Naombeni pa kujiegesha wiki mbili

Naombeni pa kujiegesha wiki mbili

Deleted_account

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2008
Posts
3,385
Reaction score
3,702
Baada ya kusota kutafuta kazi hatimaye nikapata kibarua, sasa changamoto imekuja hapa ninapokaa maana kuna mtu aliniachia chumba akatoka na makubaliano ni hadi mwisho wa mwezi huu, sasa leo mwenye nyumba amekuja ghafla (hakai hapa) anasema yeye anajua chumba kipo free na ameshapata mtu amelipia kwahiyo nitoe vitu leo. Kosa nililofanya sikumshirikisha mwanzo wakti nakuja na sasa anagoma kusubiri mwisho wa mwezi.

Chondechonde ndugu zangu, mwenye hata kichumba cha stoo nijiegeshe kwa hizi siku chache tu. Kibarua nafanyia posta hivyo ikiwa sio mbali na hapo nitashukuru. Hapa ni kigamboni.

Karibu PM kwa maelezo zaidi
 
Unapofanya kazi hauna wafanyakazi wenzako au boss wako au mtu yoyote anaeweza kukusaidia?

Nauliza hivyo kwakuwa ni rahisi zaidi kupata msaada kwa watu ulio nao karibu kuliko mtu wa mtandaoni ambae hakufahamu.
 
Ikishindikana kabisa kabisa nenda msikiti wa jirani yako waombe wwkupe hifadhi angalau siku kadhaa wakati unajipanga upya..ukijieleza vizuri waislamu ni watu wema sn wanaweza kukupa msaada mkubwa zaidi

Mimi ni mkristo lkn nawakubali sn hawa watu kwenye kutoa msaada wenye tatizo la aina yako mkuu
 
Unapofanya kazi hauna wafanyakazi wenzako au boss wako au mtu yoyote anaeweza kukusaidia?

Nauliza hivyo kwakuwa ni rahisi zaidi kupata msaada kwa watu ulio nao karibu kuliko mtu wa mtandaoni ambae hakufahamu.
Kama nilivyosema sina muda mrefu hapa, hata hivyo najaribu kuongea nao na bado sijapata
 
Ikishindikana kabisa kabisa nenda msikiti wa jirani yako waombe wwkupe hifadhi angalau siku kadhaa wakati unajipanga upya..ukijieleza vizuri waislamu ni watu wema sn wanaweza kukupa msaada mkubwa zaidi

Mimi ni mkristo lkn nawakubali sn hawa watu kwenye kutoa msaada wa Aina yako mkuu
Asante kwa wazo ndugu
 
Sasa unafanya kibarua kwa ajili gani kama hakikupi hela ya chumba Walau miezi miwili...au una bet unaliwa
 
Sasa unafanya kibarua kwa ajili gani kama hakikupi hela ya chumba Walau miezi miwili...au una bet unaliwa
Ndio maana nilipanga mwisho wa mwezi tu nalipa miezi 3, tatizo huyu mwenye nyuma amegoma kusubiri inaonekana kweli ameshapokea hela kwingine. Tatizo misunderstanding ilishatokea maana nilihamia bila kumshirikisha, rejea vizuri maelezo yangu.
 
Waungwana wapo kikubwa ukipata sehemu kawe mwaminifu kwa mke wa mwenyenyumba na ukiondoka usichukue namba ya wife wala kuchora raman ya kuingilia ndani uibe.Sorry ni maneno makali lakini ndo uhalisia wa dunia ya sasa
Asante, natambua uaminifu ni muhimu sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom