mkuu siku nyengine usiandike jina langu kwenye kichwa cha habari kama ni message yangu tu tafadhali nitumie kama private msg sababu unazuia watu wengine kuchangia uzi huu.
kati ya hizo simu kuna hata moja unayo? haswa haswa hio galaxy s6 na A8 maana kwa muono wangu simu nyingi za around budget hio zinafanana na hizo, badala ya kukimbilia kununua simu mpya tunaweza tukazirekebisha hizo hizo. na zilipopata matatizo ulizipeleka samsung shop?
pia kuna jambo jengine muhimu unatakiwa ulijue, simu za maduka yetu kibongo bongo asilimia 90 sio mpya ni refurbished wanazitoa masoko ya korea, china na marekani kuja kuzitupa huku hivyo unaponunua simu Tanzania double check ni version ya Kimataifa ambayo huuzwa kwetu na pia utume imei yake kwenda namba ya samsung ili kuhakiki zaidi. mfano unakuta simu kainunua mzungu marekani huko ina tatizo kairudisha kwenye kampuni then inaenda kurekebishwa na kuja kuuzwa kwa bei nafuu, wafanya biashara wa bongo huzinunua zile simu nafuu na kuja kuziuza huku, kama unataka kuspend hela nyingi kama hivyo hakikisha ni version ya kimataifa, kuwa safe zaidi kanunue duka la samsung official.
kuhusu network, ikiwa ni simu ya nje ambayo wameunlock na sio iliotengenezwa kwa ajili ya Tanzania unaweza kupata Tatizo la network sababu modem yake ni Tofauti, pia simu za Alluminium hazishiki vizuri Network kutokana na material yake compare na za plastic, hivyo kama eneo lako lina shida ya network pendelea zaidi simu za plastic au kama zinakuwa na alluminium iwe ni frame tu na sio full body.
kuhusu ku overheart almost simu yoyote yenye perfomance kubwa itapata moto, unachotakiwa ni kufunga apps usipotumia au kuweka battery server ili kudownclock processor simu isipate moto.
kama hizo simu hapo juu huna tena unaweza subiri miezi kadhaa ikitoka s8 basi s7 zitashuka sana bei, samsung kuacha utengenezaji wa note 7 kumefanya thamani ya s7 isishuke hivyo itakuwa ngumu kuipata budget hio (japo inawezekana kuipata), sababu umeshatumia s6 sioni simu nyengine ya kukushauri zaidi ya s7 na flagship za mwaka 2016. sema kutokana na warranty za samsung Tanzania sioni maana ya kununua kampuni za brand nyengine ambazo hata service centre hawana, labda Huawei kidogo na simu kama Honor 8 kama wataileta itamake sense budget hio.