Naomba ushauri, nimwambie ukweli?

Naomba ushauri, nimwambie ukweli?

Kwa nisivopenda kumficha mtu wangu kitu ningemwambia tu ukweli ili niwe huru zaidi... Likitokea la kutokea atakua anajua kuliko kunyamaza kimya
 
Ukweli ndo utakuweka huru. Ukisubiri itakuwa mbaya zaidi. Umenikumbusha mchezo wa Jangala ambapo mwanamke alificha ujauzito wa mwanae na baadae ikawa huwezi kuendelea kuuficha. Mambo inabidi yawe hadharani. Ni hapo mumewe akamuulizia mke kwanini ulinificha kwamba binti yetu ana mimba. Mke alijibu niliogopa ungekasirika. Mume (Jangala) alimuuliza mke " Kwani sasa nilivyojua nimefurahi?".

Ukisema ukweli inaweza mume asifurahie kilichotokea lakini utakuwa umejijengea taswira ya kuwa mkweli siku za usoni. Ukinyamaza halafu ajue mwenyewe hatakaa akuamini kamwe. Maamuzi ni yako.
 
Bora umwambie ukweli tu maana si kosa lako.ukiendelea kuficha atakuja agundue na italeta shida sana
 
Mwambie ukweli kazi zipo watu wanahama toka kazi moja kwenda nyingine. Angalia usijefanya yale ya muwa kuufanya fimbo ya kutembelea...
 
Back
Top Bottom