Naomba ushauri

Tatizo wengi huingia katika mapenzi bila kujua lengo la kuwa wapenzi. Kama hamna future ya mapenzi yenu hili sio la ajabu kabisa. Kwa ushauri wangu usije kufanya tena kosa kama hili.
 
Reactions: ram
Tatizo wengi huingia katika mapenzi bila kujua lengo la kuwa wapenzi. Kama hamna future ya mapenzi yenu hili sio la ajabu kabisa. Kwa ushauri wangu usije kufanya tena kosa kama hili.
<br />
<br />
Thank u so much Lik, hiki ndicho nilichokuwa nataka kukiongea muda si mrefu. Kuna baadhi ya watu wanaingia kwenye mahusiano bila kujitambua/kujua ni kwa nini, yaani wanafanya kama fasion mradi tu nao wanadate(simaanishi ram coz am not sure)! Sasa kwa kesi kama hii sioni haja ya kulalamika coz walitakiwa kureason tangu mwanzo. Ni kosa dogo lakini bila kulichukulia uzito linaweza likakucost sana hasa kama ulinogewa ndugu yangu siku ukipigwa tipa unabaki unambwelambwela tu!
 
Pole mpenzi, alitafuta upenyo wa kukuacha ili asiumie yeye, wewe endelea na maisha yako, tulia ingia sokoni upya, utapata mpenzi atakaekujali bila kukuumiza
 
Mmh inauma kuachwa na mtu uliempenda ila usikate tamaa kwani maisha bado yanasonga na utapata mwingine, ila hujataja umri wako usije ukazeka mapema.
 
Kaona kuna kitu hapo hawezi kukirekebisha hata baada ya kurudisha penzi upya. Yaani kuna upungufu ameuona na unao toka mwanzo ila hapo kati alirudisha mapenzi aone kama itarekebishika ila kaona hakuna kitu bora ajiondoe mapema

...sawasawa kabisa, na inawezekana pia mwanaume anajijua kasoro zake ambazo hawezi tena kuendelea na ram.
Jipe moyo usonge mbele, maisha yanaendelea. Kwenye mapenzi hakuna mshindi ati nani kaanza muacha mwenziwe.
Kuacha na kuachwa yote ni kuachana. "kila likuepukalo lina heri nawe!"
 
Lakini mimi nilimwita nikamwambia kwa ustarabu kabisa na bado akakataa, kinachoniumiza mimi ni kwanini hakuniita kama mimi nilivyofanya awali badala yake from nowhere akanicall kwamba mimi na yeye basi. Anyway asante kwa usahuri!

Kaza moyo dada, ushukuru umeambiwa, mwengine hakwambii kimya kimya anakuachia manyoya!
Utapata mwengine ucjal.
 
Unaweza kufikiri hiyo miaka mitatu umeipoteza bure lakini utakuwa umejifunza mengine kwenye mahusiano. Kimsingi huna cha kufanya bali ni kusonga mbele.
 

Kwanza Kuachwa kunauma. hata kama unataka kumuacha mtu leo, ukampigia simu ili umwambie tuachane alafu yeye akakuwahi kusema muachane, roho inauma na unatamani uahirishe muendelee, ili uje umuache yeye...

Pili "hakukupotezea muda kwa three years" bali amekupa experience ya kwenye mapenzi ya miaka mitatu, next time you will be better

Tatu "what goes around comes around" na hakuna msiba usio na mwenzie. Wewe ulivyompata huyo "ulimuacha" uliyekuwa naye. Uliyemuacha aliumia kama unavyoumia wewe. Nasita kusema kuwa "mkuki kwa nguruwe....", but mapenzi is just like flowers, leo lachanua kesho lanyauka, maisha yanasonga mbele...
 
Mamii Smile hapo mwanzo wa bandiko lako angalau ungeanza na ..... baadhi ya wanaume..... wewe una generalize tuuu mamii wangu sio wote tunakuwa ma stupids wengine tuna Degree za kuwaheshimu na kuwapenda wanawake,
 
Nakusitikia kwa kuwa hujajua kuwa iyo ni "KARMA"...."what goes around comes around" ulichomfanyie mpenzi wako wa zamani ndio kimekutokea...malipo ni hapa hapa duniani .....usiende step nyingine yakimaisha bila kujifunza ilo jambo madame... ...be nice to every person aspecially those who gives you their heart....sikusemi na kushauri tuu hata me KARMA zinaniwinda natamani niombe msamaha kwa wote nliowahi waumiza.....
 
Umemjibu vizuri mno
 
ni miaka saba sasa nahisi utakuwa ushaolewa
 
Mungu hajaruhusu mpotezee tu mkuu
 
Pambana na hali yako sababu uliacha mbachao kwa msala upitao na hii mara nyingi husababishwa na tamaa zenu wanawake hasa kwenye masuala ya fedha.
 
Kaona kuna kitu hapo hawezi kukirekebisha hata baada ya kurudisha penzi upya. Yaani kuna upungufu ameuona na unao toka mwanzo ila hapo kati alirudisha mapenzi aone kama itarekebishika ila kaona hakuna kitu bora ajiondoe mapema
Duh! wanaume?!
 
Lakini mimi nilimwita nikamwambia kwa ustarabu kabisa na bado akakataa, kinachoniumiza mimi ni kwanini hakuniita kama mimi nilivyofanya awali badala yake from nowhere akanicall kwamba mimi na yeye basi. Anyway asante kwa usahuri!
Daaah kweli dada umechanganyikiwa mpaka ushauri unasema usahuri
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…