Naomba ushauri kuhusu kampuni ya Zola

Naomba ushauri kuhusu kampuni ya Zola

Hii huduma alikuwa anaitumia bi mkubwa kipindi fulani but nadhani wao walijichanganya wenyewe maana ilikuwa kwa mwezi nalipa Tsh 10,000/= kama sikosei na jumla yao ilikuwa kama hivi 500K na point Ila baada ya kama miezi 30 wakamrithisha mama mtambo.

Sijafuatiliaga tena japo nasikia kukiwa na shida ya umeme wakiwasha inafanya kazi na kila baada ya muda wanatuma code zao kwa ajili ya kuruhusu huduma kuendelea.
 
Umeulizwa swali hapo huna mkataba nao hujajibu au umeamua kudanganya watu
 
Ila umeme ninao na ni wa uhakika

Kwa kweli walinichanganya sana awali waliniambia 500,000 BADAYE nilipoongea na makao makuu wakaniambia 780,000 leo wananiambia 890,000 kumbuka zola yao inawasha taa nne haiwashi tv wala redio NB NINA UMEME
Sasa kwa hela yote hiyo uliyo wanufaisha, huoni ungeingia mwenyewe dukani ungepata mtambo wa watt 100 wa kuangalia mpaka tv! Taa 10, unachaji simu masaa 24! nk!!!
 
Sasa kwa hela yote hiyo uliyo wanufaisha, huoni ungeingia mwenyewe dukani ungepata mtambo wa watt 100 wa kuangalia mpaka tv! Taa 10, unachaji simu masaa 24! nk!!!
Wewe acha tu ni kutokujua na hawa jamaa walikuja kwa lugha soft na ya kijanja sana ndo wakaniingiza mkenge zola yenyewe watt 40 kwa laki 9
 
Huu uhuni upo kila mahali na hiyo mikataba imekuwa ikighushiwa na kubadilishwa kwa kumsainisha mtu makaratasi mengi kwa style ileile iliyomkuta Msuva wa Wydad.

1.National Insurance Corp (NIC)
2.Bayport.
 
Back
Top Bottom