Naomba ushauri, nitamkosa binti kisa kipato kidogo

Naomba ushauri, nitamkosa binti kisa kipato kidogo

Msema yote

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2013
Posts
448
Reaction score
301
Hodi kwa mara nyingine tena wana jamii,

Bila shaka mu wazima wa afya tele. Ndugu zangu nimekuja jukwaani hapa kwa mara nyingine nipate msaada wenu wa kimawazo ni kwa namna gani naweza kuvuka huu mtihani uliopo mbele yangu. Bila kupoteza muda nianze kama ifuaatavyo;

Mwaka 2103 nilipanga kuwa ifikapo 2104 nitaacha kazi na kujiajiri kwani nilipenda sana kufanya shuguli zangu binafsi tangu nikiwa mdogo(nilipenda kujiajiri), hivo basi ilipofika 2014 kweli nilifata taratibu zote za kuacha kazi na hatimaye nikaacha na kuamua kujiajiri Namshukuru Mungu mambo yanaenda vizuri japo changamoto zipo ila naamini ipo siku nitafika.

Kiukweli shughuli zangu bado siyo kubwa sana hivo napata mapato kidogo tofauti na kipindi nilipo kuwa mwajiliwa nilipokuwa nikilipwa pesa niyngi, Sasa tatizo liko hivi:

Kuna binti ambaye ninaye kwa muda wa miaka 4 sasa na mipango yetu ilikuwa mwakani tuoane lakini mpaka sasa nimekutana na vikwazo vingi sana ambazo kiukweli vinaniumiza na kufanya utendaji wangu wa kazi upungue.

Kiukweli binti aninipenda sana nami nampenda mno tatizo ni wazazi wake hawataki binti yao aolewe na mtu ambaye mwenye maisha kama yangu(maisha ya wastani tu), wanataka aolewe na mtu mwenye pesa na aliye mtumishi au muajiriwa katika kampuni yoyote kubwa.

Kwani binti yao kamaliza chuo mwaka jana sasa mzee wake alimtafutia mtu ambaye ni bosi katika shirika flani hapo Dar na anahitaji binti yake aolewe na huyo jamaa, kiukweli inaniuma sana mpaka inafika hatua najutia kujiajiri.

Binti anaonekana kutokukubaliana na wazazi wake na hataki kwenda Dar kwa huyo jamaa japo mzee wake kamwambia amemtafutia na kazi hivo anatakiwa aende kufanya kazi huko.

Sifa za wazazi wa binti ni kama ifuatavyo

1. Ni waajiriwa katika mashirika ya flani ya kigeni hapa Mkoani.

2. Ni kabila lingne tofauti na mimi

Naomba niishie hapa kwani naamini nimeeleweka, nachoomba nisaidiwe ushauri nini cha kufanya ili nifanikiwe kuwashawishi wazazi wa binti waniozeshe binti yao kwani nampenda sana
 
hueleweki, na haupati mke ng'oo..
 
kaka usilazimishe kitu i ur life.mungu atakupa anye kufaa kwa wakati wake.
 
Ushauri ni wewe kutafuta na kuwa na hela kumzidi huyo jamaa.
 
si umwache utafute mwingine... ukilazimisha kuoa huyo bibie utajuta kwa sababu akipata shida kidogo utasikia ndio maana wazazi wangu hawakutaka niolewe na wewe.....
marriage is not one night stand think and think again...... kama now anakuwa influenced na wazazi wake akiwa ndani ya nyumba bado wazazi watataka kuingilia maamuzi ya bibie .... fanya kitu kitakupa amani wewe basi
 
mwachie mwanamke hilo sebene kama anakupenda huyo atabaki kuwa wako tu.

invest brain yako kwenye shughri zako tu. always life is not fair at all haki iko mbinguni tu. mitiani ya maisha ndio kipimo cha akili.

dedication song: safari siyo kifo by akudo sound;
sikiliza mstari huu; mimi samaki makazi yangu bahari mnanipeleka jangwani nitaishi kweli?
 
Binti ndiyo ameshika hatima ya ndoa yenu asimamie tu msimamo wake mwishowe watakata tamaa wazazi wake ni swala la muda tu.Rafiki yangu mmoja maaneo ya Bukoba alimpenda dada mmoja Mnyarwanda na akamchumbia alikuwa anakaa TZ kwa dada yake aliyekuwa anakaa TZ lakini mmewe Myarwanda pia,walikataa kabisa asimuoe baada ya muda wakamkubalia,baada ya miezi kadhaa wakabadilisha uamuzi wao kuwa hawataki huyo dada aolewe wanataka asome,bahati mbaya kijana alikuwa amelipa mahali,nakumbuka ilikuwa jioni moja tukiwa kwenye ibada ilitangazwa uchumba umevunjwa na pesa zikarudishwa hapohapo madhabahuni kulikuwa na kilio kanisani kama mtu kafiwa.

Kweli binti akaenda kusoma jamaa yangu akakubaliana na hali, mimi nikaondoka zangu kwenda kusaka maisha maana naogopa umasikini kama ukoma. miaka kama sita yule jamaa alifanikiwa kupata no.yangu akanipigia simu akaniambia kuwa alifanikiwa kufunga ndoa ya yule binti na wana watoto watatu...

"wamtumanio Bwana hawatatahayarika kamwe"
 
mwachie mwanamke hilo sebene kama anakupenda huyo atabaki kuwa wako tu.

Invest brain yako kwenye shughri zako tu. Always life is not fair at all haki iko mbinguni tu. Mitiani ya maisha ndio kipimo cha akili.

Dedication song: Safari siyo kifo by akudo sound;
sikiliza mstari huu; mimi samaki makazi yangu bahari mnanipeleka jangwani nitaishi kweli?

shukrani sana kwa ushauri wako ndugu
 
Ukitaka ugali bwana chukua unga, chemsha maji upike. Habari ya kutafuta mahindi, upepete, uyaoshe ukaushe ukoboe. Najua miaka ilikuwa shauri ya chuo kwa sasa usaili moyo wako uone kama kilicho mbele yako ni kweli au la
 
aiseee ivi bado kuna wazee maboya kiasi iko............baba anamtaftia binti mtu wa kwenda kumla??????????????? msikilize binti ye ndo mwenye uamuzi wa mwisho saivi akuna mtu anayeuzwa bila ruhusa yake bana
 
aiseee ivi bado kuna wazee maboya kiasi iko............baba anamtaftia binti mtu wa kwenda kumla??????????????? Msikilize binti ye ndo mwenye uamuzi wa mwisho saivi akuna mtu anayeuzwa bila ruhusa yake bana

asante kwa ushauri
 


sihitaji mali, nahitaji ushauri juu ya kuwashawishi wazazi wa binti


Dogo usihangaike namna ya kuwashawishi wazazi wakubali ni ngumu kukusikiliza maana huna kipato, cha msingi wewe hangaika kumhakikishia huyo binti unampenda sana na utamuoa na asimamie maamuzi yake.

Bwana akifungua mlango hakuna wa kuufunga.



 
mpe mimba kama mshikaji alivyokushauri..wakimngangani tena katika hiyo hali waachie..
 
Back
Top Bottom