Naomba ushauri kuhusu kampuni ya Zola

Naomba ushauri kuhusu kampuni ya Zola

UWOGA=UMASKINI

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2013
Posts
2,400
Reaction score
1,017
Wanajamvi niko na tatizo nilichukua Sola ya ZOLA kwa kulipia kidogo kidogo kwanza awali nililipa 75000 then iliyobaki nalipa kwa mwezi sasa leo napiga HESABU nimeshalipa 550,000 halafu Leo naambiwa bado nadaiwa 320,000 hivyo ukijumlisha JUMLA unakuwa 870,000 zola yenyewe inawasha taa nne tu haina UWEZO wa KUFANYA kingine chochote

Sasa leo wananipigia simu wananiambia nisipolipa hiyo 320000 wanakuja ngoa mtambo wao

Nishaurini nifanyeje?

UMEME NINAO NA NI WA UHAKIKA
 
Upo kijiji gani?

Wasiliana na Wizara ya Mh. Makamba mpatiwe umeme, muachane na hao watu.
 
Ila umeme ninao na ni wa uhakika
Mlikubaliana jumla utalipa sh ngapi
Kwa kweli walinichanganya sana awali waliniambia 500,000 BADAYE nilipoongea na makao makuu wakaniambia 780,000 leo wananiambia 890,000 kumbuka zola yao inawasha taa nne haiwashi tv wala redio NB NINA UMEME
 
Nijuavyo mimi usipolipia taa zao haziwaki hata km wasipong'oa mtambo wao, hivo chamsingi fanya malipo kwa mujibu wa makubaliano yenu yaliyopo kwenye mkataba

Na kingine kama ukiwapigia sahivi na ukataka kumalizana nao lazima watakupangia kiwango kikubwa maana hapo we ndo unavunja mkataba
 
Ila umeme ninao na ni wa uhakika

Kwa kweli walinichanganya sana awali waliniambia 500,000 BADAYE nilipoongea na makao makuu wakaniambia 780,000 leo wananiambia 890,000 kumbuka zola yao inawasha taa nne haiwashi tv wala redio NB NINA UMEME
Nenda nao taratibu tu, waambie wakupe mkataba uliosaini nao awali nadhani utaonyesha kiwango unachopaswa kulipa, kama wako sahihi basi lipa tu umalizane nao ila kama hawako sahihi basi komaa nao.
 
Ila umeme ninao na ni wa uhakika

Kwa kweli walinichanganya sana awali waliniambia 500,000 BADAYE nilipoongea na makao makuu wakaniambia 780,000 leo wananiambia 890,000 kumbuka zola yao inawasha taa nne haiwashi tv wala redio NB NINA UMEME
Hakuna maaandishi?
 
Hao ni sawa na Engie MYSOL zamani wakiitwa MOBISOL na wote Makao Makuu yao ni Arusha. Cha kufanya NG'OA huo Mtambo wao tafuta Mteja uza, kisha nenda Polisi kachukue RB kwamba ULIIBIWA.

Wakija waambie uliibiwa na ulitoa taarifa Polisi waonyeshe RB,hapo watakuwa hawana ujanja wa kukufanya chochote, hao ni Wahuni na Majambazi tu kama wale MOBISOL(ENGIE MYSOL), wote ni Majambazi Baba Mmoja Mama Mbalimbali
 
Ungeendelea kutumia kibatari badala ya kuchukua huo mtambo wao unaowasha taa nne tu.
 
Ila umeme ninao na ni wa uhakika

Kwa kweli walinichanganya sana awali waliniambia 500,000 BADAYE nilipoongea na makao makuu wakaniambia 780,000 leo wananiambia 890,000 kumbuka zola yao inawasha taa nne haiwashi tv wala redio NB NINA UMEME
Kwa hiyo unataka kutuambia kuwa mlikubaliana kwa mdomo hakuna mkataba ambao umeanisha kiasi na muda wa malipo pamoja na mazingira mengine kama ikitokea umeshindwa kulipa au umepata majanga n.k.

Sasa basi kama ni hivyo utakua umekosea sana kuomba ushauri humu Kwa sababu wewe utakuwa ni bonge moja la kilaza na humu wamo GT sasa sijui wakushauri nini kwa uzembe wako mwenyewe.

Anyways ushauri wangu ni kuwa kubaliana na kila watakalo kuambia Kwa sababu wewe ni muhitaji na waswahili wanasema:

" ... Kila muhitaji ni Hanithi hata kama ni Rijali ... "
 
USHAURI JUU YA KAMPUNI YA ZOLA


Wanajamvi niko na tatizo nilichukua Sola ya ZOLA kwa kulipia kidogo kidogo kwanza awali nililipa 75000 then iliyobaki nalipa kwa mwezi sasa leo...
Kwani mkataba si unao?waking'oa vyombo vya kutoa haki vipo.
 
USHAURI JUU YA KAMPUNI YA ZOLA


Wanajamvi niko na tatizo nilichukua Sola ya ZOLA kwa kulipia kidogo kidogo kwanza awali nililipa 75000 then iliyobaki nalipa kwa mwezi sasa leo napiga HESABU....
LOoooh, mkuu 'Nani'? Jina lako linatatiza sana, na naona hata tabia yako ni ya matatizo tupu!

Lakini nkuulize hili: Kwani mkataba wa maandishi mliowekeana unasemaje? Fuata makubaliano hayo hayo mliyokubaliana toka mwanzo.
 
hao ni sawa na Engie MYSOL zamani wakiitwa MOBISOL na wote Makao Makuu yao ni Arusha. Cha kufanya NG'OA huo Mtambo wao tafuta Mteja uza,kisha nenda Polisi kachukue RB kwamba ULIIBIWA.Wakija waambie uliibiwa na ulitoa taarifa Polisi waonyeshe RB,hapo watakuwa hawana ujanja wa kukufanya chochote,hao ni Wahuni na Majambazi tu kama wale MOBISOL(ENGIE MYSOL),wote ni Majambazi Baba Mmoja Mama Mbalimbali
Pole mkuu...washawahi kukutenda?

Inasikitisha kuona matapeli kutumia mainstream media kufanya advertising kisha kuliza watu.. MYSOL wamejitangaza sana kupitia radio mawingu...JATU na Mr Kuku kadhalika.
 
USHAURI JUU YA KAMPUNI YA ZOLA


Wanajamvi niko na tatizo nilichukua Sola ya ZOLA kwa kulipia kidogo kidogo kwanza awali nililipa 75000 then iliyobaki nalipa kwa mwezi sasa leo napiga HESABU...
Waambie watoe mtambo wao mkuu...umeshapata umeme sasa hicho kisola cha kuwasha taa nne cha nini...?

Count your losses now and move on, don't pay them even a cent from now onwards....
 
Back
Top Bottom