Naomba msaada wa kununuliwa gari la kubeba taka

john_selcius

Member
Jul 3, 2012
15
3
Mpendwa mwana JF,

Ninaomba msaada toka mtu yeyote au taasisi yoyote wa kununuliwa gari (tipa) lenye uwezo wa kuanzia tani saba na kuendelea liwe linaweza kubinua. Nimekusanya vijana Wilayani Mpanda mkoa wa Katavi, na kuunda kikosi kazi kinaitwa WASAFI HOME CLEANERS, tumepewa kazi na Halmashauri ya kuzoa taka kwenye kata moja ya Makanyagio.

Moja ya changamoto kubwa niliyo nayo ni gari la taka kwa kuwa magari hapa yanakodishwa kwa gharama ambayo kama kikundi hatuwezi imudu. Tumejikamua angalau kwa miezi minne. Tumefika mahali hatuwezi kuendelea na kazi kama hatutapata msaada huo.

Hivyo nakuomba msomaji wa JF na watu wote wenye nia njema na ajira kwa vijana, tusaidiwe kununuliwa au kupewa gari la kutusaidia kubeba taka baada ya kuzikusanya toka kwenye makazi ya watu.

Msaada wako utakuwa wenye tija sana kwani itatusaidia kuboresha kazi yetu hivyo kuongezewa maeneo zaidi jambo ambalo litasababisha kuongeza ajira kwa vijana wa kitanzania tulio wengi.

Tusaidie tuweze kusimama kwa miguu yetu wenyewe.

Tafadhali unaweza kutuma sms JF/Taka/Mpanda kwenye 0768 441 304 au wasiliana nami moja kwa moja. Pia unaweza PM.
 
Sisi ni wanunuzi wa magari ya aina yote kwa njia ya mtandao piga 0764 601903 tuongee
Mpendwa mwana JF, ninaomba msaada toka mtu yeyote au taasisi yoyote wa kununuliwa gari (tipa) lenye uwezo wa kuanzia tani saba na kuendelea liwe linaweza kubinua. Nimekusanya vijana Wilayani Mpanda mkoa wa Katavi, na kuunda kikosi kazi kinaitwa WASAFI HOME CLEANERS, tumepewa kazi na Halmashauri ya kuzoa taka kwenye kata moja ya Makanyagio.

Moja ya changamoto kubwa niliyo nayo ni gari la taka kwa kuwa magari hapa yanakodishwa kwa gharama ambayo kama kikundi hatuwezi imudu. Tumejikamua angalau kwa miezi minne. Tumefika mahali hatuwezi kuendelea na kazi kama hatutapata msaada huo.

Hivyo nakuomba msomaji wa JF na watu wote wenye nia njema na ajira kwa vijana, tusaidiwe kununuliwa au kupewa gari la kutusaidia kubeba taka baada ya kuzikusanya toka kwenye makazi ya watu.

Msaada wako utakuwa wenye tija sana kwani itatusaidia kuboresha kazi yetu hivyo kuongezewa maeneo zaidi jambo ambalo litasababisha kuongeza ajira kwa vijana wa kitanzania tulio wengi.

Tusaidie tuweze kusimama kwa miguu yetu wenyewe.

Tafadhali unaweza kutuma sms JF/Taka/Mpanda kwenye 0768 441 304 au wasiliana nami moja kwa moja. Pia unaweza PM.
 
Chama chenu kina wanachama wangapi?
Kimesajiliwa?
Kazi mmepewa kuzoa ghuba kupeleka dampo au pamoja na kukusanya taka kutoka kwenye dust bins zote na kufagia?
Mmepewa kazi ya kuzoa taka, ina maana pamoja na kukusanya ushuru wa taka/usafi ?
Mkataba mliopewa ni wa muda gani?
Mnalipwa kiasi gani kwa mwezi?

Tukipata majibu hapo ni rahisi kukushauri cha kufanya.
 
mm mwenyewe sijakuelewa unaomba upewe gari la kuzolea taka au unataaka kununua gari la taka?

au ulimaanishaje mkuuu unaomba usaidiwe ili baadaye kwenye makubaliano au mpatano yenu uweze kumrudishia mhsika pesa ya hilo gari au inakuwaje?
 
Chama chenu kina wanachama wangapi?
Kimesajiliwa?
Kazi mmepewa kuzoa ghuba kupeleka dampo au pamoja na kukusanya taka kutoka kwenye dust bins zote na kufagia?
Mmepewa kazi ya kuzoa taka, ina maana pamoja na kukusanya ushuru wa taka/usafi ?
Mkataba mliopewa ni wa muda gani?
Mnalipwa kiasi gani kwa mwezi?

Tukipata majibu hapo ni rahisi kukushauri cha kufanya.

Chama chetu kimesajiliwa. Tupo watano.
Kazi tulopewa ni kuzoa dampo zilizokuwepo kupeleka dampo kuu yapata kilomita tano nje ya mji. kazi ya pili ni kuzoa taka toka kwenye kaya za eneo tulokabidhiwa. Na tunakusanya ushuru, lakini ushuru ule haukidhi kurudisha gharama za mafuta, kukodi gari, kulipa vibarua na mahitaji mengine madogo madogo.
Hivyo kwa kuwa na gari letu tutakwepa gharama ya kukodi ili tubaki na gharama ya mafuta, vibarua na gharama nyingine ndogondogo.

Tunamkataba wa miaka mitatu.

Hatuna malipo yoyote toka serikalini bali tunatakiwa kuchangia sehemu ya ushuru tulioukusanya kwa Mkurugenzi. Kwa maana nyingine ile dhamana toka serikalini ya sisi kwenda kufanya kazi kwenye jamii, ndiyo tunayoitumikia. Iwapo nguvu kazi itakuwa nzuri kwa upande wa kupunguza gharama za matumizi kinachobaki ndicho faida ya chama.
 
Naomba kupewa gari na sio kununua. Na sio kuwa labda kuwe na makubaliano ya kurudishia mhusika pesa hapana. Naomba kupewa gari bure kwa maana ya kusaidiwa.
 
hahaah hebu jipange bro acha utani we nani unafikiri atakupa hela ya bure, ngoja nikusaidie kidogo kwa sababu mpo kama kikundi na mkataba wa kazi mnao na kikundi kimesajiriwa chukua usajiri wenu na mikataba wa halimashauri yenu nenda Bank zote, saccos, microfinance maana mnakidhi vigezo vingi nya mkopo narudia tena man mkopo hamna mtu atakupa hela bureee sawa nenda kaombe mkopo sio msaaada maana nyie mnafanya biashara na ikitulia hio mtapiga hela nzuri tu
 
hahaah hebu jipange bro acha utani we nani unafikiri atakupa hela ya bure, ngoja nikusaidie kidogo kwa sababu mpo kama kikundi na mkataba wa kazi mnao na kikundi kimesajiriwa chukua usajiri wenu na mikataba wa halimashauri yenu nenda Bank zote, saccos, microfinance maana mnakidhi vigezo vingi nya mkopo narudia tena man mkopo hamna mtu atakupa hela bureee sawa nenda kaombe mkopo sio msaaada maana nyie mnafanya biashara na ikitulia hio mtapiga hela nzuri tu
Asante kwa ushauri, lakini mi nimemaanisha katika ombi langu kuwa naomba. Na nina imani yupo mmoja kama si wengi wenye kushikwa na Mungu katika hili. Hivyo usichoke na usikate tamaa katika kutafuta namna ya kunisaidia, bila kujali nafanya biashara au la !!!
Yamkini tukifanikiwa katika biashara yetu, tutaongeza ajira, toka tano kwenda kumi, kutoka kumi kweda hamsini na kadhalika. Na katika mzunguko huo wa ajira tutaokoa wengi wanaojiingiza kwenye uovu kama madawa ya kulevya, ukahaba,na mengineyeo ili wote wamsifu na kulibariki jina la BWANA.
Kumbe basi yeyote atakayetusaidia takuwa ameshiriki katika kazi ya kuokoa jamii ya Kitanzania. Na atakuwa ameshiriki baraka za Mwenyezi Mungu.
Tafadhali naomba mtusaidie.
 
Haya ndio matatizo yenyewe kuwa na kikundi cha kujikwamua is a good thing. Lakini huyo aliyekupeni tender alitumia kigezo gani cha uhakika wa service delivery na wakati mshaanza kuchukua kodi za watanzania?

Wakati mnachukua tender mliwashawishi vipi kazi mtaimudu leo mtake kupewa gari la taka, kama serikari aina jinsi ya kukopesha makundi ya kijamii kujisaidia au kuja na mabenki yenye mkipo ya nafuu haya makundi hayawezi endelea.

If you ask me ningesema mnyan'ganywe tender kwa sababu kazi inaelekea kuwashinda matter of principles.
 
Chama chetu kimesajiliwa. Tupo watano.
Kazi tulopewa ni kuzoa dampo zilizokuwepo kupeleka dampo kuu yapata kilomita tano nje ya mji. kazi ya pili ni kuzoa taka toka kwenye kaya za eneo tulokabidhiwa. Na tunakusanya ushuru, lakini ushuru ule haukidhi kurudisha gharama za mafuta, kukodi gari, kulipa vibarua na mahitaji mengine madogo madogo.
Hivyo kwa kuwa na gari letu tutakwepa gharama ya kukodi ili tubaki na gharama ya mafuta, vibarua na gharama nyingine ndogondogo.

Tunamkataba wa miaka mitatu.

Hatuna malipo yoyote toka serikalini bali tunatakiwa kuchangia sehemu ya ushuru tulioukusanya kwa Mkurugenzi. Kwa maana nyingine ile dhamana toka serikalini ya sisi kwenda kufanya kazi kwenye jamii, ndiyo tunayoitumikia. Iwapo nguvu kazi itakuwa nzuri kwa upande wa kupunguza gharama za matumizi kinachobaki ndicho faida ya chama.

nimekuelewa. kutokana na maelezo yako inaonekana makusanyo ni madogo, sasa mkipewa gari, kwa kazi ya hasara kama hiyo mtawezaje kulitunza na kuliendesha kwa faida ili kesho muwe nayo mawili, keshokutwa matatu yasiyo ya kupewa? service, mafuta, malipo ya dereva? kumbuka mtu anapokupeni msaada anaangalia sustainability, mmejipanga vipi?
 
nimekuelewa. kutokana na maelezo yako inaonekana makusanyo ni madogo, sasa mkipewa gari, kwa kazi ya hasara kama hiyo mtawezaje kulitunza na kuliendesha kwa faida ili kesho muwe nayo mawili, keshokutwa matatu yasiyo ya kupewa? service, mafuta, malipo ya dereva? kumbuka mtu anapokupeni msaada anaangalia sustainability, mmejipanga vipi?
Nashukuru kwa kunielewa,kati ya vikundi tuliopewa kazi hizo wapo pia vikundi wenzetu wenye tatizo kama letu la uhitaji wa kitendea kazi kama hicho. Kwa hiyo, tumeshawahi zungumza nao kwa maana ya wao kuwa wateja kwa kukodi kutoka kwetu kama tutakuwa nalo.
Na kwa hesabu ya pamoja, tukaona na tunakubali kuwa endapo tutalipata tutaweza kumlipa dereva,hasa kwa kupitia kazi za wenzetu (Wazoa taka walio maeneo mengine ya Halmashauri, kama Kashauriri, Kichangani, Hospitali na Mpanda hotel).

Lakini pia, tunashindwa kuwa na kipato kwa sababu nguvu kazi(vibarua) ni ndogo kwa kutokana na ufinyu wa fedha, ambayo inaelekezwa zaidi kwenye malipo ya kukodisha gari. Kumbe basi kama tutakuwa na la kwetu ile pesa ya kukodi tutailekeza kwenye kuongeza kikosi kazi, na kwa jinsi hiyo tutawaendea wateja wengi kwa siku au kwa wiki.
Tuna wateja wa majumbani, viwandani (mashine za kukoboa na mbao), mahoteli, tunashindwa kuwafikia wote na kwa hesabu ya chini kama tumepiga kazi kwa hakika kwa msaada wa kitendea kazi kama hicho makisio ya makusanyo yasiyo ne deni ni laki saba kwa mwezi. Na kwa kuwa tuna malengo na ndoto ya kujitanua, tutahifadhi makusanyo ili kukidhi haja yetu.
 
Usijali, kila mtu hupita hatua fulani za maendeleo, na kila hatua yamkini kuna vikwazo vinavyoterajiwa au visivyoterajiwa. Muhimu ni kutafuta njia halali kushinda vikwazo.
 
Back
Top Bottom