Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 2,151
- 10,395
Habari wanabodi
Ni siku nyingine ya jumanne tulivu Hali ya hewa inaruhusu kufanya kazi hasa kwa wale waishio Kanda ya pwani.
Changamoto kubwa ni umeme hasa wengine ambao 95% ya kazi zetu zinahusiana na umeme
Nisiwachoshe,kichwa Cha habari kinajieleza,kwenu ndugu zangu wanasaikolojia, na wengine wenye changamoto kama yangu mnisaidie
Iko hivi ,binafsi Nina tatizo fulani la UHARAKA yaani Mimi kutaka vitu viende haraka haraka,
Kwa mfano nikiongozana na mtu barabarani hasa tukitembea kwa miguu mara nyingi naona kama hatembei,na mara nyingi watu kibao hunilaumu
Pia mtu akiniambia nimsubiri mahali mara nyingi tunaweza kukubaliana labda bàada ya nusu saa,lakini Mimi huwa nakwazika kuona mtu kachelewa lakini ukweli mtu anaripoti ndani ya muda husika
Yapo mengi,hata nikitongoza mwanamke huwa sipendi kuchelewa yaani inshort zisizidi siku mbili,kinyume na hapo ni kubwagana tu maana wapo wanaohisi sipo serious kwa UHARAKA wangu
Pia wengine huhisi nawachukulia poa au kuwafananisha na wale wakununua Hali ambayo tangu miaka mingi inanisumbua na kupelekea kukosa vitu sahihi
Lakini pia utendaji wa kazi ofisini kwangu,hapa sitaongea mengi,haraka zangu zimeleta manufaa kwa baadhi ya vitu ila kwa asilimia sabini nimeharibu
Mfano naagiza mzigo wa dukani kwangu ,lakini wakala anagundua mzigo wenye ubora haupo kwa wakati huo basi ananiambia kuwa labda nisubiri bàada ya siku kadhaa wiki n.k
Basi kipande hiki Cha kusubiri dah,kinanishinda basi matokeo yake unaletewa famba yaani mzigo hauna ubora kumbe ningesubiri ningepata kitu quality na bei ya chini ila Sasa
Majuto ni mjukuu.
Yapo mengi,nilinusurika ajali,kwa kulazimisha kuendesha gari ambayo fundi kadai turekebishe brake system,mi nikaona weeee usinicheleweshe nisiwahi mizunguko yangu kisa brake wakati inashika kumbe ni kwenye speed ya chini.what's happened, pengine nisingeandika kitu hii Leo
Pia,vijana wangu wa kazi nimewapunguza wengi kwa kuona hawafai ila bàada ya kutoka lile gap hunijulisha kuwa nimeshindwa kufanya maamuzi sahihi
Kitaalauma Mimi ni architecture yaani msanifu wa majengo nikiwa kijana mdogo sijisifii ila nimewahi kupata heshima na hata kipato Cha kueleweka .kwenye kazi hii
kabla sijaacha na kugeukia mishe zingine
Ila kilichokuwa kinanigharimu Kila nikikosea jambo kwenye mambo mengi ilikuwa ni UHARAKA yaani mtu anakwambia wewe unajua Tena sana tatizo umeharakisha
Haraka,haraka,haraka,yaani UHARAKA
Kuna jambo huwa najilaumu hadi Leo,Kuna mwaka nilimtafuta kijana wa kunitengenezea mashine fulani,na huyo dogo nililetewa na mshikaji mmoja akanihakikishia kuwa ni fundi mzuri,
Basi bwana dogo kafika,kaanza kazi kahangaika nayooooo,Hadi zikakatika siku mbili nikaona humu hamna fundi kwa haraka zangu nikampigia yule aliyemleta nimweleze kuwa huyu dogo hamna kitu
Jamaa alinihakikishia kuwa nimpe muda ,mi nikaona wasinichezee wanapeana michongo tu Hawa nikamtimua,lakini dogo alinambia tatizo yeye kasoma mashine za kitaliano na hizi za kichina zimetofautiana
Hivyo nimpe muda , nikamwambia aondoke tu, Cha ajabu nilileta mafundi 26 walishindwa nikaanza kuzunguka nayo Sasa kuwapelekea mafundi wengine ikawa holla mwaka ukakatika nikakata tamaa
Siku Moja my wife akaniambia Kuna kampuni Moja Iko pembeni ya mji kasikia Kuna fundi hashindwi kitu,kuhusu hizi mashine
Mie huyo haraka haraka nikaipeleka ,kufika kule hamadi nakutana na dogo yule fundi wa mwanzo Tena akiwa msafi kuliko kipindi kile yaani anatoa maelekezo tu kwa mafundi wenzie
Basi aliponiona alitabasamu hasa bàada ya kugundua nipo na ile mashine kufumba na kufumbua bàada ya masaa manne nilikabidhiwa chombo kikiwa safi nikajilaumu
Kwanini sikumpa muda,halafu kijana wa watu ni mstaarabu si mtu mwenye kujiona
Tatizo langu wanabodi matatizo yangu huwa ni yenye kujirudia,tatito ni nini?
Kitu siwezi kuficha ni kwamba nakunywa pombe Wala sijifichi
Tena mnywaji mzuri tu,nimebainisha hili ili niwape uwepesi pa kuanzia
Wenye mawazo yenye tija, ushauri mzuri mnakaribishwa
Ahsante sana.
Ni siku nyingine ya jumanne tulivu Hali ya hewa inaruhusu kufanya kazi hasa kwa wale waishio Kanda ya pwani.
Changamoto kubwa ni umeme hasa wengine ambao 95% ya kazi zetu zinahusiana na umeme
Nisiwachoshe,kichwa Cha habari kinajieleza,kwenu ndugu zangu wanasaikolojia, na wengine wenye changamoto kama yangu mnisaidie
Iko hivi ,binafsi Nina tatizo fulani la UHARAKA yaani Mimi kutaka vitu viende haraka haraka,
Kwa mfano nikiongozana na mtu barabarani hasa tukitembea kwa miguu mara nyingi naona kama hatembei,na mara nyingi watu kibao hunilaumu
Pia mtu akiniambia nimsubiri mahali mara nyingi tunaweza kukubaliana labda bàada ya nusu saa,lakini Mimi huwa nakwazika kuona mtu kachelewa lakini ukweli mtu anaripoti ndani ya muda husika
Yapo mengi,hata nikitongoza mwanamke huwa sipendi kuchelewa yaani inshort zisizidi siku mbili,kinyume na hapo ni kubwagana tu maana wapo wanaohisi sipo serious kwa UHARAKA wangu
Pia wengine huhisi nawachukulia poa au kuwafananisha na wale wakununua Hali ambayo tangu miaka mingi inanisumbua na kupelekea kukosa vitu sahihi
Lakini pia utendaji wa kazi ofisini kwangu,hapa sitaongea mengi,haraka zangu zimeleta manufaa kwa baadhi ya vitu ila kwa asilimia sabini nimeharibu
Mfano naagiza mzigo wa dukani kwangu ,lakini wakala anagundua mzigo wenye ubora haupo kwa wakati huo basi ananiambia kuwa labda nisubiri bàada ya siku kadhaa wiki n.k
Basi kipande hiki Cha kusubiri dah,kinanishinda basi matokeo yake unaletewa famba yaani mzigo hauna ubora kumbe ningesubiri ningepata kitu quality na bei ya chini ila Sasa
Majuto ni mjukuu.
Yapo mengi,nilinusurika ajali,kwa kulazimisha kuendesha gari ambayo fundi kadai turekebishe brake system,mi nikaona weeee usinicheleweshe nisiwahi mizunguko yangu kisa brake wakati inashika kumbe ni kwenye speed ya chini.what's happened, pengine nisingeandika kitu hii Leo
Pia,vijana wangu wa kazi nimewapunguza wengi kwa kuona hawafai ila bàada ya kutoka lile gap hunijulisha kuwa nimeshindwa kufanya maamuzi sahihi
Kitaalauma Mimi ni architecture yaani msanifu wa majengo nikiwa kijana mdogo sijisifii ila nimewahi kupata heshima na hata kipato Cha kueleweka .kwenye kazi hii
kabla sijaacha na kugeukia mishe zingine
Ila kilichokuwa kinanigharimu Kila nikikosea jambo kwenye mambo mengi ilikuwa ni UHARAKA yaani mtu anakwambia wewe unajua Tena sana tatizo umeharakisha
Haraka,haraka,haraka,yaani UHARAKA
Kuna jambo huwa najilaumu hadi Leo,Kuna mwaka nilimtafuta kijana wa kunitengenezea mashine fulani,na huyo dogo nililetewa na mshikaji mmoja akanihakikishia kuwa ni fundi mzuri,
Basi bwana dogo kafika,kaanza kazi kahangaika nayooooo,Hadi zikakatika siku mbili nikaona humu hamna fundi kwa haraka zangu nikampigia yule aliyemleta nimweleze kuwa huyu dogo hamna kitu
Jamaa alinihakikishia kuwa nimpe muda ,mi nikaona wasinichezee wanapeana michongo tu Hawa nikamtimua,lakini dogo alinambia tatizo yeye kasoma mashine za kitaliano na hizi za kichina zimetofautiana
Hivyo nimpe muda , nikamwambia aondoke tu, Cha ajabu nilileta mafundi 26 walishindwa nikaanza kuzunguka nayo Sasa kuwapelekea mafundi wengine ikawa holla mwaka ukakatika nikakata tamaa
Siku Moja my wife akaniambia Kuna kampuni Moja Iko pembeni ya mji kasikia Kuna fundi hashindwi kitu,kuhusu hizi mashine
Mie huyo haraka haraka nikaipeleka ,kufika kule hamadi nakutana na dogo yule fundi wa mwanzo Tena akiwa msafi kuliko kipindi kile yaani anatoa maelekezo tu kwa mafundi wenzie
Basi aliponiona alitabasamu hasa bàada ya kugundua nipo na ile mashine kufumba na kufumbua bàada ya masaa manne nilikabidhiwa chombo kikiwa safi nikajilaumu
Kwanini sikumpa muda,halafu kijana wa watu ni mstaarabu si mtu mwenye kujiona
Tatizo langu wanabodi matatizo yangu huwa ni yenye kujirudia,tatito ni nini?
Kitu siwezi kuficha ni kwamba nakunywa pombe Wala sijifichi
Tena mnywaji mzuri tu,nimebainisha hili ili niwape uwepesi pa kuanzia
Wenye mawazo yenye tija, ushauri mzuri mnakaribishwa
Ahsante sana.