Naomba ushauri, nataka kuanza biashara ya kuosha Magari (Car Wash)

Feb 5, 2017
37
72
Mimi ni kijana mpambanaji, baada ya kupambana sana na kazi ya bodaboda kwa muda mrefu sasa nahitaji kuiacha na kufanya mishe nyingine, katika kuwaza sana kipi naweza kukifanya nikapata wazo la kufungua car wash.

Katika tembea zangu kuna sehemu kuna car wash ambayo jamaa ameshindwa kuiendesha kutokana na changamoto za mhusika mwenyewe, kuulizia nikaambiwa kodi yake ni 300,000 kwa mwezi na unatakiwa kulipia miezi 6 ambayo inakua ni 1.8m.

Hapa mfuko wangu unasoma 3ml.

Lengo la kuja kwenu ni kuomba ushauri kwa wenye uzoefu wa hii biashara ya car wash, je kwa pesa hii niliyonayo ninaweza fanikisha kuanza biashara hiyo?

Je kodi hiyo ipo sawa katika kazi hiyo? Ni vifaa gani napaswa nianze navyo?

Ni kipi napaswa kukijua zaidi kabla sijaingia huko, karibuni wana jamvi tujadili na kupeana madini ili tupate kujikwamua na kupata kusonga mbele.

Na mwenye idea nyingine ya mtaji kama huo naomba anaisaidie kunijuza ili nipate kufungua ubongo. Asanteni
 
Fanya tafiti ujue kwanini jamaa kashindwa kuiendesha.
Vifaa anakuachia au utaanza na vyako?

Vifaa natakiwa kutafuta vya kwangu, jamaa hakua na vifaa zaidi ya mipira tu, nilichokiona na kuhisi ni jamaa kutokuwa serious katika kazi hiyo maana ana muda mrefu maji alishakakatiwa kijana aliebaki anatumia kuchota maji kwenye ndoo, hapa anasubiria kumaliza mkataba wake tu.
 
Vifaa natakiwa kutafuta vya kwangu, jamaa hakua na vifaa zaidi ya mipira tu, nilichokiona na kuhisi ni jamaa kutokua serious katika kazi hiyo maana ana mda mrefu maji alishagakatiwa kijana aliebaki anatumia kuchota maji kwenye ndoo,hapa anasubilia kumaliza mkataba wake tu
Ok mkuu kama location inalipa jaribu kila kitu ni kuthubutu. Upatikanaji wa maji na umeme upo wa uhakika?
Vitu muhimu
-Mashine(hii ni bei not less than 1.2 nzuri)
-tank la maji (At least 3000L+)
-vacuum cleaner/woover
-vijana wa kazi( waaminifu sio vidokozi)
-viosheo kwa ujumla

Piga hesabu jumlisha na kodi halafu fanya maamuzi
 
Ok mkuu kama location inalipa jaribu kila kitu ni kuthubutu. Upatikanaji wa maji na umeme upo wa uhakika?
Vitu muhimu
-Mashine(hii ni bei not less than 1.2 nzuri)
-tank la maji (At least 3000L+)
-vacuum cleaner/woover
-vijana wa kazi( waaminifu sio vidokozi)
-viosheo kwa ujumla

Piga hesabu jumlisha na kodi halafu fanya maamuzi

Asante sana mkuu, kwa kunipa maono, kuhusu vijana waaminifu kwanza kabisa nitakuepo mwenyewe ili kusimamia shughur nzima, unaweza kujua bei ya tank hilo la 3000L,
Vacuum na woover ni mashine mbili tofauti? Bei zake zikoje, asante
 
Asante sana mkuu, kwa kunipa maono, kuhusu vijana waaminifu kwanza kabisa nitakuepo mwenyewe ili kusimamia shughur nzima, unaweza kujua bei ya tank hilo la 3000L,
Vacuum na woover ni mashine mbili tofauti? Bei zake zikoje, asante
3000 litre sio chini ya 450K tafuta hata used yapo(sina hakika sana na bei)
Woover na vacuum cleaner ni kitu kimoja.. mpya 230K na kuendelea.
Screenshot_20230305-121857_Gallery.jpg
Screenshot_20230305-121857_Gallery.jpg
 
Nina uzoefu wa hii kazi kwa miaka mitatu 3 sasa
-Mashine nzuri ni kampuni ya Edon, eagle na easy power yenye kuanzia PSI 2500 inauzwa 950,000/=
-Vacuum kwa ajili ya kuvuta vumbi hii inauzwa kuanzia 200,000 hadi 550,000/=
-Pollish kwa ajili ya interior hii inauzwa 8,000/=
-Brush kwa ajili ya kusugulia tairi hii inauzwa 5000/=
-Sabuni nzuri tumia ya maji kwa sababu ya unga si nzuri sana inapausha gari na vioo
-Tafuta vijana waaminifu muelewane utawalipaje kwa pikpiki,bajaji na gari

Muhimu hakikisha eneo liwe na mzunguko mkubwa linafikika kirahisi,huduma rafiki na maji ya kutosha. Kama utakuwa na swali usisite kunijuza nitakusaidia kufikia ndoto yako.
 
Nina uzoefu wa hii kazi kwa miaka mitatu 3 sasa
-Mashine nzuri ni kampuni ya Edon, eagle na easy power yenye kuanzia PSI 2500 inauzwa 950,000/=
-Vacuum kwa ajili ya kuvuta vumbi hii inauzwa kuanzia 200,000 hadi 550,000/=
-Pollish kwa ajili ya interior hii inauzwa 8,000/=
-Brush kwa ajili ya kusugulia tairi hii inauzwa 5000/=
-Sabuni nzuri tumia ya maji kwa sababu ya unga si nzuri sana inapausha gari na vioo
-Tafuta vijana waaminifu muelewane utawalipaje kwa pikpiki,bajaji na gari

Muhimu hakikisha eneo liwe na mzunguko mkubwa linafikika kirahisi,huduma rafiki na maji ya kutosha. Kama utakuwa na swali usisite kunijuza nitakusaidia kufikia ndoto yako.

Asante sana mkuu, hiki ni chakula cha ubongo umenipa, ndugu nisamehe maana sitaacha kukusumbua pindi nitakapo kuushibisha ubongo wangu, na mda si mrefu nakuja pm, asante sana
 
Nina uzoefu wa hii kazi kwa miaka mitatu 3 sasa
-Mashine nzuri ni kampuni ya Edon, eagle na easy power yenye kuanzia PSI 2500 inauzwa 950,000/=
-Vacuum kwa ajili ya kuvuta vumbi hii inauzwa kuanzia 200,000 hadi 550,000/=
-Pollish kwa ajili ya interior hii inauzwa 8,000/=
-Brush kwa ajili ya kusugulia tairi hii inauzwa 5000/=
-Sabuni nzuri tumia ya maji kwa sababu ya unga si nzuri sana inapausha gari na vioo
-Tafuta vijana waaminifu muelewane utawalipaje kwa pikpiki,bajaji na gari

Muhimu hakikisha eneo liwe na mzunguko mkubwa linafikika kirahisi,huduma rafiki na maji ya kutosha. Kama utakuwa na swali usisite kunijuza nitakusaidia kufikia ndoto yako.
Watu Kama nyinyi Ndo mnahitajika JamiiForums
 
Mimi ni kijana mpambanaji, baada ya kupambana sana na kazi ya bodaboda kwa muda mrefu sasa nahitaji kuiacha na kufanya mishe nyingine, katika kuwaza sana kipi naweza kukifanya nikapata wazo la kufungua car wash.

Katika tembea zangu kuna sehemu kuna car wash ambayo jamaa ameshindwa kuiendesha kutokana na changamoto za mhusika mwenyewe, kuulizia nikaambiwa kodi yake ni 300,000 kwa mwezi na unatakiwa kulipia miezi 6 ambayo inakua ni 1.8m.

Hapa mfuko wangu unasoma 3ml.

Lengo la kuja kwenu ni kuomba ushauri kwa wenye uzoefu wa hii biashara ya car wash, je kwa pesa hii niliyonayo ninaweza fanikisha kuanza biashara hiyo?

Je kodi hiyo ipo sawa katika kazi hiyo? Ni vifaa gani napaswa nianze navyo?

Ni kipi napaswa kukijua zaidi kabla sijaingia huko, karibuni wana jamvi tujadili na kupeana madini ili tupate kujikwamua na kupata kusonga mbele.

Na mwenye idea nyingine ya mtaji kama huo naomba anaisaidie kunijuza ili nipate kufungua ubongo. Asanteni
I dont advise on such a business. No future, kwamtaji ulionao you cannot make a difference maybe kama you really know what your doing. Fanya kitu ambacho una passion nacho ili usichime mtaji
 
I dont advise on such a business. No future, kwamtaji ulionao you cannot make a difference maybe kama you really know what your doing. Fanya kitu ambacho una passion nacho ili usichime mtaji
Sasa umeshauri nini Cha maana zaidi ya kumkatisha tamaa kijana anayetaka kupambana?
 
Back
Top Bottom