Naomba ushauri, hivi huyu ananipenda kweli?

Naomba ushauri, hivi huyu ananipenda kweli?

Hahahaaaa..mkuu nimecheka sana kwa tabia za huyo jamaa a.k.a shemeji yetu.

Hizo tabia 50% zinafanana na zangu ila nilipomlizia hapo mwisho nikashusha pumzi "oooops kumbe sio mimi"..huyo atakuwa usalama wa taifa mkimbizi au mume wa mtu kamwacha mkewe kijijini
 
Bi dada unamjua husein bolt,,,kama unamjua fanya anachofanya
 
Ukikaachini Ukitafakari Kwa Makini Ulipomkubalia awe Mpenzi wako Ulijuaje au Uliaminije kua anakupenda na Ukamkubalia? Ukishagundua ulijuaje anakupenda na Ukamkubalia utakuwa umepetajibu kama anakupenda au Lah! Na ukifikiria kwa Makini yote anayokufanyia honestly Wewe Unaona Kweli anakupenda? Ukipata jibu Fanya maamuzi.
 
Kweli NEW AGE mna mapepo, yaani unatoa mimba tena 3 alafu unakuja kujisifu hapa 👮, haki ya nani do!!

Unavua chupi ovyo na kijana anaendelea kufaidi wewe unashindwa kufanya maamuzi course of your future. Eeh!!!!!!!!!!!!!!!

Kasema alimdanganya bana kua ana mimba,mara zote hizo tatu,ila actually hakua nazo.akua anamskilizia jamaa atasemaje.
 
Hatakuoa kwa sababu hawezi kuoa mwanamke aliyekwisha to a mimba tatu,uongo wako ndo umekuponza
 
Makubwaaa! Hakuna cha ndoa hapo hupendwi! Anakutumia muda ukiisha anasepa anakuacha na maumivu debe
 
Habari zenu wana jamvi,

Naombeni ushuri juu ya huyu boyfriend wangu sijui ananipenda au la? Tumekuwa kwenye uhusiano kwa miaka mitatu sasa, ana miaka 33,hajanitambulisha kwa mtu yeyote kwao hata rafiki pia,haoneshi dalili ya kutaka kuoa.

Sasa japo nikimwambia ananiambia ndio anafanya mipango,nyumbani kwake nimeshaenda na kulala pia hakuna dalili ya mchepko,ila ukitaka ugomvi shika simu yake.

Aliwahi kuibamiza na kuivunja simu yake samsung galaxy s5 kisa niliishika nikawa naangalia nikimuuliza anasema ananipenda, nimemdanganya nina mimba kama tatu zote ananipa hela anasema nikatoe sasa simuelewi anasema ananipenda , eti jamani hapo kuna mapenzi kweli.

Naomba ushauri wenu

ruksa kushikana na siyo kushikiana simu by the way huyo awez kukuoa anza kuweka mguu mmoja nje

By
wanga pesa
 
Mvumilivu hula mbivu,kwani umemshika na kamba mpaka ashindwe kuachana na wewe,huyo anakupenda ila kuna upepo anaangalia,usifanye papara kama Mungu kakupangia awe wako atakuwa tu.Unaweza kufanya papara ukakimbilia hao wanaotangaza kuoa fastafasta mwisho wa siku anakubadilikia kuchomoka ukashindwa ukabaki unaugulia maumivu na hapo ndio ukute mmesha zaa na watoto.Nakushauri endelea kuvuta subira,mambo mazuri hayataki haraka.
 
Kweli NEW AGE mna mapepo, yaani unatoa mimba tena 3 alafu unakuja kujisifu hapa í-½í±®, haki ya nani do!!

Unavua chupi ovyo na kijana anaendelea kufaidi wewe unashindwa kufanya maamuzi course of your future. Eeh!!!!!!!!!!!!!!!

rudi usome amesema anamdanganya
 
Hakuna kazi ngumu kama kushauri mapenzi, ukichoka utaondoka mwenyewe
 
mwambie unayo mimba nyingine dokta kasema hiyo kutoa million 5 akikupa azisha biashara achana nae huyo baba
 
Miaka mi3 hajakutambulisha kwa yeyote,haoneshi dalili ya kutaka kukuoa,hataki ushike simu yake,umedanganya una mimba anakupa hela utoe,bado unataka tukuthibitie kama kuna mapenz hapo!!!
Ok!Huyo ANAKUPENDA sana,tena usimuache!
Umefurahi ee???

Hahahahahaaa huwiiii
 
Hahahaaaa..mkuu nimecheka sana kwa tabia za huyo jamaa a.k.a shemeji yetu.

Hizo tabia 50% zinafanana na zangu ila nilipomlizia hapo mwisho nikashusha pumzi "oooops kumbe sio mimi"..huyo atakuwa usalama wa taifa mkimbizi au mume wa mtu kamwacha mkewe kijijini

Hill nalo neno, "usalama Wa taifa" maana hana dalili za mchepujo but haruhusu simu yake kutazamwa au kuguswa dah hiyo danger.
 
Back
Top Bottom