Naombeni mwongozo


mkuu, hii ni TOPIC mpya kabisa (ijapokuwa ni nzuri). topic tunayojadili hapa sio pana kihivyo--jaribu kubaki kwenye hoja ya MSINGI--usiende mbali sana. hapa tunaongelea WILAYA lakini wewe unataka kutulazimisha tuumulike MKOA mzima! i think u get the logic.
 
Kwani huzijui? corporate organisations wanatumia mobile lines za voda, tigo na airtel kama simu za mezani. Si unajua ttcl ilishazimia?

sio kwamba sijui ila najua zinaitwa simu za MKONGA, haziitwi simu za MKONGE. nimefurahi jinsi ulivyoweka msisitizo, hata mimi ningependa kumiliki moja ila nina wasiwasi kama itamfaa beki 3 wangu kwa jinsi anavyokatiza mitaa.
 
Hayo ni maoni yako. Issue hii ambayo inahusu wasaidizi wa nyumbani na usalama wa familia ni pana sana kuliko wewe unavyotaka tuamini, ila kwa taarifa yako mie nimeshajitoa kwenye huu mjadala na wala sitaki maswali.

CC: Fixed Point usicheke tafadhali lol!!!! 🙂🙂🙂


 
Last edited by a moderator:
Bahati mbaya hata ujui mada ipi ya kutoa povu ila kwa kuwa umejua kusema neno hilo basi unalitumia hata mahali ambapo halina haja,mfano wako ulioutoa mbona haulingani na mada iliyopo?

haulingani kivipi?

beki 3 anaachiwa airtime kwa ajili ya emergency badala yake anaitumia kwa mambo mengine.

unampa mwanao fedha kwa ajili ya kulipa ada ya shule badala yake anatumia fedha hizo kuchezea kamari.

je, hizo statemets 2 zinazozungumzia MATUMIZI YASIYOKUSUDIWA hazina mfanano? wewe ulitaka zifananeje?

eti wadau, hakuna ulinganifu wowote hapo?
 

mi nimeweka simu ya ttcl hizi za mezani na kwetu kupata vocha za ttcl ni kazi kwahiyo nikiweka 2000 namwambia kukiwa na dharula anipigie ambapo huwa sipokei nakata then nampigia. Inaweza na kutuma sms kama hajapiga atatuma sms sasa vocha huwa haiishi cause ile line ina namba 4 tu. So hana kisingizio kuwa amempigia nani na vocha ikiisha hana ujanja wa kuipata na naweza hata siku yoyote nikaangalia salio anaogopa kama nikikuta limeisha. Every weekend nampa simu awapigie nyumbani na wote anaotaka kuongea nao. Wala sipati shida. Nimemwambia kama kwenu wakitaka wakupigie hapo ila si unajua kupiga ttcl na kijijini wengi hawapigi. Zipo za mitandao mingine ila hizo vocha ni rahisi kupata na chenji sitazikuta na simu itakuwa haina hela kila siku.
 
Unatafuta hisani ya wadau kwenye mfano wako?Uliwahi kumuuliza mtoa mada kuwa kuliwahi kuwa na tatizo zito nyumbani kwake na hakujulishwa kwa namna yoyote ile?
 
Asante rafiki.
Ila sasa nikiiblock kupiga namba nyingine si nitakuwa namwonea? akitaka kuongea na wazazi wake au ndugu wengine itakuwaje?

Kumbe unataka awapigie wazazi wake na ndugu zake wengine, sasa unacholalamika hapa ni nini hasa? Acha atumie simu vizuri, usilalamike.

Tiba
 
Mi namuelewa mtoa mada. Nimempa msichana simu namuwekea vocha lakini kukiwa na shida home always hana hela ya ku beep. Usiku utamsikia akiongea na hani na bebi wake ( wako zaidi ya mmoja). Anyway thats non of my business ila naomba kuwauliza hao wanaosema house girls nao wanapaswa kuwa na social life, I totally agree, swali ni kwamba social life ya kuwapigia simu bwana zake kupitia gharama zangu inakuwaje hii? Kwa nini asichukue mshahara wake akautumia wooote akitaka akawa na hiyo social life akawapigia mabwana wote I wouldn't give a damn! Lazima kuwe na balance bwana ajue ile ni simu ya kazini. Upo nje ya home unapiga simu fundi yupo getini amfungulie simu ipo buzy nusu saa...! Aaah jamani!
 

Nina wasiwasi hata maana ya kuelewa hujui!
 

Umsomeshe mtu halafu uje ulalamikie matumizi ya buku?

Hata kale ka kondoo kangu pale nyumbani kataikataa hii ....!!
 

Na tatizo langu ni hiyo hiyo buku ya eataimu

Hivi kama unalalamika kwenye buku ya eataimu kwenye mambo mengine inakuwaje?
 
wewe ndio mumewe, umejuaje kuwa jambo liko hivyo, kama unavyotaka tuamini kuwa ipo hivyo
 
Anawapigia wazazi wake kijijini kwao kuwajulia hali.
 
Kwani huzijui? corporate organisations wanatumia mobile lines za voda, tigo na airtel kama simu za mezani. Si unajua ttcl ilishazimia?
Nilikuwa nayo ya ttcl wakaamua kuiharibu sababu ilikuwa inawafunga kubaki home. sasa ngoja nikajaribu voda, lol!
 
Mie pia hii avatar hunifurahisha kila niionapo, ila michango yake imetulia. Napenda kuisoma michango yake.
yaani tpaul kanisaidia sana kujibu hoja katika hii mada yangu, kaielewa kupita kiasi.
Nimemfurahia sana..... keep it up mpendwa
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…