Samahani Daktari, naomba muda wako wa dakika mbili tatu tu

MR KUO

JF-Expert Member
Jan 8, 2016
2,399
3,250
Mwezi mmoja nyuma nilipatwa na hali ya kuumwa kwa, kuchoka mwili na homa ile ya watu wazima mwili hauchemki ila kwa mbali unajisikia hovyo, nikaenda maabala, nikapima mkojo, tyiphoid na malaria mara nyingi ndo magonjwa yanayonisumbua sana haya nikakutwa na typhoid na mkojo mchafu malaria haipo nikanunua dawa azuma nikameza dozi ikaisha nikajisikia kupona.

Ila baada ya wiki moja hali ikarudi, kuchoka na kujisikia hovyo, kukosa hamu ya kula n.k ikabidi niende maabala nyingine kupima vyote nikakutwa na malaria 10 pekee daah.nikashangaa haya maajabu. Isiwe kesi nikanunua dawa zile za 2000 nikameza hadi dozi ikaisha nikawa kama nimepona pia nikaendelea na shughuli zangu.

Sasa juzi hapa hali imerudi kama kawaida muda huu ninavyoandika hamu ya kula sina na mdomo ni mchungu balaa.

Naomba ushauri wako nini nifanyeje, dawa gani au vipimo gani nipime hadi nikae sawa.

Naomba msaada raia mwenzenu nikifa taifa linapoteza nguvu kazi na ninategemewa na watu sio chini ya watano.
 
Nenda kwenye maabara ya kueleweka, findings zake daktari akikuandikia dawa, usinunuwe dawa fake Nunuwa kwenye pharmacy za kueleweka pia.
Sijui uko wapi ningekushauri uende wapi.

By the way Una dalili zote za typhoid.
Niko morogoro mjini
 
Mbona kwa mbali naona ni primary infections za acute hiv stage.....vipi hujapa rashes ...... vipi ukima mate koo linauma uma kwa mbali.... je usiku unapata homa ....kama ndio pima na mzee wa kazi HIV
Dah.nje ya hayo niliyotaja hakuna mengine chief.hata uzito nilipima ni ule ule wa siku zote kg 65.3
 
Kinachoniuma ni kwamba Tanzania ni kazi sn Mtu kujua kuwa anaumwa ugonjwa fulani hasa kwa sisi watu wa chini.
Pole mkuu, ila fuatilia vizuri utapata ufumbuzi.
Na maabala zetu za kitapeli, imewahi kunikuta miaka kadhaa pia hii sio mara ya kwanza.ninepima malalia hakuna typod hakuna kuna mkojo tu ile namaliza dwa hali ikarudi nikahama maabala na kupima tena nikabikuta vyote.
 
Back
Top Bottom