Naomba msaada wa kisheria. Kesi ya kulawiti

Mhindih

JF-Expert Member
Mar 14, 2011
331
68
Habari wanaJF ni matumaini yangu hamjambo. Tafadhali naombeni msaada wenu.Nina mdogo wangu ana umri wa miaka 11 na miezi kama 8 hivi yuko darasa la 6 ametuhumiwa kesi ya kulawiti mtoto wa jirani yetu mwenye miaka 8 akiwa na wenzake watano. Januari mwaka huu alichukuliwa kwenda polisi tulipofika ndio tukaambiwa kuwa mnamo tarehe kati ya 24-27 mwezi wa 12 mwaka jana akiwa na wenzake watano walimlawiti mtoto mwenzao.Ikabidi tuulize kwa nini mlalamikaji amechelewa kutoa taarifa polisi? Tukaambiwa kuwa taarifa ilifika ila aliekuwa amefungua jalada alichukua likizo hivo sasa ndio ametoka likizo. Tukiwa police watoto walipigwa sana hadi kufikia mdogo wangu kukubali kuwa kweli alishiriki. Hapo police mama wa mtoto (mlalamikaji) alitoa cheti kutoka kwa daktari kuonyesha kuwa ni kweli alifanyiwa vitendo vya kinyama. Baada ya uchunguzi watoto 4 waachiwa kwa vigezo kuwa walio juu ya miaka 12 kesi itaenda mahakamani na waliochini ya miaka 12 wameachiwa.Kweli kesi imeenda mahakamani na tumeambia kesi itatajwa tarehe 6/3/2012. Naombeni msaada wenu wa kisheria ili nimsaidie dogo ukizingatia yuko shule na muda wa masomo anapoteza kwa ajili ya kufuatilia kesi. Nawasilisha samahani kwa maelezo marefu
 
Hilo chezo tu ongea vizuri na polisi hila usiwe mbahiri toa mpunga tu then muamishe dogo shule nyingine tena mkoa mwingine kabisa,polisi watazuga dogo amefungwa mchezo umekwisha,tanzania hii hata ukiua kama una kisu unatoka kesho yake!
 
Hilo chezo tu ongea vizuri na polisi hila usiwe mbahiri toa mpunga tu then muamishe dogo shule nyingine tena mkoa mwingine kabisa,polisi watazuga dogo amefungwa mchezo umekwisha,tanzania hii hata ukiua kama una kisu unatoka kesho yake!

Tayari kesi ipo mahakamani na itatajwa tarehe 6/3/2012
 
adhabu yake ni kifungo cha maisha jela, muulize babu seya atakuambia kuwa mimi sikudanganyi.
 
Ndugu Mhindih unahitaji kukutana na mtaalamu wa sheria ana kwa ana ili upate ushauri wa kitaalamu, maana hapo ninachokiona ni kwamba bado kuna mambo ambayo bado hujaya'disclose na ambayo yanaweza kuwa muhimu katika kutoa ushauiri unaoweza kumsaidia bwana mdogo. Mfano hujasema ni sehemu gani katika kituo cha polisi watoto walipewa kipigo maana nadhani kama ni hadharani usingekubali wapigwe. Maana hii ni kinyume na haki za watoto na haki za binadamu kwa ujumla [angalia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanazania ya mwaka 1977 ibara ya 13 - presumption of innocence na haki ya usawa mbele ya sheria]

Lakini yote kwa yote Sheria ya Mwenendo ya Makosa ya Jinai inawakataza polisi matumizi ya mabavu japo Sheria ya Ushahidi inaruhusu matumizi ya ushahidi uliopatikana kwa matumizi ya mabavu endapo mabavu yalisaidia kuweka wazi ukweli. Hivyo basi, kwanza, mtuhumiwa anaweza kukana maneno aliyokiri polisi kama alisukumwa kuyasema kutokana na kipigo, na lakini kukana huko kutakuwa na maana kama polisi hawatakuwa na ushahidi mwingine unaoweza kuonyesha kuwa alihusika. Pili kulingana na Kanuni ya Adhabu kuna presumption kwamba kijana wa kiume hana uwezo wa kujamiiana akiwa chini ya umri wa miaka 12 lakini hii inaweza kuthibitishwa vinginevyo.
 
Ndugu Mhindih unahitaji kukutana na mtaalamu wa sheria ana kwa ana ili upate ushauri wa kitaalamu, maana hapo ninachokiona ni kwamba bado kuna mambo ambayo bado hujaya'disclose na ambayo yanaweza kuwa muhimu katika kutoa ushauiri unaoweza kumsaidia bwana mdogo. Mfano hujasema ni sehemu gani katika kituo cha polisi watoto walipewa kipigo maana nadhani kama ni hadharani usingekubali wapigwe. Maana hii ni kinyume na haki za watoto na haki za binadamu kwa ujumla [angalia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanazania ya mwaka 1977 ibara ya 13 - presumption of innocence na haki ya usawa mbele ya sheria]

Lakini yote kwa yote Sheria ya Mwenendo ya Makosa ya Jinai inawakataza polisi matumizi ya mabavu japo Sheria ya Ushahidi inaruhusu matumizi ya ushahidi uliopatikana kwa matumizi ya mabavu endapo mabavu yalisaidia kuweka wazi ukweli. Hivyo basi, kwanza, mtuhumiwa anaweza kukana maneno aliyokiri polisi kama alisukumwa kuyasema kutokana na kipigo, na lakini kukana huko kutakuwa na maana kama polisi hawatakuwa na ushahidi mwingine unaoweza kuonyesha kuwa alihusika. Pili kulingana na Kanuni ya Adhabu kuna presumption kwamba kijana wa kiume hana uwezo wa kujamiiana akiwa chini ya umri wa miaka 12 lakini hii inaweza kuthibitishwa vinginevyo.

nimekuelewa mkuu. Vijana walipigwa wakiwa central police. Pia tulipoenda mahakamani siku ya kwanza dogo alikataa kuwa hajahusika na huo mchezo.
 
Nitasema kama mzazi! halafu na wewe fikiria kama mzazi! Hapa nafikiria scenerio moja tu ili kufupisha mazungumzo - nyingine zawezekana pia

Kweli ulawiti umetokea na mdogo wako kafanya hivyo! (Hii haimanishi kwamba mdogo wako hakuhusika na ulawiti huu - ya wezekana kabisa kundi lao zima wamesingiziwa na ulawiti huo ulitokea kwingine. Pili, yawezekana kabisa mdogo wako alishuhudia tu ulawiti huo ukitokea na mwisho yawezekana kabisa mdogo wako alikuwa kinara) Lakini kwa kuwa unatafuta wanasheria namba moja na mbili watayapembua kirahisi na kujenge utetezi ambao mdogo wako atakuwa huru. Ila iwapo namba tatu imetokea basi unakazi zaidi ya kulinda maslahi ya mdogo wako tu.

Cha kwanza kaa chini uongee na mdogo wako vizuri na kwa undani. Mtoe hofu na kumuahidi utamsaidia - (ingawa ingekuwa ni mimi mdogo wangu kafanya hivyo - kweli kabisa ningemuacha afungwe - afungwe afugwe- atapelekwa mahakama ya watoto kujifunza (ingawa pia katika jela zetu za sasa siamini kwamba sinamzaidia mfugwa kujifunza ubinadamu zaidi ya kumpa mateso). Ila wewe inaonekana unataka sheria imlinde mdogo wako hata kama anakosa - hiyo ni hiari yako na unahaki ya kuamua jinsi gani ungependa maslahi ya mdogo wako yalindwe. Sasa, ili mwanasheria aweze kumsaidia nilazima afunguke na itakuwa vyema kama atafunguka kwako. Nacho maanisha hapa, lazima ufungue nafsi yako na ukubali uhalisia na kosa iwapo mdogo wako katenda - si haki kutumia sheria tu kumaliza maswala ya ubinadamu.

Pili tafuta kuelewe kiini cha tabia hiyo katoa wapi - na basi kama anapaswa kuanza kubadilishwa afanyiwe hivyo. Maana mara nyingi, watoto wanaolawiti wenzao - mara kadhaa walishawahi kulawitiwa ama kushuhudia ulawiti wa aina hiyo - ama wanajihusisha na makundi ambayo yanafanya vitendo hivyo. Ama wengine ni misukumo ya miili yao - kwa hiyo ni vyema ungalie nje ya sheria tu. yawezekana kabisa unaweza kumlinda na sheria sasa lakini sheria ikamkamata baadaye. unaweza kumlinda na mtoto wa jirani baadaye akakamata wa ndugu! usijaribu kumaliza matatizo tu - fumbua na uwelewe tatizo ni nini? mtoto wa miaka 11 kupata wazo la kulawitii ni mapema sana - labda anaangali filamu za ngono! I will definetly be concerned with the sexual wellbeing of the young man!

Tatu, iwapo utajua ukweli, na kushauriana na mwanasheria wako - je unaweza kuwasialiana na mzazi wa mtoto aliyelawitiwa? Nadhani kunamichuko ya kibinadamu inapaswa kuangaliwa. Hata kama kesi inaendelea, na kama haitaingilia taratibu za kesi hiyo, kutoa pole kwa mzazi hata kwa mtoto pia ni jambo jema sana.

Hapa nataka ujiulize swali, iwapo mdogo wako angekuwa ni yeye kalawitiwa ungelifanyaje?
 
Nitasema kama mzazi! halafu na wewe fikiria kama mzazi! Hapa nafikiria scenerio moja tu ili kufupisha mazungumzo - nyingine zawezekana pia

Kweli ulawiti umetokea na mdogo wako kafanya hivyo! (Hii haimanishi kwamba mdogo wako hakuhusika na ulawiti huu - ya wezekana kabisa kundi lao zima wamesingiziwa na ulawiti huo ulitokea kwingine. Pili, yawezekana kabisa mdogo wako alishuhudia tu ulawiti huo ukitokea na mwisho yawezekana kabisa mdogo wako alikuwa kinara) Lakini kwa kuwa unatafuta wanasheria namba moja na mbili watayapembua kirahisi na kujenge utetezi ambao mdogo wako atakuwa huru. Ila iwapo namba tatu imetokea basi unakazi zaidi ya kulinda maslahi ya mdogo wako tu.

Cha kwanza kaa chini uongee na mdogo wako vizuri na kwa undani. Mtoe hofu na kumuahidi utamsaidia - (ingawa ingekuwa ni mimi mdogo wangu kafanya hivyo - kweli kabisa ningemuacha afungwe - afungwe afugwe- atapelekwa mahakama ya watoto kujifunza (ingawa pia katika jela zetu za sasa siamini kwamba sinamzaidia mfugwa kujifunza ubinadamu zaidi ya kumpa mateso). Ila wewe inaonekana unataka sheria imlinde mdogo wako hata kama anakosa - hiyo ni hiari yako na unahaki ya kuamua jinsi gani ungependa maslahi ya mdogo wako yalindwe. Sasa, ili mwanasheria aweze kumsaidia nilazima afunguke na itakuwa vyema kama atafunguka kwako. Nacho maanisha hapa, lazima ufungue nafsi yako na ukubali uhalisia na kosa iwapo mdogo wako katenda - si haki kutumia sheria tu kumaliza maswala ya ubinadamu.

Pili tafuta kuelewe kiini cha tabia hiyo katoa wapi - na basi kama anapaswa kuanza kubadilishwa afanyiwe hivyo. Maana mara nyingi, watoto wanaolawiti wenzao - mara kadhaa walishawahi kulawitiwa ama kushuhudia ulawiti wa aina hiyo - ama wanajihusisha na makundi ambayo yanafanya vitendo hivyo. Ama wengine ni misukumo ya miili yao - kwa hiyo ni vyema ungalie nje ya sheria tu. yawezekana kabisa unaweza kumlinda na sheria sasa lakini sheria ikamkamata baadaye. unaweza kumlinda na mtoto wa jirani baadaye akakamata wa ndugu! usijaribu kumaliza matatizo tu - fumbua na uwelewe tatizo ni nini? mtoto wa miaka 11 kupata wazo la kulawitii ni mapema sana - labda anaangali filamu za ngono! I will definetly be concerned with the sexual wellbeing of the young man!

Tatu, iwapo utajua ukweli, na kushauriana na mwanasheria wako - je unaweza kuwasialiana na mzazi wa mtoto aliyelawitiwa? Nadhani kunamichuko ya kibinadamu inapaswa kuangaliwa. Hata kama kesi inaendelea, na kama haitaingilia taratibu za kesi hiyo, kutoa pole kwa mzazi hata kwa mtoto pia ni jambo jema sana.

Hapa nataka ujiulize swali, iwapo mdogo wako angekuwa ni yeye kalawitiwa ungelifanyaje?

Nashukuru kwa maoni na ufafanuzi uliotoa ni mawazo mazuri, nitayafanyia kazi
 
Back
Top Bottom