Erini Thomas
New Member
- Dec 21, 2018
- 1
- 0
Leo nimeenda NSSF kwa maana ninatarajia kupata asilimia 33.3% ambayo ni sehemu ya mshahara wangu niliokuwa nikipata kazini kwa mara ya mwisho, lakini baada ya kufika pale nikakutana na wahanga wenzangu wao wakiwa na furaha tele sambamba na tamko la Mhe, Rais, wakijua ya kuwa tunapewa michango yetu yote kwa mkupuo, nilipozunguka kwa pembeni kiasi chake nikakuta kundi la watu wakiliongelea hili suala kivingine tena, sasa ndugu zangu hili jambo sijalielewa hata na mimi pia ndio maana nimeona ni vema tusaidiane kimawazo maana sijaelewa kwamba nitapatiwa asilimia 33.3% ama nitapewa pesa zangu zote kwa mkupuo. Naomba msaada tafadhali