Naomba ushauri, nimwambie ukweli?

Naomba ushauri, nimwambie ukweli?

Unless ulidanganya kuwa hukuwahi kuwa na mtu kabla ya mumeo, sioni atakasirika vipi ukimwambia ukweli. Hata ukipata namna ya kuikwepa hiyo kazi, jamaa ameshajua uko wapi, so ataendelea kukusumbua tu.
 
Mungu hakukosea kusema ukweli humuweka mtu huru, na uhuru huo ndio unaoleta amani na faraja ndani ya mioyo ya wanadamu. Palipo na ukweli hamna mafarakano na mashaka. Nimefurahishwa sana na kitendo cha kumkwepa huyo X wako ili tu utunze heshima ya ndoa yako na wewe mwenyewe kwa ujumla.

Kama usiposema ukweli sasa hivi, Je ikitokea wao kwa wao wakaambiana unadhani mmeo atajihisi yupo salama kwako!? Na atafikiria kwanini muda huo hukumwambia. Unatmueka ktk hali kubwa sana ya mawazo.

Siku zote katika mapigano au katika mashindano ukimuona mtu amekushambulia na wewe ndo unajipanga ujue utamshambulia wapi. Hii ni indicator na umeoneshwa kuwa huu ni wakati muafaka wa wewe kufanya marekesho kwa Mme na X wako.

Ushauri wangu, mwambie mmeo ukweli wote kama ulivyoeleza hapa, na kama kuna mengine usisite kumueleza. Hata mume awe mkali vipi, kwa kesi ilivyo lazima atakusifu na kukuona wewe ni shujaa. Mueleze mmeo ukweli naye atakuelewa.

Nakutakia kila la heri!
Fuata ushauri huu!
 
Yaani wewe bado unampenda x wako. Sasa utamkimbia mpaka wapi? Unatakiwa ujifunze kufunga mafaili. Ila nakuheshimu kwa kujitambua udhaifu wako, Na kukimbiza bawa lako lisivunjike.

Usimuambie mumeo, itamuumiza sana especially kwa vile huyo rafiki yake Hana nia njema Na wewe. Sikushauri kuchukua hiyo kazi.msihi mumeo muambie hauko comfortable kuanza kazi hapo.
 
Ukweli humuweka mtu huru.
Kheri asikie kweli kutoka kwako na mapema. Kuliko kuja kuskia kwa watu baadae.
Hatokaa akuamini tena hata umwambie Mungu Mmoja.
 
Kama mumeo hakukuta bikra anajua ulishabanduliwa, mwambie ukweli na umwambie hukufanya interview na ajira umepewa hiyo ni mbinu mbovu ya x wako ujue hilo. Hamnaga kazi ya ofa kwa usawa huu wa Magu, utakuja kulia rafiki. Kuna mdada huku analia boss anambandulia ofisini, we fanya mchezo uone
 
Ww pia kimeo kama ulikuwa na aliyepata transfer musoma mara huyo tena aisee


Ila sema tu ukweli kwa mume uwe safe
 
Asikuongopee mtu ukieleza jambo hili kwa mumeo inakula kwako. Muombe mumeo akutafutie kazi sehemu nyingine, kumbuka wapenzi huwa hawaachani bali wanatengana tu, ukiingia tu hapo umeliwa, imagine hujafanya interview lakini kakutengenezea mazingira ya kupata kazi!
 
We eleza ukweli, ila sema tu hapo kwn hiyo ofisi kuna "bosi mmoja" amewahi kukutaka ukamkataa ndio maana hutaki kufanya kazi hapo. Usimtaje kama ni huyo rafiki ya mumeo.
 
Kama mimi ndo ningekuwa mumeo nisingependa kusimuliwa hiyo story kabisa maana baada ya kunisimulia hamu ya kuonana na rafiki yangu itakata kabisa na hata wewe upendo wangu kwako utapungua for sure.
 
Mbona rahisi sana? Mweleze tu ukweli mume wako, mambo ya reaction yake yasikutishe maana mwishoni ataelewa kuwa wewe ni mkweli.
 
Hiyo movie kaianzisha Ibilisi, akitaka kuimaliza na matokeo mabaya yaani; wewe kurudiana na Ex wako, ndoa kuvurugika, ex kukuhamishia kwake/kukupangishia nyumba japo baadae atakutelekeza vibaya mno. Ili kuepuka hayo yote, fanya haya; kwa kuwa Ex ameshaonesha nia ya kukurudi tena, tafuta mda mzuri siku ya weekend, mkae wewe na mmeo umwambie kuwa unashukuru kwa yeye kukutafutia kazi ila hukwenda kwa interview wala hutaenda kufanya kazi pale kwa kuwa kabla ya kuoana naye miaka 2 iliyopita uliwahi kutoka na huyo boss(ex wako) halafu mkaachana, hivyo hutaweza kwenda kufanya kazi chini yake, hata hivyo msisitize kuwa ex wako atakusumbua ukifanya naye kazi kwani kitendo cha kudanganya kuwa umefanya interview wakati sio ni mbinu ya uongo ya kutaka kurudiana na wewe tena. KUMBUKA UNA NJIA 2 MBELE YAKO; BARAKA AU LAANA, BHASI FUATA BARAKA UPATE UZIMA (Kumbuka kusali kwanza).
 
Mwambie hali ilivyo kwani si alikukuta hayo mambo umeshaanza, atakuwa wa ajabu kama ata react differently! Ukimwambia utakuwa umeongeza point muhimu ya uaminifu wako kwake na hakika atakuthamini zaidi. Mwisho fanya tathmini za gharama ya kuficha hilo na kueleza hali halisi uone gharama zipi utamudu then uchukue maamuzi. Kama vyeti ni vyako, kazi utapata POPOTE na MUDA WOWOTE.
 
Kua mkwel mapema Ila swala la kutofanya interview baki nalo
 
Mwambie ukweli aiseee ataumia Ila utakusaidia pia x wako hana nia nzuri na wewe ni wazi anakutaka kwa nguvu zote ndo mana interview hujafanya na kazi umepata Kama kaweza kufanya hili anaweza kufanya lingine lolote ili akupate ikiwemo kumwambia mumeo ukweli wenye chumvi nyingi pia ili akuharibie bora wewe kuwa wa kwanza kumwambia ukweli mumeo
 
Siyo kila kweli inaweza kukuweka huru, unaweza kumuambia mume wako ikawa shida anaweza hata kupunguza upendo wake kwako hapa inategemea na tabia ya mume wako, wewe fanya kazi huyu bos mpe kufuli kila mahali, ukimwambia mumeo siku bosi labda kakupa kazi ya kukuchelewesha mumeo hata kuwa na amani
 
Kwani MNA ugomvi na X boyfriend wako kiasi kwamba hamuwez kuwa watu wa kawaida?? Au bdo MNA pendana??? Mimi nadhani ungeanza kumdadisi mumeo...eg. Hivi sivi MTU anaaeza kufanya kazi na x wake?? Ili umsome reaction yake kabla huja muambia. Ila kila kitu kina suluhisho. Usiogope.
 
Back
Top Bottom