Naomba msaada wa kitaalam viungo vyangu vya mwili vinakosa nguvu

Siri ya sifuri

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
2,018
1,508
Habari zenu wakuu,

Naomba msaada wa kidaktari, mimi mwana Jf mwenzenu ninatatizo la kiafya linalonipelekea kuhisi kwamba mwili wangu hauko timilifu kiutendaji, yaani mfumo wa fahamu unafanyakazi chini ya kiwango.

Ni hivi nimezaliwa nikiwa mzima wa afya sina tatizo lolote, ila baada ya kufikia umri kati ya miaka ishirini na ishirini na tano kuna tatizo la afya lilianza kujitokeza. Mwili wangu ulianza kupoteza nguvu na kunisababishia ulegevu wa viungo, nilishindwa kufanyakazi ngumu kwasababu nilikuwa nachoka mapema baadae maskio nayo yalianza kuwa mazito kusikia na sauti kupotea, yaani sauti ilikua inatoka kwa chini sana hata nikiongea kwa nguvu kiasi kwamba watu wengine wakawa wanapata tabu kusikia lakini sikuwa nikipata maumivu yoyote ya maskio wala kifua.

Baada ya kupata matibabu ya muda mrefu mahospitalini tatizo la mwili kukosa nguvu lilianza kupungua na baadae kuonekana kama limekwisha kabisa ,hata hivyo kwa upande wa maskio na sauti hali iliendela kuwa mbaya. Mpaka hivi sasa miaka karibia kumi toka nianze kuumwa na kupatiwa matibabu ya mara kwa mara bado sisikii vizuri na sauti inatoka kwa chini sana, yaani nikiongea kwa sauti ya kawaida naonekana kama ninaehema kwa nguvu bila kusema kitu lakini siumwi.

Nilishakwenda hospitali ya taifa Muhimbili, KCMC Moshi, Mnazimmoja Zanzibar na vituo kadhaa vya afya vya tiba mbadala na kote huko nimefeli kurekebisha hali ya maskio na Sauti.

Hata hivyo mara nyingi nilipokwenda hospitalini nimekuwa nikifuatilia huduma ya maskio na sauti ila sasa nataka nirudi tena mahospitalini kwa ajili ya vipimo ili niwezekujua chanzo cha tatizo, naamini likijulikana tatizo lilipoanzia kama ni kwenye Ubongo au Mishipa ya fahamu nawezakupata mafanikio na maeneo mengine.

Sasa naombe kujua ni aina gani ya vipimo ninavyoweza kupima na kujua hitilafu ilipoanzia ili nianze kutibu eneo hilo badala ya kupambana na maskio na sauti ambavyo huenda matatizo yake yanasababishwa na kiungo kingine ambacho ndicho kinachopasa kutibiwa.

(Natanguliza shukrani)
 
Asante saana mkuu, Je hapa jukwaani kwa kuanzia siwezi pata msaada wowote? maana nilitaka kujua kwanza chanzo cha tatizo kabla ya kuanza matibabu.
 
Naanza kupata wasiwasi juu ya wataalam wa afya ya mwanaadam waliomo kwenye jukwaa hili huru la Jf, ama hamna wataalam wenye ujuzi wakutosha au kama wapo basi hawana moyo wa kujitolea na au wapo kwa malengo yao maalum na si kwaajili yakusaidia na kama ndivyo basi inasikitisha sana.

Hivi mtu mwenye tatizo la kweli anawezaje kuomba msaada angalau kwa ushauri tu na akakosa!? Tuwe na moyo wa kujitolea wakuu na Mwenye-ez-mungu ndie mwenye kulipa kwa kila jema alitendalo mwanaadam na malipo yake ni bora zaidi...
 
Mkuu habari, tatizo la kutosikia vizuri ni changamoto mpya sikuhizi ni wengi sana wnashida hiyo na wao hugundua badae sana pindi wakisjindwa kabisa kusikia sehemu kubwa ya maneno.

chanzo cha masikio huwa ni matumizi ya earphone (za masikioni) na kuweka nyimbo kwa sauti ya juu zaidi kwa muda mrefu zaidi, ndio maana ukivaa earphone na uplay mziki mtu akikuita husikii.

Chanzo kingine ni sauti za mitambo na viwandani nazo ni iwapo tu utakuwa exposed kwa muda mrefu, pia kuna sababu isiyo rasmi ya matumizi ya dawa za Quinine ambazo nahisi serikali ilizipiga marufuku, hizo quinine zimeleta sama shida ya masikio kwani zinaua sama nerves za masikio.

sasa ukiwa na shida ya masikio kutokana na changamoto hizo lazima na sauti iwe ndogo sana, hii sio kama unashida ya sauti hapana hii ni kutokana unajitahidi kucontrol ukubwa wa sauti unayoongea yani wewe unajisikia sawa kabisa ila wengine wanaona unanong'ona na unahofia ukiongeza sauti basi itazidi na watu wote watasikia.......fanya mazoezi ya kuongea kwa sauti na usikike yatakusaidia.

tiba ya masikio kwakweli sidhani kama ipo (kitaalamu vipo vifaa maalumu pia kuna operation ya kuotesha nerves (vinyweleo vya masikio) Hii technology nahisi haijafika bado kwetu, pia unaweza tumia mchanganyiko wa Vitamins kwa dawa zinatengenezwa Arab kama sio misri zinaitwa Nurotons (kama nipo sahihi) hizo Nurotons zinahusika sana na uzalishaji wa nerves haswa hivo vinyweleo vinavyopatikana masikion ambavyo ndio vinapokea sauti na kuielewa sasa cases nyingi zipo neutral kuna wanaopona na kuna ambao hali haibadilili ila wote wanasema inaimprove sana.

Ila a good thing ni kwamba unaweza kuimprove hali yako ya kusikia kwa kufanya mazoezi kwa kiasi (usioverdo maana najua unashida ya kizunguzungu), kula matunda sana, kuondoa stress kwa maana ukiwa stressed ndio hata uwezo kidogo wa kusikia unapotea kabisa, pia kuwa na company ya watu wamaojua shida yako ili waweze kukuelekeza na kukufichia shida yako.

NB: Experience hiyo nilipata kwa roommate 2016 back yeye pia alijaribu tiba kama mafuta ya mzeituni na mdarasini, akajaribu pia mafuta ya kuku wa kienyeji ila hali ilibaki hivo, japo anasikia kwa sehemu kubwa sababu ya mazoezi nadhani na kula vizuri.
 
naimani nimeweza kukufungua kidogo, maswali naweza chelewa kujibu kwa sababu nitahitaji kumuuliza mhusika (sikuhizi hayupo tena Tanzania) ili nirudi kukuwekea anayopitia.
 
naimani nimeweza kukufungua kidogo, maswali naweza chelewa kujibu kwa sababu nitahitaji kumuuliza mhusika (sikuhizi hayupo tena Tanzania) ili nirudi kukuwekea anayopitia.
Asante mkuu, nashukuru sana umekuwa rafiki mwema kwangu, M/mungu akulipe yaliyo mema. Hii sababu ya matumizi ya dawa huenda ikawa na ukweli na ndio nilivyoaminishwa na wataalam wa afya wa mwanzoni kabisa kunihudumia.

Hata kama si quinine, wakati nikiwa bado mdogo niliwahi kuugua homa ya manjano pamoja na matete maji kwa pamoja, hii homa si yakufanyia mzaha hata kidogo hasa kwa watoto na dawa zake ni kali hasa na bila shaka tatizo lilianzia hapo ila kama ulivyosema madhara yake yanaanza taratiibu sana kiasi ambacho huwezi kutambua mapema unakuja kufaham wakati tatizo lishakuwa kubwa.

Nilishatumia vidonge vya multivitamin mara kadhaa hasa hivyo vyenye nembo ya nchi za kiarabu lakini hakuna jipya, pale muhimbili walipata kunishauri wanipe kifaa cha kukuza sauti (spiker)nitumie kama phone ila mimi mwenyewe nilikataa hiyo huduma nikaachana navyo. Nashukuru sana umeniongezea maarifa.
 
Asante mkuu, nashukuru sana umekuwa rafiki mwema kwangu, M/mungu akulipe yaliyo mema. Hii sababu ya matumizi ya dawa huenda ikawa na ukweli na ndio nilivyoaminishwa na wataalam wa afya wa mwanzoni kabisa kunihudumia...
Pole mkuu hata huyu rafiki angu hakuwa anatumia miaka yote mitayu ya chuo ila nahisi sahizi anatumia nje.....shida ya hizo hearing aid za brand mbovu ni kuwa zinaongeza sauti tu ila haziongezi efficiency yako kusikia (kama nipo sahihi) so hizo saiti zikiwa za juu kwanza masikio yanauma pili sauti hautasikia maana makelele yatakuwa mengi mwisho hata ule uwezo wa kusikia utarudi chini kwamaana utakiwa tegemezi sana kwenye vifaa....

Huwa napenda tafiti mambo meng youtube inasaidia.....

jitajidi ufanye mazoezi ili usijepata shida ya body balance (kitoweza uweka mwili katika usawa/ kushindwa kutembea vizuri) kuna uzi wa jamaa alielezea kwa undani sana magonjwa ya husuyo kichwa na milango ya fahamu nikiuona nitakutag
 
Dont feel down n kujiona hufai kaka ni wengi wenye tatizo hilo pia kila binadamu anaudhaifu wake, kuna wanaoshindwa tembea, hawazalishi, wengine hawaoni, wengine waathirika, wengine wafungwa maisha etc.

kila mtu anashida yake anayopitia inayomkosesha amani akiwa peke ake, jitahidi uishi hivyo ila ujipe furh na amani mwenyewe na kumtegemea Mungu kwamaana akiamua kukuponya hakuna wakuweka kizuizi.
 
Asante sana mkuu, pia namshukuru Mungu kwa kuniweka salama katika maeneo mengine, ni hulka tu kama si silika ya mwanaadamu inayonisukuma kuendelea kupambana kila ninapopata hisia ya kufanya hivyo. Kwa uwezo wa M/mungu maisha yanaendelea. Nashukuru sana kwa kunijali, kuwa na amani mkuu.
 
Asante sana mkuu, pia namshukuru Mungu kwa kuniweka salama katika maeneo mengine, ni hulka tu kama si silika ya mwanaadamu inayonisukuma kuendelea kupambana kila ninapopata hisia ya kufanya hivyo. Kwa uwezo wa M/mungu maisha yanaendelea. Nashukuru sana kwa kunijali, kuwa na amani mkuu.
Mkuu anytime am here bro ukifeel shida nikumbuke tujadili, kila binadamu anachangamoto kuwa huru.
 
Mkuu anytime am here bro ukifeel shida nikumbuke tujadili, kila binadamu anachangamoto kuwa huru.
Pamoja sana kaka, na hata wewe iwapo utapata chochote chenye manufaa ukinihabarisha litakuwa ni jambo jema. Na M/mungu ni mwingi wa malipo. (Irham manfil'ardh yarhamkum manfisamai--Wahurumie walio ardhin atakuhurumia alie mbinguni.
Tabaraka wataala--Mtukufu mwenye sifa njema.
 
Mkuu wewe ni Daktari? au unajitolea kwa yale tu ambayo M/mungu amekujaalia kuyajua? Mimi ni mtaalam kwenye ujenzi wa nyumba na mara kwa mara nakuwepo Daresalam ila Makazi yangu hasa ni Morogoro.
 
Mkuu wewe ni Daktari? au unajitolea kwa yale tu ambayo M/mungu amekujaalia kuyajua? Mimi ni mtaalam kwenye ujenzi wa nyumba na mara kwa mara nakuwepo Daresalam ila Makazi yangu hasa ni Morogoro.
hapana mkuu mimi sio daktari ni mwalimu tu, yes taarifa nazijua za baadhi ya magojwa mengi ya kichwa maana course hiyo nimeisoma mkuu.....

Hongera mkuu, usikate tamaa pambana na weka malengo yako vizuri, haluna kitakachozuia mafanikio yako, maana my friend sahizi ni amefanikiwa mara 3 kushinda mimi.....

Pia ninapofundisha kuna watoto 3 wanashida hii, wanatokea familia zenye mali nyingi ila wameshindwa waponya sema kwa watoto hawapo stressed wanaaamani na wapo vizuri sana kwenye masomo na sjughuli za ziada.
 
hapana mkuu mimi sio daktari ni mwalimu tu, yes taarifa nazijua za baadhi ya magojwa mengi ya kichwa maana course hiyo nimeisoma mkuu.....

Hongera mkuu, usikate tamaa pambana na weka malengo yako vizuri, haluna kitakachozuia mafanikio yako, maana my friend sahizi ni amefanikiwa mara 3 kushinda mimi.....

Pia ninapofundisha kuna watoto 3 wanashida hii, wanatokea familia zenye mali nyingi ila wameshindwa waponya sema kwa watoto hawapo stressed wanaaamani na wapo vizuri sana kwenye masomo na sjughuli za ziada.
Nashukuru mkuu, Rabbizidnii ilman warzuqniifahman--M/mungu akuzidishie elimu na akuongezee ufaham.
 
Back
Top Bottom