Naomba ushauri wa mgogoro wa njia

Naomba ushauri wa mgogoro wa njia

queenkami

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2010
Posts
1,857
Reaction score
1,407
Habari zenu wakuu.

Miaka kadhaa nilinunua kiwanja kikiwa kina njia 2 za kupita gari. Baada ya muda akauziwa mtu na kujenga uzio njia moja ikafa ilabaki moja. Njia iliyobaki nasikia napo panataka kuuzwa na madai ni kuwa hiyo sio njia eti ni kiwanja cha mtu.

Wakati nauziwa nilioneshwa kuwa hizo ni njia na ktk hati yangu ya serikali za mtaa inaonesha kiwanja kina njia 2.

Nafsi yangu inahuzunika sana nikifikiria jinsi ambavyo mchakato wa kudai haki yangu unayoenda kuniingiza kwenye uadui. So far sina adui wala sijawahi kugombana na mtu na ninatamani iendelee hivi ila nimejenga nyumba nzuri kubwa ya kisasa hapo lakini bila njia hiyo nyumba itashuka sana thamsni.

Wakuu nawaomba mnishauri njia nzuri ya hekima ya kukabiliana na changamozo hii.

Natanguliza shukrani🙏
 
Habari zenu wakuu.

Miaka kadhaa nilinunua kiwanja kikiwa kina njia 2 za kupita gari.Baada ya muda akauziwa mtu na kujenga uzio njia moja ikafa ilabaki moja.
Njia iliyobaki nasikia napo panataka kuuzwa na madai ni kuwa hiyo sio njia eti ni kiwanja cha mtu.

Wakati nduziwa nilioneshwa kuwa hizo ni njia na ktk hati yangu ya serikali za mzaa inaonesha kiwanja kina njia 2.

Nafsi yangu inahuzunika sana nikifikoria jinsi ambavyo mchakato wa kudai haki yangu unayoenda kuniingiza kwenye uadui.So far sina adui wala sijawahi kugombana na mtu na ninatamani iendelee hivi ila nimejenga nyumba nzuri kubwa ya kisasa hapo lakini bila njia hiyo nyumba itashuka sana thamsni.

Wakuu nawaomba mnishauri njia nzuri ya hekima ya kukabiliana na changamozo hii.


Natanguliza shukrani🙏
Pole mkuu umeshaenda ofisi ya ardhi kuwapa issue hii???
 
Dai haki yako hata kama unaona utaumiza watu , kama unaona haupendi kuumiza watu , jiandae kuumia wewe.

Note. Ila busara ya kwanza inaanza kwa kujijali wewe kwanza na wengine ndio wanafuata.
Itabidi tu nifanye hivyo mkuu.
Kwa kweli sio kila anayepigana vita ni mshari.
Nachukia magomvi basi tu
 
Squarter za uswazi humalizwa ngazi ya kata,aonanena balozi wa nyumba kumi
Cha kuchekesha sijui kuhuznisha mzee aliyeniuzia ndo balozi sasa.🤔
Cha kusikitisha mzee "ananipenda" kama mwanae na wakati najenga hapo alinifanyia wepesi kwenye mamvo mengi hadi mafundi akikua anagombana nao wakiniharibia au kuiba.
Siishi hapo ila siwezi kwenda huko bila kumuona "babq" na kumbebea chochote kitu.
Nawaza sana sijui izakuaje?
Natamani nipate haki yangu bila mimi na "baba" kugombana😭
 
Habari zenu wakuu.

Miaka kadhaa nilinunua kiwanja kikiwa kina njia 2 za kupita gari.Baada ya muda akauziwa mtu na kujenga uzio njia moja ikafa ilabaki moja.
Njia iliyobaki nasikia napo panataka kuuzwa na madai ni kuwa hiyo sio njia eti ni kiwanja cha mtu.

Wakati nduziwa nilioneshwa kuwa hizo ni njia na ktk hati yangu ya serikali za mzaa inaonesha kiwanja kina njia 2.

Nafsi yangu inahuzunika sana nikifikoria jinsi ambavyo mchakato wa kudai haki yangu unayoenda kuniingiza kwenye uadui.So far sina adui wala sijawahi kugombana na mtu na ninatamani iendelee hivi ila nimejenga nyumba nzuri kubwa ya kisasa hapo lakini bila njia hiyo nyumba itashuka sana thamsni.

Wakuu nawaomba mnishauri njia nzuri ya hekima ya kukabiliana na changamozo hii.


Natanguliza shukrani🙏
Muite surveyor apime kwa kutumia handheld receiver.
Akipata coordinates ataenda kuangalia kama kuna TP Drawing kwenye eneo lako na ilitoka lini.
Pia itaonyesha kama eneo lako lilikuwa surveyed na plots mipaka yake ipo vipi.
Pia utajua kama utahitaji kufanya amendment ya matumizi na mipkaka na pia kutengeneza leeway/easement.
Hatua ya kwanza, Surveyor.
 
Back
Top Bottom