Naomba ushauri kuhusu kampuni ya Zola

Naomba ushauri kuhusu kampuni ya Zola

Zola ni wahuni kama wahuni wengine.

Wanapaswa kushtakiwa mahali husika
 
Nimeshafika mahakamani kuwashtaki ZOLA, Ni matapeli. Mimi nimewalipa pesa waje kufunga mtambo wao. Wakapiga hela na mtambo sijafungiwa. Miezi 6 sasa.

Mwenye mawasiliano yao ya makao makuu naomba. Namba za simu, email na anuani ya posta
 
Pole mkuu...washawahi kukutenda?

Inasikitisha kuona matapeli kutumia mainstream media kufanya advertising kisha kuliza watu.. MYSOL wamejitangaza sana kupitia radio mawingu...JATU na Mr Kuku kadhalika.
Nawafahamu nami niliwalipa malipo ya awali Tsh.285,000 hao MYSOL waje wanifungie Sola wakaja kufunga.Sola ikakaa siku 26 haiwaki kila nikiwapigia simu wanaahidi kuja halafu hawaji,nikaanzisha Uzi humu JF kuomba ushauri,

kuna jamaa akajitokeza anaitwa KENGEMAJI99 alishawahi kufanya kazi na hao jamaa kwa miaka 5,akanipa ushauri kwamba nikaitoe Sola pamoja na TV yake nikaiuze kisha nikachukue RB Polisi.

Na ndicho nilichofanya,nikapata kama 1,400,000 hivi wakati mimi niliwalipa 285,000hivyo nikapata faida nono sana na jamaa KENGEMAJI99 nikampoza na 50,000!

Hiyo ilikuwa mwezi Mei,na mpaka sasa nimeshawapiga mitambo yao mingine miwili.Naendelea kufanya michakato ya KUWAIBIA zaidi
 
Hakika umebarikiwa. Unatoa shs 12000 kwa mwezi yaani 12000÷30=400.
Unalipa shs 400 kwa siku kwa taa 4.

Chukua mshumaa mmoja shs 400 halafu washa chmba kimoja. Mshumaa haumalizi saa 3 umeisha wakati zola ni usiku mzima kwa vyumba vinne.

Naona ungeendelea tu na zola
 
Ila umeme ninao na ni wa uhakika

Kwa kweli walinichanganya sana awali waliniambia 500,000 BADAYE nilipoongea na makao makuu wakaniambia 780,000 leo wananiambia 890,000 kumbuka zola yao inawasha taa nne haiwashi tv wala redio NB NINA UMEME
Komaa nao mwisho utaambiwa elfu 50
 
HUYU PUNGUWANI ALIFANYA MALI KAULI BILA MAANDISHI... NDIO MAANA AONA HAAYA KUJIBU...

VUNA ULICHOPANDA...
 
Hizi kampuni za kitapeli bado zipo tu tanzania pamoja na kuwa na umeme wa REA.hawa hawana tofauti na deci au pride na brac ni wanyonyaji mno.taa zao hazina ufanisi na usipolipa unapigiwa simu na namba mbalimbali zikikutaka ulipe.
 
Ila umeme ninao na ni wa uhakika

Kwa kweli walinichanganya sana awali waliniambia 500,000 BADAYE nilipoongea na makao makuu wakaniambia 780,000 leo wananiambia 890,000 kumbuka zola yao inawasha taa nne haiwashi tv wala redio NB NINA UMEME
Kwahiyo mnawasiliana kwa mdomo tiu hakuna sehemu ulipewa bei kwa maandishi? Kama ni kwa maneno tuu Lipa maana huna ushahidi wa bei ya hiyo Sola ya Zola.
 
Nimeshafika mahakamani kuwashtaki ZOLA, Ni matapeli. Mimi nimewalipa pesa waje kufunga mtambo wao. Wakapiga hela na mtambo sijafungiwa. Miezi 6 sasa.

Mwenye mawasiliano yao ya makao makuu naomba. Namba za simu, email na anuani ya posta
Aiseeee kumbe Asante kuniongezea points
 
Vipi kwani hauna mkataba? Labda tuanzie hapo

Nijuavyo mimi usipolipia taa zao haziwaki hata km wasipong'oa mtambo wao, hivo chamsingi fanya malipo kwa mujibu wa makubaliano yenu yaliyopo kwenye mkataba

Na kingine kama ukiwapigia sahivi na ukataka kumalizana nao lazima watakupangia kiwango kikubwa maana hapo we ndo unavunja mkataba
Wewe ni mwenzao nini yaani sola inawasha taa nne niwe nimeinunua karibia laki 9 na ushee halafu wewe unaona sawa kweli
 
Waambie watoe mtambo wao mkuu...umeshapata umeme sasa hicho kisola cha kuwasha taa nne cha nini...?

Count your losses now and move on, don't pay them even a cent from now onwards....
Thanks for the great idea 💡 be bless
 
Back
Top Bottom