekaa tyu...!!????? huwezi kuwa mwanaume mwenzangu ww.
 
kaa ..tupa kule

Vitu vingine havihitaji ushauri.
Ukioa lazima ujutreeeeeeeeeeeeee
 
Wanaume siku hizi tumekua watu wa kulia lia kama watoto, hata wanawake wanatushangaa, yaani mtu sio mke wako anakuendesha hivyo na hata kama angekua mke wako ndio akuendeshe hivyo na wewe unachekelea tu.

Mara akutemee mate,akutukane,akunyanyase bado tu umemng'ang'nia, ashagundua huna jinsi au ulimpata kwa bahati sio level yako na wewe hutaki kuganduka acha akuendeshe na mimi nasema akuendeshe tu mara maana sasa hakuna namna nyingine, tumechoka.

Huyo mwanamke ukimuoa si atakuwekea kidole kwa mtindo huo, na wewe mbona umemganda sana kwani huwezi kupata mwanamke mwingine kwa nini ukomae nae hivyo?yaani hadi unatishiwa kifo wewr upo tu, unatishiwa kurogwa ambayo ingekua tiket ya kuachana nae wewe upo tu.

Hataki wazazi wako wewr umemganda tu tena sio mke wako wewe upo tu.
Mkuu kuna stori ukisoma unashikwa na hasira unatamani uwe karibu na mlalamikaji umtie makofi ya haja. pambaf kabisa.
 
Hivi huko shule mnaendaga kusomea ujinga?ni aibu mtu kuomba ushauri kwa jambo kama hli then unajiita graduate.una tofauti gani na deiwaka wa mtaani sasa?
Acha kabisa kumlinganisha huyu na deiwaka. Wewe ulishawahi kuona deiwaka anaendeshwa kama gari bovu na mwanamke??
 
Mkuu,wanawake wapo wengi sana!Mimi nilipitia kama yako,unfortunately nilimuoa yule mwanamke,kilichokuja kunipata na kinachonipata mpaka sasa, NAJUTA KUMFAHAMU! kuwa makini muda wa maamuzi ni sasa! Najua kumuacha ni kazi ngumu but jitahidi coz mapenzi yanahusiana na uhai mojakwamoja!
Kama wewe ulivyomuoa hata huyu atamuoa tu wallah tena, yaani uhakika wa 99% hiyo 1% ni nafasi yake ya kuchomoka. Sijui huwa inakuwaje ila kwenye ishu kama hizi yaani mtu anajua kabisa kuwa huyu mtu hanifai lakini bado tu anaendelea naye na anaoa. Inawezekana kufanywa msukule huwa inahusika pia.
 
Kiajana chukua mwanao ulee.. As for her mwache aande zake coz kama hakusaidii saiv sidhan kama anaweze kukisaidia bdae.. Life ya sasa ni kusaidiana si kutegemeana..
 
Kijana acha kulia lia...

Kwa namna ulivyoeleza inaonesha kabisa hakuna mbele baina yenu...

Na tayari inaonekana ushafanywa msukule maana hata maamuzi magumu washindwa yafanya...

Edit isomeke, "Na tayari inaonekana ushafanywa msukule maana hata maamuzi mepesi washindwa yafanya..."
 
'' ...Alishanitishia nikicheza ataniua kisirisiri au anifanye msukule, nilijipa moyo haiwezekani.."

Sorry to say this; ameshakugeuza msukule!Lile ulilosema haliwezekani naona limewezekana


Binadamu mwenye akili timamu hawezi kufanyiwa hayo yote na akabaki anaangalia tu.Something is wrong brother.....

Huitaji ushauri, unahitaji kufanya maamuzi
 
sasa unataka nn tenaa wakati tiketi umeshapewa mkuu??huitaji kuwa na diploma kuamua hilo
 
Back
Top Bottom