Naomba ushauri wako, nahitaji kulima mihogo

mapipando

JF-Expert Member
Jun 8, 2015
2,922
3,559
Habari za muda huu wanafamilia ya Jamii Forum na heri ya mwaka mpya pia,

Wakuu,kipato hakikidhi mahitaji ya muhimu na msingi hasa kwa kutegemea mshahara.Hivyo nimeona naweza nikageukia kilimo ambacho kwa namna moja ama nyingine kinaweza kuniongezea hatua kadhaa mbele kiuchumi.
Kilimo chenyewe si kingine ni cha mihogo,nikiamini kwamba hakina complications sana kama vile close supervision,madawa,maji n.k
Nimetafuta na kupata eneo la ukubwa wa heka sita huko maeneo ya Bunju kwa Kibosha,sasa kwa wenye uzoefu wa kilimo husika pamoja na eneo husika pia,ningependa kufahamishwa mambo kadhaa kama ifuatavyo....

1. Je huu ni wakati sahihi kupanda mbegu ama nimechelewa?(nalenga kuvuna kipindi cha mwezi wa Ramadhani)

2. Magonjwa na dawa zake

3. Nini kifanyike/kizingatiwe ili zao likue ipasavyo na kutoa mavuno mazuri?

Nitashukuru sana kwa michango yenu wakuu.....!
 
Mihogo gani mkuu? kuna ya Jang'ombe, Kibandamaiti, mchambawima nk.zina mahitaji tofauti.
 
Lima me ni mnunuzi ujalewa andaa Shamba ila huwezi vuna ramazani ushachelewa utavuna mwezi wa kumi kuendelea
 
Lima me ni mnunuzi ujalewa andaa Shamba ila huwezi vuna ramazani ushachelewa utavuna mwezi wa kumi kuendelea
Nashukuru kwa mchango,je kwa huo mwezi soko linakuwepo zuri ama?
Na je ni aina gani ya mbegu inafaa zaidi mkuu?
 
Mihogo gani mkuu? kuna ya Jang'ombe, Kibandamaiti, mchambawima nk.zina mahitaji tofauti.
Mkuu hali sio nzuri,nafikiri ungeweka pembeni utani kisha uje na mawazo ya kujenga.
Bado nina imani na wewe...!
 
Back
Top Bottom