Naomba msaada wa kisheria

airwing

JF-Expert Member
Dec 8, 2017
306
398
Habari?

Kuna changamoto niliipata na kampuni moja ya ukopeshaji mtandaoni.. Nilikopa kwao pesa 21/01- Na makubariano yalikuwa niwalipe siku ya tarehe 27. Ilikuwa siku ya tarehe 27 nikapokea simu kutoka kwao wakinikumbusha kulipa deni lao niliwajibu nipo njiani naendesha gari ila sikuhiyo hiyo ningekamilisha malipo.

Mchana wakanipigia tena, Nikawaambia nitalipa kabla ya tarehe 27 kugeuka, nimepata hitilafu ya tairi ninairekebisha ila nikifanikiwa kutoka hapo nitatafuta mpesa iliyokaribu nitafanya malipo.

Dakika chache baadae nikaanza kupokea simu kutoka kwa watu wangu wa karibu wakidai wanapokea message kutoka kwenye kampuni hiyo ikinituhumu mimi kuwa ni tapeli "mjanja mjanja" nisiyetaka kuwalipa pesa zao. Waliwashirikisha deni langu na taarifa zangu binafsi.

Nilijaribu kuwatafuta watoa huduma wao ambao niliwasiliana nao awali, inakuwaje?
Wakadai wakati najisajili huwa wanaingilia mifumo ya namba za simu za mteja, nikauliza pia mbona sijakataa kuwalipa deni lao! Wakanijibu shit.

Je kwa upande wa sheria ninaweza kuishtaki hii kampuni?

Kwa kunidharirisha kuniita tapeli
Kwa kuingilia mifumo yangu ya simu pasipo ridhaa yangu,
Kwa kunichafua kwa watu wangu wa karibu kwa kuniita mimi ni kitu ambacho sicho.
Ushahidi wa vyote ninao.

NB: Deni lao nililipa siku usiku kama ilivyo makubaliano
 
"....ilikuwa siku ya tarehe 27 nikapokea simu..." mara tena "......nikawajibu nitawalipa kabla ya tarehe 27" mara tena siku hiyo ya kuwalipa wakati naenda kwalipa njiani tairi la gari likaharibika.
ACHA BLAAAHBLAAH! LIPA DENI LA WATU! MXIUUUUUHH!
 
"....ilikuwa siku ya tarehe 27 nikapokea simu..." mara tena "......nikawajibu nitawalipa kabla ya tarehe 27" mara tena siku hiyo ya kuwalipa wakati naenda kwalipa njiani tairi la gari likaharibika.
ACHA BLAAAHBLAAH! LIPA DENI LA WATU! MXIUUUUUHH!
Makubaliano ya kwenye app hayakuwa katika muda fulani
Ila Hisivuke tarehe 27
Nilikuwa ndani ya muda ni ni halali kwangu kulipa mda wowote ule hata kama saa tano dakika 59 usiku...
 
Kama upo serious kabisa Mkuu tuwasiliane. Ila kwa haraka haraka una nakala ya makubaliano ya mkopo uliojaza online?, pili una jina kamili la kampuni husika?, tatu una statement ya mkopo na ya malipo?. Kama vipo vitasaidia jambo.
 
Uwe makini kunaswali hua linaulizwa kuhusu hao watu kama marafiki au ulionao kwenyesimu ,ukisema ndio umekwisha
 
Ukivunja laini hawakupati piga uwa garagaza therefore hii comment yangu haifundishi utapeli hilo lieleweke 🤞
 
Kama upo serious kabisa Mkuu tuwasiliane. Ila kwa haraka haraka una nakala ya makubaliano ya mkopo uliojaza online?, pili una jina kamili la kampuni husika?, tatu una statement ya mkopo na ya malipo?. Kama vipo vitasaidia jambo.
Hebu ngoja nihakikishe kama Vinatimia kwanza
 
Ukivunja laini hawakupati piga uwa garagaza therefore hii comment yangu haifundishi utapeli hilo lieleweke
Nia yangu ilikuwa kuwalipa na nilifanya hivyo ndani ya mda ule wa makubaliano
Tatizo ni pale waliyafanya hayo ili hali hakuna hujuma yeyote niliyowafanyia
 
Kwenye deni ni kulipa. Ila kama umechelewa masharti ni wao kukuongezea tozo na kukufungia usidai tena.
Mie wamewahi kunitumia tangazo la uongo kuwa natafutwa na polisi oystebay. Na mimi ikachakata wakaona niko polisi oysterbay. Na niko na fulani pale. Wakakaa kimya mpaka nilipolipa.
Huwa wanawapa wanaoitwa wakusanya madeni. Wala hakuna kutoshika. Siwezi kutupa namba yangu kisa nimekopa. Si mpaka nipate hela?
 
Habari?

Kuna changamoto niliipata na kampuni moja ya ukopeshaji mtandaoni.. Nilikopa kwao pesa 21/01- Na makubariano yalikuwa niwalipe siku ya tarehe 27. Ilikuwa siku ya tarehe 27 nikapokea simu kutoka kwao wakinikumbusha kulipa deni lao niliwajibu nipo njiani naendesha gari ila sikuhiyo hiyo ningekamilisha malipo.

Mchana wakanipigia tena, Nikawaambia nitalipa kabla ya tarehe 27 kugeuka, nimepata hitilafu ya tairi ninairekebisha ila nikifanikiwa kutoka hapo nitatafuta mpesa iliyokaribu nitafanya malipo.

Dakika chache baadae nikaanza kupokea simu kutoka kwa watu wangu wa karibu wakidai wanapokea message kutoka kwenye kampuni hiyo ikinituhumu mimi kuwa ni tapeli "mjanja mjanja" nisiyetaka kuwalipa pesa zao. Waliwashirikisha deni langu na taarifa zangu binafsi.

Nilijaribu kuwatafuta watoa huduma wao ambao niliwasiliana nao awali, inakuwaje?
Wakadai wakati najisajili huwa wanaingilia mifumo ya namba za simu za mteja, nikauliza pia mbona sijakataa kuwalipa deni lao! Wakanijibu shit.

Je kwa upande wa sheria ninaweza kuishtaki hii kampuni?

Kwa kunidharirisha kuniita tapeli
Kwa kuingilia mifumo yangu ya simu pasipo ridhaa yangu,
Kwa kunichafua kwa watu wangu wa karibu kwa kuniita mimi ni kitu ambacho sicho.
Ushahidi wa vyote ninao.

NB: Deni lao nililipa siku usiku kama ilivyo makubaliano
Pole kuna thread iliyopita kuna mdau pia umetoa malalamiko kama yako nafikiri ni vyema hizo MOBILE LOAN APP' zikaanza kuwa regulated na kutolewa ripoti juu ya matendo yao,pia nafikiri ni vyema kama hatujakopa pesa katika hizi Mobile Loans App kuhakikisha tunasoma TERMS & CONDITIONS zao kabisa na ikiwezekana Screenshot kabisa kwa ajili ya Record
 
Back
Top Bottom