Habarini wenzangu,
Jamani mimi nimekutana na maswaibu makubwa sana hata sijajua namna ya kuyasuluhisha ndani ya moyo wangu.Nimekuwa nikisumbuana na mume wangu muda mrefu tokea tunaoana ila nimeendelea kumvumilia hadi tumezaa nae mtoto mmoja ambae kwa sasa ana miaka minne.
Wiki iliyopita sijajua mwenzangu kachanganyikiwa nini kaanza kunipiga wiki nzima bila sababu ya msingi kila akirudi anakuta nimelala na mtoto anaanza kunipiga hadi majirani wanakuja kuamulia siku ya nne alivyoanza tu kunipiga nikakimbia na kutorokea kwa wazazi kwa vile sio mbali sana na hapo tunapoishi na mume wangu kesi imeenda kwenye dawati la jinsia na wakanishauri nisimpeleke mahakamani kwa sababu kwa kosa lake hilo la kunipiga kila siku bila hata sababu angeshtakiwa kufungwa kuanzia mwaka mmoja hadi mitatu.
Niko bado kwenye kuona namna gani aadhibiwe mtu huyu na pia tulikuwa tumeshachokana sana.Cha ajabu leo nimeona siku zangu zimepitiliza kama wiki hivi ikanibidi nikanunue kipima mimba ili nipime kama ninayo au la, nilivyopima nikajikuta ninayo.
Uwiii mimi kwa mateso niliyoyapata kwa mwanaume huyu toka anioe sipendi kabisa kurudiana nae sasa kwa hali hii ya ujauzito wake nilionao nitafanyeje wadau yaani nimepanic nimekuwa kama kichaa maana akija kujua nina ishu yake hawezi kuniacha atanikomalia wakati mwanaume ni mtesaji kama polisi magereza.
Nakaribisha ushauri kwa pande zote maana nimedata. Nawaza je nitoe na sijui huwa wanatoaje mimba? Au je nilee mimba? Na nikiulizwa baba wa mtoto nani nikimtaja mume wangu atanirudia wakati ndo kwanza tumeachana.
Jamani mimi nimekutana na maswaibu makubwa sana hata sijajua namna ya kuyasuluhisha ndani ya moyo wangu.Nimekuwa nikisumbuana na mume wangu muda mrefu tokea tunaoana ila nimeendelea kumvumilia hadi tumezaa nae mtoto mmoja ambae kwa sasa ana miaka minne.
Wiki iliyopita sijajua mwenzangu kachanganyikiwa nini kaanza kunipiga wiki nzima bila sababu ya msingi kila akirudi anakuta nimelala na mtoto anaanza kunipiga hadi majirani wanakuja kuamulia siku ya nne alivyoanza tu kunipiga nikakimbia na kutorokea kwa wazazi kwa vile sio mbali sana na hapo tunapoishi na mume wangu kesi imeenda kwenye dawati la jinsia na wakanishauri nisimpeleke mahakamani kwa sababu kwa kosa lake hilo la kunipiga kila siku bila hata sababu angeshtakiwa kufungwa kuanzia mwaka mmoja hadi mitatu.
Niko bado kwenye kuona namna gani aadhibiwe mtu huyu na pia tulikuwa tumeshachokana sana.Cha ajabu leo nimeona siku zangu zimepitiliza kama wiki hivi ikanibidi nikanunue kipima mimba ili nipime kama ninayo au la, nilivyopima nikajikuta ninayo.
Uwiii mimi kwa mateso niliyoyapata kwa mwanaume huyu toka anioe sipendi kabisa kurudiana nae sasa kwa hali hii ya ujauzito wake nilionao nitafanyeje wadau yaani nimepanic nimekuwa kama kichaa maana akija kujua nina ishu yake hawezi kuniacha atanikomalia wakati mwanaume ni mtesaji kama polisi magereza.
Nakaribisha ushauri kwa pande zote maana nimedata. Nawaza je nitoe na sijui huwa wanatoaje mimba? Au je nilee mimba? Na nikiulizwa baba wa mtoto nani nikimtaja mume wangu atanirudia wakati ndo kwanza tumeachana.