NAOMBA MSAADA WENU WANA JF JUU YA HILI!!!

UMUNYU

JF-Expert Member
Jan 28, 2017
685
484
Wadau naombeni mwongozo wa taratibu za kufuata kisheria ili nihamishe umiliki wa kiwanja toka kwa mtu aliyeniuzia ambaye ana ofa tu na mwingine ana hati kamili ya kiwanja.Ni taratibu gani napaswa kuzifuata kisheria ?MSAADA WANAJF
 
Kwanza nenda kwenye ofisi za serikali ya mtaa kujua hatma ya kiwanja kama kipo sawa na hakuna maingiliano na serikali, pili omba taarifa za mwenye kiwanja kujua kama ni mkazi au mliki halali wa kiwanja husika, tatu nenda na mwenyekiti, mjumbe au afisa ardhi katika eneo husika kudhibitisha eneo rasmi la mauziano, nne kama umeshapata maridhiano ya kuridhisha andaa nyaraka za makubaliano ya kimaandishi na wahusika yaani viongozi wa mahala hapo kama niliowataja hapo awali pamoja na mashaidi wako kadhaa, tano wekeni wino kwenye karatasi alafu utowe nakala za maandishi ubaki nazo. Na amini utakuwa umeshamaliza kila kitu cha muhimu na unaweza kumalizana na wahusika niliotaja kama wana chakuongeza kutoka udhuru wao kuja kukusaidia kwenye shughuli yako ya umiliki upya wa ardhi husika.
 
Kwanza nenda kwenye ofisi za serikali ya mtaa kujua hatma ya kiwanja kama kipo sawa na hakuna maingiliano na serikali, pili omba taarifa za mwenye kiwanja kujua kama ni mkazi au mliki halali wa kiwanja husika, tatu nenda na mwenyekiti, mjumbe au afisa ardhi katika eneo husika kudhibitisha eneo rasmi la mauziano, nne kama umeshapata maridhiano ya kuridhisha andaa nyaraka za makubaliano ya kimaandishi na wahusika yaani viongozi wa mahala hapo kama niliowataja hapo awali pamoja na mashaidi wako kadhaa, tano wekeni wino kwenye karatasi alafu utowe nakala za maandishi ubaki nazo. Na amini utakuwa umeshamaliza kila kitu cha muhimu na unaweza kumalizana na wahusika niliotaja kama wana chakuongeza kutoka udhuru wao kuja kukusaidia kwenye shughuli yako ya umiliki upya wa ardhi husika.
Asante sana kwa kunipa pa kuanzia katika suala langu!!Kiufupi hivyo viwanja vyote vimepimwa na serikali na hao ni wamiliki halali sema mmoja ana ofa na mwingine ana hati!Nilikuwa nina wadai pesa wameona bora wanilipe kwa kuuziana viwanja hivyo ninachotaka kujua ni namna ya kubadilisha hiyo hati na hiyo ofa zisomeke jina langu!Viwanja vipo kwenye maeneo mapya yaliyopimwa!!
 
Back
Top Bottom