Mtumaini Mungu
JF-Expert Member
- Aug 3, 2021
- 879
- 1,061
Naliinua na kulitukuza jina lako We Bwana, Baba Muumba wa vyote vyenye uhai na visivyo hai.
Habari zangu ndugu zangu, imekuwa karibu miezi miwili nikiwa kimya hapa jukwaani, sababu hasa za ukimya wangu ni maradhi yanayonisumbua na kunitesa kiasi kupelekea kutomudu majukumu yangu ipasavyo. Mwezi wa 11 mwanzoni nililazwa kutokana na maradhi ya vidonda vya tumbo.
Nikiwa hospital nilifanyiwa vipimo na kugundulika nina shida pia ya maambukizo kwenye sehemu ya mwisho ya utumbo ambayo imeungana na njia ya haja kubwa (Lakini madaktari wamenihakikishia sio saratani).
Ndugu zangu kwa sasa naendelea vizuri japo bado sijaruhusiwa kwasababu matibabu yanaendelea.
Lengo haswa la Mimi kufungua nyuzi hi ni kuomba MSAADA toka kwako wewe mwana JamiiForums mwenzangu, ninatakiwa kulipa gharama ya Tsh 91,200/= ili niweze kuendelea kupata matibabu na kuruhusiwa. Pesa hi ni sehemu ya gharama za matibabu (NIMESHINDWA KULIPA PESA YOTE).
NINAOMBA kwa yeyote ambaye anaweza kunikopesha pesa hii anikopeshe, NITAILIPA 30/12/2021, nipo tayari kuilipa na riba ya Tsh 15000/=.
Lakini pia endapo Mungu hajakujalia kuwa na pesa hii kwa pamoja, NINAOMBA mchango wa kiasi chohote ili nikamilishe malipo ya deni hili.
Nawasihii wapendwa msinisahau katika sala, dua na maombi yenu.
Kama una chochote na ungependa kunisaidia basi ninaomba tumia namba hii Ili kuwasiliana na Mimi mwenyewe, na pia kutuma mchango wako.
Mungu mwenyewe aliye mpaji na awabariki, awarudishie na kuwaongezea pale palipopungua.
Mtumaini Mungu
Mtwara, Tanzania.
SHUKRANI KWENU NYOTE.
Ninawashukuru kwa MSAADA wenu, nimepata MKOPO toka kwa mmoja wa wana JF.
Habari zangu ndugu zangu, imekuwa karibu miezi miwili nikiwa kimya hapa jukwaani, sababu hasa za ukimya wangu ni maradhi yanayonisumbua na kunitesa kiasi kupelekea kutomudu majukumu yangu ipasavyo. Mwezi wa 11 mwanzoni nililazwa kutokana na maradhi ya vidonda vya tumbo.
Nikiwa hospital nilifanyiwa vipimo na kugundulika nina shida pia ya maambukizo kwenye sehemu ya mwisho ya utumbo ambayo imeungana na njia ya haja kubwa (Lakini madaktari wamenihakikishia sio saratani).
Ndugu zangu kwa sasa naendelea vizuri japo bado sijaruhusiwa kwasababu matibabu yanaendelea.
Lengo haswa la Mimi kufungua nyuzi hi ni kuomba MSAADA toka kwako wewe mwana JamiiForums mwenzangu, ninatakiwa kulipa gharama ya Tsh 91,200/= ili niweze kuendelea kupata matibabu na kuruhusiwa. Pesa hi ni sehemu ya gharama za matibabu (NIMESHINDWA KULIPA PESA YOTE).
NINAOMBA kwa yeyote ambaye anaweza kunikopesha pesa hii anikopeshe, NITAILIPA 30/12/2021, nipo tayari kuilipa na riba ya Tsh 15000/=.
Lakini pia endapo Mungu hajakujalia kuwa na pesa hii kwa pamoja, NINAOMBA mchango wa kiasi chohote ili nikamilishe malipo ya deni hili.
Nawasihii wapendwa msinisahau katika sala, dua na maombi yenu.
Kama una chochote na ungependa kunisaidia basi ninaomba tumia namba hii Ili kuwasiliana na Mimi mwenyewe, na pia kutuma mchango wako.
Mungu mwenyewe aliye mpaji na awabariki, awarudishie na kuwaongezea pale palipopungua.
Mtumaini Mungu
Mtwara, Tanzania.
SHUKRANI KWENU NYOTE.
Ninawashukuru kwa MSAADA wenu, nimepata MKOPO toka kwa mmoja wa wana JF.