badshah
Member
- Mar 16, 2013
- 51
- 33
Siwezi kusema kama atakuwa hakupendi hapana, ila angalia kitu kimoja, je ndani ya hizo siku mbili nawe pia uko kimya? kama ni hivyo basi mtakuwa mnashindana na huwa kuna kitu kimoja kinapenda sana kutokea watu wanapokuwa katika uhusiano. kitu hicho ni kwamba kila mmoja anamtegea mwenzie aone kama anamapenzi ya kweli au la! na hata hivyo anavyowasiliana nawe labda anakupima aone ni jinsi gani uta react kuhusu suala hilo. cha msingi kabla ya kumtuhumu BF wako kwanza jipendekeze uone kama ataacha tabia hiyo. kama ataacha basi ujue alikuwa anataka kufahamu hakika yako ndani ya moyo, na kama ataendelea basi ujue ndiyo tabia aliyojichagulia ambayo usipoangalia itakuumiza kichwa na hunda ukashindwa kufanya mambo mengine.
Staryte - Elimu, Burudani na Maendeleo
Staryte - Elimu, Burudani na Maendeleo