- Thread starter
- #21
Mkuu Mimi sitaki kumfanyia hivyo ndo maana nimeomba ushauri.Vijana tambueni jambo moja la msingi sana mnapaswa kulijua.
Ni rahisi sana kumshauri mtu juu ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi tu kuliko mahusiano ya ndoa.
Ndoa sio kulalana tu kitandani ukajua umemaliza, ndoa ni maagano (covenant) baina ya wawili walioamua kwa "dhati" ya kweli ya mioyo na nafsi kuishi pamoja "milele" na ndio maana inahusisha viapo .
Kaa tafakari kwa kina hilo neno "milele" lina dhana pana sana ndani yake. Na hakuna jambo lenye madhara kama kuapa, ukikiuka kiapo hubaki salama hata kidogo.
Suala la kabila la wanawake wa kipare kuwa kisima cha kijiji nadhani ni nadharia tu kwakuwa hilo linahusu mtu mmoja mmoja(nafsi) ,ni mara ngapi member wa jf wanalalamikia wenza wao kuchepuka na si wa kabila hilo?
Maamuzi ni yako ndugu
Sent using Jamii Forums mobile app